Tuesday, April 30, 2013

MWANTUMU BAKARI MAHIZA ATEULIWA KUWA SKAUTI MKUU TANZANIA

Mheshimiwa Mwantumu Mahiza.

























Na Mashirika Mbalimbali ya habari,
Dar es Salaam.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Mwantumu Bakari Mahiza kuwa Skauti mkuu nchini.

Kwa mujibu wa barua ya Katibu mkuu kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa, uteuzi wa Mahiza umeanza tangu Aprili 19 mwaka huu.

Mahiza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Kanali mstaafu Iddi Kipingu, ambaye amemaliza muda wake.

                                     Imetolewa na:

          Kaimu Katibu mkuu, Wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi.

GODBLESS LEMA ALIA NA POLISI, ASIMULIA JINSI WALIVYOMVAMIA NYUMBANI KWAKE

Umati wa watu ukiwa umejaa nje ya jengo la Mahakama Arusha, kusikiliza kesi ya Lema.



















Na Waandishi wetu,
Arusha.

MBUNGE wa Arusha mjini Godbless Lema kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) ambaye amechiwa huru kwa dhamana na Mahakama ya Hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa huo, amewataka wanachama wa chama hicho kumzomea mkuu wa mkoa wa Arusha Magessa Mulongo kila watakapomuona.

Pia Lema amesimulia jinsi alivyovamiwa nyumbani kwake, usiku wa kuamkia Aprili 26, mwaka huu.

Lema akiwa amefuatana na wafuasi na wanachama wa Chadema walikusanyika katika viwanja vya Ngarenaro ambako mbunge huyo aliwahutubia kwa dakika kadhaa na kuwataka wafuasi wake warejee nyumbani.

WANAFUNZI WAFARIKI DUNIA KWENYE DIMBWI LA MAJI

Na Mwandishi wetu,
Tarime.

WANAFUNZI wawili wanaosoma darasa la sita wilayani Tarime, wamekutwa na mauti baada ya kuzama katika dimbwi lenye tope na maji mengi.

Wanafunzi hao ni wa shule ya msingi Nyamwaga, katika kijiji cha Nyakunguru, kata ya Kibasuka wilayani humo.

MWALIMU MSTAAFU AFARIKI DUNIA KWA KUNYWA GONGO

Kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma, Deusdedith Nsimeki




















Na Steven Augustino,
Tunduru.

MWALIMU mstaafu katika kijiji cha Kidodoma wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma Rajab Mohamed Kalesi (65) amekutwa akiwa amefariki dunia baada ya kunywa pombe haramu ya gongo.

Mashuhuda wa tukio hilo akiwemo mdogo wa marehemu  Athuman Saidi walisema kuwa kabla ya mkasa huo, marehemu huyo alionekana akinywa Pombe hiyo kwa siku mbili mfululizo, huku akiwa amejificha katika nyumba ya muuzaji wa pombe hiyo Hamdi Swalehe.

Habari zinaeleza kuwa mwalimu huyo kabla ya kukutwa na mauti, alikuwa akiwa anatamba kuwa na fedha nyingi, alizokuwa ametoka kulipwa kama mafao ya kustaafu kazi hiyo.

Monday, April 29, 2013

WARIOBA: ITATOLEWA KATIBA YENYE MASLAHI YA TAIFA

Kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo (Jumatatu, Aprili 29, 2013). Kulia ni Katibu wa Tume, Assaa Rashid. (Picha na Tume ya Katiba)


















Dar es Salaam, 
Tanzania.

Tume ya Mabadiliko ya Katiba LEO imesema imejipanga kuandaa rasimu ya katiba itakayoweka mbele maslahi ya taifa na kuwaomba wananchi waijadili na kutoa maoni yao katika mabaraza ya katiba yatakayokutana kuanzia mwezi Juni mwaka huu (2013).

Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Jospeh Warioba amesema lLEO (Jumatatu, Aprili 29, 2013) jijini Dar es Salaam kuwa katika kuandaa rasimu hiyo, Tume yake haitapokea shinikizo kutoka taasisi, asasi, makundi au vyama vya siasa.

“Tume haitengenezi katiba ya vikundi au vyama, tunaandaa katiba ya nchi,” amesema Jaji Warioba katika mkutano wake na waandishi wa habari katika ofisi za Tume na kufafanua kuwa Tume inazingatia uzito wa hoja zilizotolewa  na wananchi na sio idadi ya watu waliotoa maoni.

Jaji Warioba amewataka wananchi kutokubali kutumiwa na makundi, asasi, taasisi na vyama wakati wa kujadili na kutoa maoni katika mabaraza ya katiba ya wilaya.

 Mabaraza ya Wananchi wenye ulemavu:

Akizungumza kuhusu ushiriki wa walemavu katika mabaraza ya katiba, Jaji Warioba amesema Tume yake inatarajia kuunda mabaraza ya Katiba ya watu wenye ulemavu ili kuwapa fursa walemavu kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kutoa maoni yao kuhusu rasimu ya Katiba itakayotolewa na Tume.

Hatua hii inafuatia ombi la Shirikisho la Vyama vya Watu wenye ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) na Umoja wa Watu wenye ulemavu Zanzibar (UWAZA) waliloliwasilisha kwa Tume.

Jaji Warioba amesema Baraza moja litaundwa Tanzania Bara na jingine Zanzibar na kwamba yatashirikisha wananchi kutoka ngazi ya chini ya wilaya hadi Taifa.

“Tunaelewa kuwa watu wenye ulemavu ni karibu asilimia 10 ya watanzania wote na mchakato huu hauwezi kuwatenga katika ngazi yoyote,” amesema Jaji Warioba na kuongeza kuwa taarifa ambazo Tume yake inazo zinaonyesha baadhi ya watu wenye ulemavu wamependekezwa na mitaa, vijiji, vitongoji na shehia kuwa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya.

 Chaguzi za Wajumbe Mabaraza ya Katiba ya Wilaya:

Aidha, Jaji Warioba amezungumzia mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika chaguzi zilizofanyika nchini kote hivi karibuni za kuchagua Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba kuanzia ngazi ya mitaa, vijiji, vitongoji na shehia.

Kwa mujibu wa Jaji Warioba, tathmini ya Tume inaonyesha kuwa kwa kiwango kikubwa viongozi na watendaji katika ngazi za vijiji, mitaa, shehia na kata walizingatia mwongozo uliotolewa na Tume na kuwa maeneo mengi wananchi walichaguana kwa amani na utulivu.

“Kwa mfano jumla ya shehia 323 sawa na asilimia 96.4 kati ya shehia 335 kwa upande wa Zanzibar zimekamilisha vizuri mchakato huu, hali kadhalika jumla ya Kata 3,331 sawa na asilimia 99.8 kati ya Kata 3,339 kwa Tanzania Bara nazo zimekamilisha mchakato wa kuwapata wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya kwa kuzingatia utaratibu uliotolewa kwa mujibu wa Mwongozo,” amesema Jaji Warioba.

Kuhusu hatua inayofuata baada ya chaguzi hizo, Jaji Warioba alisema Tume inaendela kupokea majina kutoka kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa na ya wananchi wote waliopendekezwa kutoka katika Kata na Shehia na kazi hiyo inatarajia kukamilika ifikapo tarehe 30 Aprili mwaka huu (2013).

Changamoto:

Akizungumzia kuhusu changamoto zilizojitokeza katika chaguzi hizo, Jaji Warioba amesema kuwa pamoja na mafanikio yaliyopatikana pia kulijitokeza changamoto kadhaa ambazo zilisabishwa na misimamo ya kisiasa na kidini

“Katika baadhi ya maeneo mikutano ya uchaguzi ngazi za vijiji, mitaa na shehia ilishindwa kufanyika kutokana na mivutano ya kisiasa na kidini zilizosababishwa na baadhi ya wananchi kufangamanisha chaguzi za Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya na masuala ya kisiasa na kidini,” amesema Jaji Warioba.

Jaji Warioba ametaja changamoto nyingine kuwa ni pamoja na baadhi ya wananchi kujiingiza katika vitendo vya rushwa katika chaguzi hizo ili wapendekezwe kuwa wajumbe wa mabaraza hayo ya katiba.

 “Tumepokea pia malalamiko ya vitendo vya rushwa,” alisema Mwenyekiti huyo na kusema vitendo hivyo ni kinyume cha sheria na kuongeza kuwa taasisi zenye mamlaka ya kupambana na vitendo hivyo zinapaswa kushughulikia malalamiko hayo.

 Aina na Majukumu ya Mabaraza ya Katiba:

Katika mkutano huo uliofanyika katika katika Ofisi za Tume zilizopo mtaa wa Ohio jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti huyo pia alizungumza kuhusu aina na majukumu ya Mabaraza ya Katiba.

Kwa mujibu wa Jaji Warioba, Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 imetoa fursa ya kuundwa kwa mabaraza ya aina mbili ambayo ni Mabaraza yatakayoundwa, kusimamiwa na kuendeshwa na Tume katika muda na tarehe itakayopangwa na Tume.

Aina ya pili, kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo, ni Mabaraza ya Katiba ya Asasi, Taasisi na Makundi mbalimbali yenye malengo yanayofanana. Mabaraza haya yatajiunda, yatajisimamia na kujiendesha yenyewe na kisha kuwasilisha maoni yao kuhusu rasimu ya Katiba ndani ya muda utakaopangwa na Tume.

“Kazi kubwa ya Mabaraza ya Katiba ya aina zote mbili ni kuipitia, kuijadili na kuitolea maoni rasimu ya Katiba itakayokuwa imeandaliwa na Tume kutokana na maoni yaliyokusanywa kutoka kwa wananchi,” alisema Jaji Warioba na kuziomba taasisi, makundi, asasi na vyama mbalimbali kutumia fursa hiyo ya kisheria kuunda mabaraza na kutoa maoni yao kuhusu rasimu ya Katiba itakayotolewa.

BREAKING NEWS: MWANAFUNZI AKATWA MKONO, AUGUZA JERAHA HOSPITALINI


Na Steven Augustino,
Tunduru.

MWANAFUNZI anayesoma darasa la pili katika shule ya msingi Mwongozo kata ya Ligoma tarafa ya Namasakata wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma,  ameumizwa vibaya katika mkono wake wa kulia baada ya kukatwa na upanga na mwanafunzi mwenzake.
Ikra Said mwenye umri wa miaka saba ndiye aliyekatwa mkono wake, na amelazwa katika hospitali ya wilaya ya Tunduru akiendelea na matibabu.

Mwandishi wa habari hizi amezungumza na majeruhi huyo ambapo alisema  kuwa mkasa huo ulimpata wakati akiwa na wanafunzi wenzake ambao walikuwa wametumwa na mwalimu waliye mtaja kwa jina moja la Komba ili wakamtafutie kuni msitu uliojirani na shule hiyo.

Akifafanua taarifa hiyo mwanafunzi huyo alisema kuwa wakati wakiwa katika harakati hizo za kutafuta kuni, ghafla alijikuta akishambuliwa kwa kukatwa na panga katika mkono wake wa kulia, na mwanafunzi mwenzake Ashraki Said anayesoma darasa la tatu shuleni hapo.   

Friday, April 26, 2013

MWAMBUNGU: WATENDAJI AMBAO NI KIKWAZO CHA MAENDELEO RUVUMA NITAWAFUKUZA KAZI

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu.



















Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

WATENDAJI wa serikali katika Halmashauri za mkoa wa Ruvuma, wametakiwa kufanya kazi zao ipasavyo kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma, na kwa yule atakayekiuka atachukuliwa hatua za kisheria, ikiwemo kufukuzwa kazi.

Vilevile mtendaji atakayeonekana kuwa kikwazo katika shughuli za kimaendeleo ya wananchi, hatavumiliwa badala yake atachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufikishwa fikishwa mahakamani.

Rai hiyo ilitolewa na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu, alipokuwa akihutubia katika Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani humo lililoketi leo kwenye ukumbi wa Jumba la maendeleo mjini hapa.

Friday, April 19, 2013

MAKAMPUNI YANAYOKIUKA TARATIBU ZA UNUNUAJI WA KAHAWA MBINGA YAANDALIWA MWAROBAINI

Gaudence Kayombo, Mbunge wa Mbinga Mashariki.



















Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

BODI ya kahawa kanda ya Ruvuma, imeagizwa kufanya ufuatiliaji wa karibu juu ya makampuni yanayojiandikisha majina mawili tofauti na kujihusisha na ununuzi wa zao hilo, kwa wakulima vijijini na mnadani Moshi ili yachukuliwe hatua za kisheria.

Agizo hilo lilitolewa katika kikao cha wadau wa kahawa mkoani humo, kilichoketi kwenye ukumbi wa Kanisa Katoliki uliopo Mbinga mjini, ambapo ilielezwa kuwa makampuni yanayofanya hivyo yanamuumiza mkulima na wafanyabiashara wadogo wadogo.

Kufuatia agizo hilo kampuni ya Tutunze ambayo inajishughulisha na ununuaji wa kahawa wilayani Mbinga, ilinyoshewa kidole na wadau hao kwamba inaongoza kwa ukiukaji wa taratibu za ukoboaji wa kahawa mbivu mitamboni huko vijijini.

WATUMISHI WAZEMBE KAZINI TUNDURU, KUFUKUZWA KAZI

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu.


















Na Steven Augustino,
Tunduru.

MKUU wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, Chande Nalicho amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa  Halmashauri ya wilaya hiyo, kuwachukua hatua ikibidi hata kuwafukuza kazi, watumishi wasiowajibika ikiwa ni juhudi za serikali kuinua taaluma wilayani humo.

Nalicho alisema hayo wakati akifunga mkutano wa kutathimini matokeo kidato cha pili, nne na sita uliofanyika katika ukumbi wa klasta Mjini humo na kuongeza kuwa hali hiyo imetokana na serikali kubaini kuwa watumishi  wa kada zote wilayani humo, hawako tayari kufanya kazi kwa kujituma hali iliyopelekea wilaya hiyo kuwa nyuma kielimu.

 “Viongozi ndio wasiopenda kufanya kazi, wamebakia kula mishahara tu na ndiyo maana katika wilaya hii, tumeendelea kuwa nyuma kielimu”, alisema Nalicho na kuongeza kwa kumtaka mkurugenzi awachukulie hatua za kinidhamu.

TUNDURU SEKTA YA ELIMU BADO NI TATIZO


Na Steven Augustino,
Tunduru.

IMEBAINISHWA kuwa mahusiano mabaya kati ya Walimu na Wanafunzi ni moja kati ya kikwazo kilichoelezwa kwamba huchangia kuzorota kwa elimu wilayani humo.

Kadhalika  wanafunzi kukataa kukaa katika mabweni au hosteli ni miongoni mwa vikwazo vya maendeleo ya elimu wilayani Tunduru na kusababisha wilaya hiyo kupata matokeo mabaya kwa wanafunzi waliofanya mitihani ya kidato cha pili na nne katika kipindi cha mwaka 2011/2012.

Hayo yalibainishwa na afisa elimu sekondari Ally Mtamila wakati akiwasilisha taarifa yake ya matokeo ya kidato cha pili na cha nne katika kipindi cha mwaka 2011/2012 katika mkutano maalum ulioketi wilayani humo, na kuongeza kwa kuwataka wazazi kushiriki kikamilifu katika usimamiaji wa watoto wao ili waweze kuwa na hamasa ya kupenda masomo wanapokuwa shuleni au nyumbani.

Monday, April 15, 2013

BREAKING NEWS: MVUA YASABABISHA MAAFA WILAYANI NYASA, MAKAZI YA JAA MAJI, MTU MMOJA AFARIKI DUNIA NA EKARI 45 ZA SOMBWA NA MAJI

Ziwa Nyasa.


















Na Kassian Nyandindi,
Nyasa.

YAMEJITOKEZA maafa makubwa  wilayani Nyasa mkoa wa Ruvuma, kufuatia mvua kubwa iliyonyesha wilayani humo, na kusababisha mtu mmoja kufariki dunia, mazao yaliyolimwa shambani na mifugo kusombwa na maji.

Tukio hilo limetokea usiku wa tarehe 14 mwaka huu, ambapo watu wamekosa mahali pa kuishi kutokana na nyumba zao kujaa maji na kulazimika, kwenda kuomba msaada kwa majirani wenzao.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi, Mkuu wa wilaya hiyo Ernest Kahindi alisema kunyesha kwa mvua hizo kumesababisha kuwepo kwa maji mengi yaliyokuwa yakitokea milimani na kuelekea kwenye makazi ya watu.

Friday, April 12, 2013

MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA ZA ASILI YATABORESHA ZAO LA KAHAWA


Upande wa kushoto mtaalamu wa mimea na udongo Kaminyoge Mhamerd wa kampuni ya Sustainable Harvest, ya kutoka wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro, akiwa katika eneo la shamba darasa la kilimo cha kahawa, kikundi cha Unango kata ya Ngima wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, akiwaelimisha wakulima wa zao hilo kuzingatia kanuni za kilimo bora.(Picha na Kassian Nyandindi)



Na Kassian Nyandindi,



KAHAWA ni moja kati ya bidhaa muhimu na maarufu inayopendwa duniani, vilevile ni chanzo cha mapato kwa nchi zinazozalisha zao hilo.
     
Uzalishaji wa zao hili si kazi rahisi bali ni kazi ngumu inayohitaji ujuzi wa hali ya juu, na kwamba  ili kuwawezesha wakulima kuzalisha zao hilo kwa viwango vyenye ubora, mara zote sekta husika zimekuwa zikiwaelimisha wakulima hao mara kwa mara namna ya uzalishaji huo.

Tanzania ni moja kati ya nchi inayozalisha kahawa, huku jitihada mbalimbali zimekuwa zikifanywa ili kuboresha uzalishaji wake kwa ushirikiano, kati ya serikali na taasisi binafsi.

BREAKING NEWS: WAANDISHI WAWILI NA AFISA UHAMIAJI WAFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA GARI MKOANI TANGA

IGP Said Mwema























Na Mwandishi wetu,
Tanga.

AJALI mbaya iliyotokea jana wilaya ya Handeni mkoani Tanga na kusababisha vifo vya watu watatu, ambao ni waandishi wa habari wawili kutoka kampuni ya Mwananchi Communication na gazeti la Uhuru na Mzalendo, Radio Aboud na Ofisa Uhamiaji wa wilaya hiyo.
 
Ajali hiyo iliyotokea Aprili 11 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi iliuhusisha msafara wa Mkuu wa wilaya hiyo Muhingo Rweyemamu, ni msafara unaodaiwa kuwa ulikuwa na magari matatu tu lakini gari moja liliacha njia na kupinduka.

Waliofariki ni pamoja na Hussein Semdoe mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Hamis Bwanga wa Radio Uhuru na Abood pamoja na Mariam Hassan ambaye ni Ofisa Uhamiaji wilaya ya Handeni.

Mkuu wa wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo pamoja na vifo vya marehemu hao.

Akizungumza na Mwandishi wetu, Mkuu wa wilaya hiyo alisema ajali hiyo ilitokea wakiwa kwenye msafara, kuelekea Ndolwa kupanda miti.

Muhingo alieleza kwamba gari lililopata ajali ni la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Handeni, lenye namba za usajili STJ 4673 ambalo ndilo lililokuwa likitumiwa na Ofisa Uhamiaji, Hassan pamoja na wanahabari hao.

Alisema huu ni msiba  mkubwa kwa wilaya ya Handeni kwani wamepoteza wachapakazi na watu muhimu katika mchakato wa maendeleo ya wilaya hiyo.

"Wilaya ya Handeni imepoteza wanahabari kwa asilimia 100, kwani waandishi hawa ndiyo walikuwa wanahabari pekee wilayani hapa,

"Msiba huu ni mkubwa si kwa tasnia ya wanahabari pekee bali hata kwa juhudi za maendeleo ya wilaya ya Handeni, tulikuwa tukizunguka nao katika shughuli mbalimbali hapa wilayani hivyo ni pigo kubwa," alisema Muhingo.
 
Aidha Mkuu wa wilaya hiyo alisema marehemu Hassan ambaye alikuwa afisa uhamiaji kabla ya umauti alikuwa mpambanaji mkubwa wa wahamiaji haramu katika wilaya hiyo.

Aliongeza kuwa hivi karibuni alifanikiwa kuwakamata takribani wahamiaji 70 eneo hilo, hivyo kifo chake ni pigo kubwa kwa nguvu kazi ya wilaya ya Handeni.

Miili ya waandishi imechukuliwa na ndugu na kwamba serikali inatoa pole kwa ndugu na jamaa waliopatwa na matatizo hayo.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Tanga Costantine Massawe amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo.

Thursday, April 11, 2013

BREAKING NEWS: MWANDISHI NA OFISA UHAMIAJI WAFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA GARI, WENGINE WAJERUHIWA VIBAYA



Na Mwandishi wetu,
Tanga.

WATU wawili wamefariki dunia na wengine wanne kujeruhiwa vibaya hivi punde, baada ya kutokea ajali katika wilaya ya Handeni wilayani Tanga.

Waliofariki dunia ni Mwandishi wa habari wa Uhuru na Mzalendo na Radio Aboud, Hamis Bwanga na Ofisa uhamiaji wa wilaya ya Handeni, Mariam Hassan akiwemo pia Mwandishi wa gazeti la Mwananchi Hussein Semdoe ambaye amejeruhiwa vibaya na hali yake sio nzuri mpaka sasa.

VIKONGWE WAKAMATWA WAKIWAFUNDISHA WATOTO USHIRIKINA, WASWEKA RUMANDE KULINDA USALAMA WAO

Na Steven Augustino,

Tunduru.

VIKONGWE wa tano kutoka katika kijiji cha Mtonya wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, wamezuiliwa katika kituo kidogo cha polisi Nakapanya, ili kulinda usalama wa maisha yao na kuwafanya wasishambuliwe kutokana na kutuhumiwa kufanya ushirikina na kuwafundisha taaluma hiyo watoto wa watu bila ridhaa ya wazazi wao.

Tukio hilo lilitokea baada ya vikongwe hao wanaodaiwa kuwa na uwezo wa kufungua na kuingia katika nyumba za watu kwa njia za kishirikina, walifumwa wakifanya vitendo hivyo katika kijiji cha Mindu wilayani humo.

Taarifa zilizothibitishwa na Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Nakapanya Kubodola Ambali, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Spia Msusa (50), Ayana Iddi (75) Adresia Maulid (68), Jenifer Saimon(60) na mwingine aliyefahamika kwa jina la Biti Nyoya mwenye umri wa miaka 60.

AFARIKI DUNIA BAADA YA KUVAMIWA NA TEMBO



Na Steven Augustino,
Tunduru.

MKAZI mmoja wa kijiji cha Daraja mbili kata ya Namwinyu tarafa ya Matemanga wilayani Tunduru mkoani Ruvuma, Chalamanda  Masapi (65) amefariki dunia baada ya kuvamiwa na kushambuliwa na Tembo.

Taarifa za tukio hilo zinaeleza kuwa marehemu Masapi  alikumbwa na mkasa huo  baada ya kukutana na tembo huyo ambaye alikuwa na mtoto, ghafla wakati akikagua uharibifu wa mazao uliofanywa na kundi la wanyama hao, katika shamba lake lililopo nje kidogo na kijiji hicho.

Mtoto wa marehemu Chalamanda ambaye alikuwa ni miongoni mwa shuhuda wa tukio hilo Rashid Chalamanda  alisema, yeye na marehemu baba yake kwakushirikiana na kundi la wananchi wanaolima katika eneo hilo, walikwenda katika mashamba yao kushiriki katika zoezi la kuwafukuza tembo hao ambao pia walivamia kijijini hapo na kufanya uharibifu mkubwa wa mazao yao.

Tuesday, April 9, 2013

UHURU AAPISHWA KUWA RAIS WA KENYA, AHUTUBIA TAIFA

Kulia ni Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta na Makamu wa Rais wa nchi hiyo Wiliiam Ruto baada ya kuapishwa hivi punde.



















UHURU Kenyatta ameapishwa kuwa rais mpya wa Kenya akifuatiwa na William Ruto ambaye hivi punde ameapishwa naye kuwa Makamu wa Rais wa Kenya.

Msajili wa Mahakama, Gladys Shollei ndio amemuapisha Uhuru Kenyatta kuwa rais wa nne Kenya na baadaye amemuapisha William Ruto kuwa Makamu wa Rais wan chi hiyo.

Marais mbalimbali wamewasili  hivi punde katika Uwanja wa Karasani kwa ajili ya kushudia kuapishwa kwa rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta.

MKUU WA WILAYA YA MBINGA AOMBWA KUINGILIA KATI SUALA LA KUINUA KIWANGO CHA MPIRA WA MIGUU NA MIKONO MBINGA

Mkuu wa wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga.




















Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

WADAU wa michezo wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, wamemuomba Mkuu wa wilaya hiyo Senyi Ngaga, kuingilia kati suala la kuinua kiwango cha mpira wa miguu na mikono wilayani humo.

Vilevile wadau hao walisema endapo mkuu huyo wa wilaya atafanya hivyo, wana hakika kiwango cha mpira wilayani humo kitaenda vizuri, na kuifanya wilaya hiyo wananchi wake waweze kupenda michezo.

Hayo yalisemwa na wadau hao walipokuwa wakizungumza na mwandishi wetu, kwa nyakati tofauti mjini hapa.

Wednesday, April 3, 2013

TUNDURU WALIA NA HALI NGUMU YA MAISHA, KUTOKANA NA WAJANJA WACHACHE KUJINUFAISHA KATIKA ZAO LA KOROSHO



Na Steven Augustino,

Tunduru.


CHAMA cha Wananchi CUF Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, kimewaomba wananchi wa wilaya hiyo kutotoa nafasi kwa viongozi watakaosimamishwa kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika chaguzi zijazo.

Hayo yalibainishwa na Viongozi wa chama hicho wakati wakizungumza katika mkutano wa hadhara, uliofanyika katika viwanja vya baraza la Idd na kuongeza kuwa kauli hiyo wanaitoa kufuatia viongozi wa CCM waliopewa dhamana na wananchi kushindwa kutimiza wajibu wao.

Mkurugenzi wa haki za bianadamu na sheria  Mtukumbe Selemen Issa Ismail na Katibu wa CUF wilaya  Mchemela Salum Abudalah  ni miongoni mwa waliobainisha maelezo hayo, na kuongeza kuwa hali hiyo inatokana na viongozi waliopewa mamlaka hayo kutotimiza wajibu wao na kusababisha hata zao la Korosho wilayani humo, wakulima kukosa soko la uhakika.

KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA TUNDURU, WAOMBA MSAADA



Na Steven Augustino,

Tunduru.

HALMASHAURI ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, imeahidi kutoa msaada wa shilingi milioni 2.8 katika kituo cha kulelea watoto yatima, kinachomilikiwa na Kanisa la Bibilia kijiji cha Mbesa  wilayani humo ikiwa ni juhudi yake ya kujali watoto hao.

Ahadi hiyo ilitolewa na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Robert Nehatta wakati akizungumza kwenye  maadhimisho ya Wanawake wa kikristo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini hapa.

Tayari fedha hizo zimekwisha pewa Baraka na Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya hiyo na kupitishwa katika bajeti ya mwaka 2013/2014.

Monday, April 1, 2013

UZINDUZI WA ALBAMU YA INJILI WAFANA, MKUU WA WILAYA YA MBINGA AWATAKA WANANCHI KUJENGA USHIRIKIANO

Mkuu wa wilaya ya Mbinga, Senyi Ngaga (Aliyeinama katikati) akiingiza DVD yenye nyimbo za Injili zilizotungwa na Rose Mahenge kwenye radio, ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa albamu ya Waweza zeeka mapema, uliofanyika kwenye ukumbi wa Uvikambi mjini Mbinga. (Picha na Kassian Nyandindi)





Na Kassian Nyandindi,

Mbinga.

WANANCHI wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, wametakiwa kujenga ushirikiano na sio kujengeana ubaguzi, ikiwa ni lengo la kuwafanya waweze kusukuma mbele gurudumu la kimaendeleo kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.

Sambamba na hilo wametakiwa kushiriki kikamilifu katika suala zima la ulinzi na usalama, ili wilaya hiyo iweze kuwa na amani na utulivu na hatimaye wananchi wilayani humo, waweze kuishi kwa raha mustarehe bila kuwepo vikwazo vya hapa na pale.

Mkuu wa wilaya hiyo Senyi Ngaga aliyasema hayo jana wakati wa uzinduzi wa albamu ya nyimbo za injili, ‘Waweza zeeka mapema’ iliyotungwa na mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili wilayani humo Rose Mahenge, uzinduzi ambao ulifanyika kwenye ukumbi wa Uvikambi uliopo Mbinga mjini.