Friday, May 31, 2013

MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYWAJI MAZIWA KITAIFA MKOANI RUVUMA YAFANA, MKUU WA MKOA ASISITIZA WANANCHI KUWA NA MAZOEA YA KUNYWA MAZIWA

 

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu, akizindua wiki ya unywaji wa maziwa kwa kuonyesha mfano wa kunywa maziwa, ikiwa ni njia moja wapo ya kuhamasisha Wananchi wa mkoa huo kujenga mazoea ya kunywa Maziwa. Maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya Manispaa ya Songea.
 



Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said  Mwambungu akikagua banda la maonyesho ya bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na maziwa katika sherehe ya uzinduzi wa wiki ya maziwa ambazo kitaifa zimefanyika mkoani Ruvuma. Kulia ni Dkt. Ruth Rioba Mwenyekiti wa Bodi ya Maziwa Taifa.
 
Mwambungu akiendelea kupokea maelezo juu ya matumizi ya bidhaa zinazotengenezwa kwa maziwa alipokuwa akikagua bidhaa zilizoletwa na wazalishaji na wasindikaji wa maziwa.






 Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said  Mwambungu (aliyeshika maiki) akitoa nasaha kuhamasisha unywaji wa maziwa kwa Wananchi wa mkoa huo ili waweze kujenga afya zao.  Maadhimisho hayo yalifanyika katika uwanja wa Manispaa ya Songea ambapo mkoa wa Ruvuma una Ng`ombe 371,000 kati yao wa maziwa ni 12,032  ambao huzalisha lita 96,256 kwa mwaka.


 
Dkt. Ruth Rioba Mwenyekiti wa Bodi ya maziwa taifa, akifafanua jambo juu  ya kuleta maadhimisho ya wiki ya maziwa mkoani humo, katika uzinduzi wa wiki ya maziwa uliofanyika viwanja vya Manispaa ya Songea.
 
Viongozi mbalimbali wa serikali, asasi, taasisi nao walishiriki katika uzinduzi huo.
 







Ng`ombe wa maziwa wakiwa katika banda maalumu katika viwanja vya Manispaa ya Songea katika eneo ambalo maadhimisho hayo yalifanyika na kilele chake kitakuwa Juni Mosi mwaka huu.



CUF NA CHADEMA WATII AMRI YA KUOMBA RADHI BUNGENI

 


    Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, Ezekiel Wenje.


















    Dodoma, 
    Tanzania. 

    Chama cha CUF na Chadema hivi punde Bungeni , vimekubali kuomba radhi kutokana na vurugu zilizosababishwa na CUF  yenye mrengo wa Kiliberali  na Chadema imemfanya hivyo kutokana na kuihusisha CUF na masuala ya ushoga na usagaji.

    Vyama hivyo vimeomba radhi baada ya Kamati ya Maadili ya Bunge kufanya kikao  kuanzia saa 11:00 jioni mpaka saa 2:30 usiku na kukubaliana kila chama kumuomba spika radhi, na pia kuliomba Bunge radhi kutokana na vurugu za jana.

    CUF wamelazimika kumuomba spika radhi; kuomba radhi Bunge na kuwaomba radhi Chadema kwa kumtukana Waziri kivuli wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Ezekeil Wenje wakati akisoma hutuba yake ambayo ndani yake ilieleza sera za mrengo wa Kiliberali ambazo  pamoja na mambo mengine ni ushoga na usagaji.  

    MATOKEO KIDATO CHA SITA, ASILIMIA 93 WAFANYA VIZURI, 89 MATOKEO YAZUILIWA

      Na Mashirika mbalimbali ya Habari,

    BARAZA la mitihani hivi sasa limetangaza matokeo ya kidato cha sita mwaka 2013. Matokeo hayo yatapatikana muda mfupi ujao kwenye tovuti yao.

    Asilimia 93 ya waliofanya mtihani huo wa kidato cha 6 wamefaulu.

    Shule ya kwanza iliyoongoza ni Marian Girls ya mkoani Pwani na ya pili ni Mzumbe ya Morogoro.

    TAARIFA YA UCHUGUZI JUU YA KUTEKWA NA KUUMIZWA VIBAYA KWA ABSALOM KIBANDA HII HAPA

    Rais Jakaya Kikwete akimtaka hali Absalom Kibanda, hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam ambako alilazwa baada ya kuumizwa vibaya hivi karibuni.    


       
    UTANGULIZI:

    Usiku wa Jumanne ya Machi 5 kuamkia Machi 6, 2013, Mhariri Mtendaji wa New Habari (2006) Ltd, ambaye pia Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda alivamiwa na kujeruhiwa vibaya akiwa nje ya lango la kuingilia nyumbani kwake Mbezi Juu, Dar es Salaam.

    Tukio hilo liliishtua na kutikisa taifa kwa kiwango kikubwa si tu katika tasnia ya habari nchini, bali pia jamii kwa ujumla hasa baada ya aina ya utekaji, utesaji na usiri uliotumika katika kufanikisha uhalifu huu kufanana kwa karibu na tukio lilomkuta Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madkatari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka lililotokea karibu miezi tisa kabla ya tukio la Kibanda yaani, usiku wa Juni 26, 2012.

    Ukiacha matukio hayo, miezi sita kabla ya Kibanda kutekwa na kuteswa Mwandishi Daudi Mwangosi, aliuawa akiwa mikononi mwa vyombo vya dola Septemba 2, 2012 huko Nyololo, Iringa akiwa kazini.

    Tukio la Kibanda limekuwa na sura ya mwendelezo wa mauaji au utesaji wa wanahabari, hasa ikitiliwa maanani kuwa Mwandishi Issa Ngumba (45) wa Radio Kwizera aliyekuwa anafanyia kazi zake katika Wilaya ya Kakonko, Kigoma, Januari mwaka huu, alipigwa risasi na kuuawa katika mazingira ya kutatanisha.Kama hiyo haitoshi, tukio la kutekwa na kudhuriwa kwa Kibanda limetokea mwezi mmoja tu baada ya Mwandishi wa Gazeti la Tanzania Daima, Shaaban Matutu kupigwa risasi na polisi akiwa nyumbani kwake Dar es Salaam kwa maelezo kuwa kimakosa polisi walidhani Matutu ni jambazi.

    Mazingira ya kutekwa na kuumizwa kwa Kibanda yalitia wasiwasi kuwa upo uwezekano, na dalili zilionyesha kwamba waliofanya kitendo hicho cha kinyama hawakuwa wezi wala majambazi kutokana na ukweli kwamba licha ya kuwa na fedha zipatazo shilingi milioni tatu taslimu ndani ya gari, laptop, simu tatu za gharama (ipad, iphone na Blackberry), watekaji hawa hawakuchukua chochote baada ya kukamilisha uhalifu wao.Kibanda aliumizwa kwa kiwango kikubwa.

    Alitobolewa jicho la kushoto, akaumizwa vibaya kichwani kiasi cha kusababisha kuvunjika kwa baadhi ya mifupa ya kichwa. Aling’olewa meno mawili na kucha mbili, tena bila gazi.

    Watekaji hawa, katika unyama wa ajabu kabisa, walimkata pingiri ya kidole cha pete chini ya kucha na kuondokana nayo.Hali hiyo iliibua maswali mengi, watu wengi wakajiuliza na kutafuta sababu za kutekwa na kuumizwa kwa Kibanda kiasi hiki.

    Kutokana na kuwapo kwa maelezo mengi yanayotofautiana kuhusu tukio hilo, ikabidi Jukwaa la Wahariri Tanzania lifanye uamuzi.Katika kikao cha Machi 8, 2013 Jukwaa la Wahariri Tanzania liliunda TIMU ya watu watano na kuipa hadidu rejea za kufanya uchunguzi wa kihabari juu ya shambulio hilo kubaini limetokana na nini.

    Timu hiyo iliundwa kufuatia uamuzi wa Jukwaa la Wahariri kufanya uchunguzi huo na baada ya kukubalika kwa ombi la ruzuku ya kufanya uchunguzi huo wa kihabari kutoka Mfuko wa Vyombo Vya Habari Tanzania (TMF).

    Ruzuku ya TMF ililenga kiujumla kutumia tukio la Kibanda kuwa chanzo cha kutengeneza mazingira salama zaidi kwa waandishi na wahariri na kwamba kiwango cha matukio ya kuteswa, kupigwa na kuuawa kwa waandishi yanapungua kila mwaka.

    Timu hii imefanya kazi usiku na mchana kwa kwa zaidi ya mwezi. Timu imezungumza na wadau 26. Kati ya hawa yumo Kibanda mwenyewe, mke wake, ndugu zake, wasaidizi wake, waajiri wake wa zamani na wa sasa, viongozi wa kisiasa na vyombo vya dola kutafuta ukweli wa jambo hili.

    Pia tumesoma matamko na habari zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii na magazeti ya kati ya Machi 5, 2012 na Aprili 5, 2012 kwa nia ya kufanya ulinganishi wa taarifa tulizozipata kutokana na uchunguzi na habari zilizochapishwa baada ya kutekwa kwake.

    Vyombo vya dola akiwamo Waziri mwenye dhamana walikataa kuhojiwa wakisema kuna tume ya serikali inayofanya kazi hiyo na kwamba kuhojiwa kungeonyesha kutokuwa na imani na tume hiyo.Leo tunawasilisha muhtasari wa ripoti hii.

    MATOKEO KIDATO CHA NNE 2012 YATANGAZWA UPYA, BAJETI YA KAWAMBWA YAUNDIWA ZENGWE


     
    Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa. 



















    Dar es Salam,
    Tanzania.


    WAKATI Baraza la Mitihani Taifa (NECTA) likitangaza matokeo mapya ya kidato cha nne, baada ya kufanya marekebisho ya alama za viwango vya ufaulu, njama za kukwamisha hotuba ya Bajeti ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa zinaandaliwa.


    Habari zilizonaswa kwa msaada wa vyanzo mbalimbali  vinaeleza kuwa, Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamejipanga kukwamisha hotuba ya Wizara hiyo, kwa madai kwamba Waziri huyo ameshindwa kusimamia sekta ya Elimu.

    Thursday, May 30, 2013

    MWILI WA MAREHEMU MANGWEA KUCHUNGUZWA NA JOPO LA MADAKTARI KABLA YA KUWASILI NCHINI


    Marehemu Albert Mangwea (kulia)enzi za uhai wake, akiwa na M 2 The P ambaye yuko Hopitali bado, wasanii hao walikutwa wakiwa hoi katika chumba kimoja nchini Afrika Kusini.



    PRETORIA, 
    Afrika Kusini.

    WAKATI utaratibu mzima wa mapokezi ya mwili wa marehemu Albert Mangwea, ukiendelea kufanyika huko Mbezi Beach jijini Dar es Salaam nyumbani kwa Baba mdogo wa marehemu, taarifa kutoka Pretoria Afrika Kusini zinaeleza kuwa, mwili wa marehemu huyo utaanza kufanyiwa uchunguzi wa kina leo kabla ya kusafirishwa kuja nchini Tanzania.

    Jamira Saidi anayeishi nchini Afrika Kusini alipozungumza kwa njia ya simu na Mwandishi wetu alisema kwamba, mwili wa marehemu leo utaanza kufanyiwa uchunguzi wa kina na jopo la Madaktari ili kujua sababu hasa ya kifo chake.

    Monday, May 27, 2013

    VIONGOZI CHADEMA MBINGA WAFUNGASHA VIRAGO, KUTOKANA NA KUTOWAJIBIKA IPASAVYO

    Freeman Mbowe.
























    Na Kassian Nyandindi,

    Mbinga.


    HALI ya kisiasa kwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma imeendelea kuwa tete, kufuatia viongozi wa chama hicho ngazi ya Wilaya na Jimbo kuvuliwa madaraka, kutokana na kushindwa kukiimarisha chama na kutowajibika ipasavyo.

    Kauli hiyo ilitolewa na aliyekuwa Katibu wa Baraza la vijana la chama hicho (BAVICHA) Felix Katoto, ambaye hivi sasa anashikilia ofisi ya CHADEMA wilayani Mbinga kwa muda, kutokana na uongozi uliokuwa awali kuondolewa madarakani.

    Katoto alisema hayo alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake, ambapo alieleza pia uongozi huo wa awali ulikuwa hautekelezi majukumu ya chama kwa mujibu wa taratibu walizojiwekea, na ndio maana wamefikia maamuzi hayo.

    RAIS BARACK OBAMA KUJA NA UJUMBE WA WATU 700 TANZANIA

    Barack Obama.



    Dar es Salaam, 
    Tanzania.

    RAIS wa Marekani, Barack Obama, atakuwa na ujumbe wa watu 700 katika ziara yake ya siku mbili nchini Tanzania kuanzia Julai Mosi mwaka huu.

    Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari.

    Alisema kutokana na ziara ya kiongozi huyo, alitoa wito kwa wafanyabiashara wenye hoteli, migahawa, magari ya kukodisha waziboreshe biashara zao ili Wizara hiyo iingie mkataba nao.

    Aliongeza kuwa, akiwa nchini, Obama atafanya mkutano na viongozi wa nchi zinazoendelea kwa kuzungumzia umuhimu wa sayansi na teknolojia katika nchi zao.

    DOKTA SLAA ASEMA VURUGU ZA MTWARA ZINASABABISHWA NA UMASKINI, HUKU AKIKINYOSHEA KIDOLEA CHAMA CHA MAPINDUZI

    Dkt. Willbroad Slaa.


      












    Editruda Mashimi,
    Dar es Salaam.

    WAKATI Serikali ikiendelea kuwatupia wanasiasa lawama kuhusiana na vurugu za wakazi wa Mtwara, wanaopinga hatua ya Rais Kikwete na serikali yake kusafirisha gesi hadi jijini Dar es Salaam kwa njia ya mabomba, Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dkt. Willbroad Slaa, amesema kwamba machafuko yanayotokea katika mkoa huo hayasababishwi na mambo ya kisiasa, isipokuwa ni umaskini unaoikabili nchi.

    Dkt. Slaa alisema kwamba umaskini huo unaosababisha vurugu za Mtwara unachangiwa na CCM tangu zama za kale na si kwa siasa za sasa. 

    “Yanayotokea Mtwara ni matokeo ya umaskini ambao CCM imewaletea wananchi,

    “Mtwara wanakumbuka ya Mwadui, Geita na North Mara sasa wanayakataa”, alisema Dkt. Slaa katika ukurasa wake wa Tweeter.

    Friday, May 24, 2013

    SAFARI YA MWISHO YA MTUNZI MAARUFU WA VITABU CHINUA ACHEBE



















    Na Halima Kambi,

    MAELFU ya waombolezaji wamehudhuria katika mazishi ya mtunzi mashuhuri wa vitabu barani Afrika, Chinua Achebe yaliyofanyika karibu na nyumbani kwa familia yake mjini Ogidi, mji mdogo kwenye vilima vya jimbo la Anambra.

    Mwili wa marehemu Achebe uliwasili nchini Nigeria siku ya Jumatano, kutokea mjini Bostan, Marekani ambako alikuwa amefariki dunia.

    Mazishi hayo yalifanyika  katika kanisa la mtakatifu Philip la Anglikana, na kuhudhuriwa na waombolezaji ambao wamepewa mualiko maalum  huku wengine wakiwa nje wakisikiliza ibada hiyo, baada ya kuwekewa spika.

    Thursday, May 23, 2013

    RAIS KIKWETE ATEMA CHECHE JUU YA VURUGU ZA MTWARA

    Rais Jakaya Kikwete, wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.






















    Na Mwandishi wetu,

    Rais Jakaya Kikwete amekemea vikali vurugu zilizotokea jana mkoani Mtwara, baada ya kusomwa Bungeni kwa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini.

    Akizungumza katika eneo la Kizota, Dodoma wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Barabara ya Dodoma kwenda Iringa, Rais Kikwete alisema wote waliohusika na vurugu hizo watasakwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

    Rais Kikwete alisema rasilimali inayopatikana mahali popote pale nchini inatakiwa kutumiwa na Watanzania wote.

    BREAKING NEWS: SHEHA ZANZIBAR AMWAGIWA TINDIKALI

    Sheha wa Tumondo, aliyemwagiwa Tindikali.

















     
    ZANZIBR:

    Mohamed Omary Said, amemwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana na hivyo kupata maumivu makali sehemu yake ya kifua na jicho kuumia vibaya.

    Sheha huyo alikimbizwa katika hospitali ya Mnazi mmoja, mjini Unguja ambako anatiwa matibabu ya dharura.

    HALI YAZIDI KUWA TETE MKOANI MTWARA, WATU 91 WATIWA MBARONI

    Jinsi hali ilivyokuwa tete mkoani Mtwara.














    MTWARA, TANZANIA:

    Waziri wa mambo ya ndani Dkt. Emmanuel Nchimbi ametoa tamko kali hivi karibuni juu ya  vurugu zinazoendelea kutokea katika Manispaa ya Mtwara, kwamba damu ya Wanajeshi wanne waliofariki katika ajali haitamwagika bure, na kwamba vyombo vya usalama vinawasaka ndani na nje ya nchi watu wote wanaohusika na vurugu hizo.
    Askari waliopoteza maisha ni wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambao walipata ajali wakati wakitoka Nachingwea kwenda Mtwara, ili kuongeza nguvu katika kutuliza ghasia.

    Dk Nchimbi amesema wanajeshi 32 waliagizwa kwenda kuongeza nguvu na kwamba waliojeruhiwa ni katika  ajali hiyo 20.

    VURUGU ZA MTWARA: VIKAO VYA BUNGE VYA ENDELEA KUAHIRISHWA, NYUMBA YA MWANDISHI WA HABARI YACHOMWA MOTO

    Spika Anna Makinda akizungumza na Wabunge Dodoma leo.
























    BUNGENI DODOMA:

    HALI imekuwa tete mkoani Mtwara kufuatia mapambano ya wananchi na askari wa Jeshi la Polisi yakiendelea mkoani humo, ambapo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda amelazimika kuahirisha vikao vya Bunge kwa siku ya pili sasa, ili kuipa serikali nafasi ya kumaliza mgogoro huo ambao unaendelea.

    Spika huyo alifikia maamuzi hayo leo asubuhi baada ya Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Dkt. Emmanuel Nchimbi, kutoa maelezo ya serikali juu ya mapigano hayo yaliyoanza jana mkoani humo.

    Wananchi wa Mtwara walianzisha mapigano hayo kwa lengo la kupinga hotuba ya Wizara ya nishati na madini, iliyosomwa Bungeni na kuweka msisitizo kwamba gesi hiyo lazima isafirishwe hadi Jijini Dar es Salaam.

    Wednesday, May 22, 2013

    WAKAZI WA TINGINYA WILAYANI TUNDURU WANUFAIKA NA MFUMO WA UMEME JUA

    Mkuu wa wilaya ya Tunduru, Chande Nalicho.



    Na Steven Augustino,

    Tunduru.

    WAKAZI wa kijiji cha Tinginya tarafa ya Nakapanya wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, wameipongeza serikali kwa kuwafungia mfumo wa umeme Jua(SOLA) katika zahanati yao na kueleza kuwa mradi huo, utawakomboa wanawake ambao kwa muda mrefu walikuwa wakijifungua wakiwa gizani.

    Fatuma Mapila na Alihad Abdalahman ambao walikuwa wamepeleka mtoto wao kwa ajili ya matibabu na muuguzi wa zahanati hiyo, Grolia Lupindo ni miongoni mwa baadhi ya wananchi ambao walishindwa kuzuia furaha yao, baada ya kushuhudia wakati mfumo huo ukiwashwa katika zahanati yao na katika nyumba ya mganga, iliyopo jirani na eneo hilo la kutolea huduma ya afya.

    Wakizungumza kufuatia hali hiyo walisema,  kwa muda mrefu tangu zahanati yao ifunguliwe mwaka 1990 na kuanza kutoa huduma, wanawake wa kijiji cha Tinginya na vitongoji jirani walikuwa wakitumia vijinga vya moto kumulikia wakati wa kujifungua, hali ambayo ilikuwa ikihatarisha maisha yao na watoto wanaojifungua.

    Monday, May 20, 2013

    MAWAZIRI WATATU WA JAKAYA KIKWETE AMBAO WAKO HATI HATI KUTOLEWA, HAWA HAPA

      
    Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi  Dk Shukuru Kawambwa.

     Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Dk. Mathayo David Mathayo 
    Dkt. Mathayo David Mathayo, Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi.

     https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhAGwjzsUVqfq3UijG9oxL4vlY6gQyP3eQAFOSljCMNGYldUBT_R_DGZMbDnj6bKKkXNpBr4bfFyDD2Wg8UZON6lNoAylCH47CvSyB9vkS7c7eGCQiH_kZxntuIx7IsQYoCPWrFvpjE9w4/s1600/Dk.+Fenella+Mukangara,+Waziri+wa+Habari,+Vijana,+Utamaduni+na+Michezo.JPG 
    Dkt. Fenella Mukangara, Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.


    Na Mwandishi wetu, 

    UPEPO mbaya ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unazidi kuvuma, safari hii wabunge wake wakimtaka Rais Jakaya Kikwete kuwafukuza kazi mawaziri watatu.

    Mawaziri wanaotakiwa kung’olewa ni Dkt. Shukuru Kawambwa (Elimu na Mafunzo ya Ufundi), Dkt. Mathayo David Mathayo (Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi) na Dkt. Fenella Mukangara (Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo).

    MATUKIO MBALIMBALI YA KIKAO CHA WABUNGE WA CCM MJINI DODOMA LEO

     
    Wabunge wakifurahia jambo nje ya ukumbi wakati wa mkutano huo, Kutoka kushoto ni Dkt. Mary Mwanjelwa,  Ritha Kabati, Angela Kairuki, Beatrice Shelukindo na Vicky Kamata.
    Shabiby akizungumza na Angela Kairuki.
    Vicky Kamata na Ana Kilango Malecela wakiwa ukumbini.
    Dkt. Asha Rose Migiro akimsalimia Mama Anna Kilango Malecela.
    Dkt. Maua Daftari na Samiah Suluhu wakiwa ukumbini.
    Job Ndugai akimpongeza Mbunge wa Igunga Dkt. Dalaly Peter Kafumu kurejeshewa Ubunge.
    Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dkt. Asha Rose Migiro akimsalimia Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa wakati wa kikao hicho cha Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete na wabunge wa CCM.


    Mbunge wa Kyela Dkt. Harrison Mwakyembe, akimsikiliza kwa makini Mbunge mwenzake Innocent Kalogeris  wakati wa mkutano huo. (Picha zote na Bashir Nkoromo).

    RAIS KIKWETE AFANYA KIKAO NA WABUNGE WA CHAMA CHA MAPINDUZI LEO MJINI DODOMA


     Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasili ukumbini wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo katika ukumbi wa jengo la White House, makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenista Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.
     Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa kikao chake na wabunge wa CCM, leo katika ukumbi wa jengo la White House, makao makuu ya CCM, mjini Dodoma. Wengine kushoto ni Spika wa Bunge Anna Makinda, Katibu wa Wabunge wa CCM, Jenister Mhagama na Mwenyekiti wa Wabunge wa CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.
      Wabunge wa CCM wakiwa kwenye kikao chao na Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete leo kwenye ukumbi wa Jengo la White House, makao makuu ya CCM mjini Dodoma.
     Wajumbe kwenye kikao hicho wakibadilishana mawazo ukumbini. Walioketi mbele, Kushoto ni Katibu wa NEC Uchumi na Fedha Zakiah Meghji na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dkt. Asha Rose Migiro na Mbunge wa Urambo na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta.
      Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Mwigulu Nchemba akibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar) Vuai Ali Vuai na Katibu wa NEC Oganaizesheni Dk. Muhammed Seif Khatib kwenye kikao hicho.
     Katibu wa NEC Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Dk. Asha-Rose Migiro(kulia) akisalimiana na Mbunge wa viti Maalum Vicky Kamata wakati wa kikao hicho. Kushoto ni Mbunge wa Same Anne Kilango Malecela.
     Mbunge wa Songea na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dkt. Emmanuel Nchimbi (kushoto) akitaniana kuhusu Uyanga na Simba na Mwenyekiti wa Simba, Mbunge wa Tabora Aden Rage nje ya ukumbi kabla ya kuanza mkutano huo. Kulia ni Mbunge wa Viti Maalum Esther Bulaya.
    Mbunge wa Bunga Steven Wasira (kulia) akibadulishana mawazo na wabunge wenzake, Dkt. Kamani na Mkullo kabla ya kikao kuanza.
    Mbunge wa Kinondoni, Iddi Azan (kushoto) akibadilishana mawazo na wabunge wenzake Khamis Kagasheki na Shabiby nje ya ukumbi.(Picha zote na Bashir Nkoromo)

    Friday, May 17, 2013

    ASKOFU MTEGA AELEZA SABABU ZA KUJIUZURU

    Askofu Norbeth Mtega.





































    Na Mwandishi Maalum,
    Songea.

    ASKOFU Mkuu wa Kanisa Katoriki, Jimbo Kuu la Songea, mkoani Ruvuma ambaye juzi ametangaza kujiuzulu, Norbert Mtega, ameelezea sababu zilizomfanya achukue uamuzi huo.

    Akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema hali hiyo inatokana na kusumbuliwa na magonjwa mbalimbali ambayo ni presha, miguu, magoti kujaa maji na kukosa usingizi kwa muda mrefu hivyo kujisikia kizunguzungu na tayari amewahi kuanguka zaidi ya mara nne.

    Alisema jamii inayomtazama inamuona yupo kawaida lakini ana matatizo makubwa ya kiafya kwa muda mrefu ila alikuwa akijitahidi kufanya kazi za kitume hali ambayo imechangia afya yake kuendelea
    kuwa dhoofu.

    Thursday, May 16, 2013

    ASKOFU NORBETH MTEGA WA JIMBO KUU LA SONGEA AJIUZURU WADHIFA WAKE

    Askofu Norbeth Mtega.
    Hizi ni sehemu ya nyaraka zinazothibitisha kujiuzuru kwa Askofu Norbeth Mtega.










































































    Kassian Nyandindi,
    Songea.

    ASKOFU mkuu wa jimbo kuu la Kanisa katoliki Songea, Mhashamu Norbeth Mtega amejiuzulu.

    Taarifa za kujiuzulu kwa kiongozi huyo zilipatikana jana majira ya mchana zikieleza kuwa Askofu Mtega, alikuwa ametembelea Abasia ya Wabenediktini iliyopo Hanga wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma. 

    Mhashamu Mtega alipokuwa katika abasia hiyo ya Hanga aliwatangazia waumini na watawa wa shirika la Wabenediktini kuwa, kuanzia sasa yeye siyo Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Songea.

    Tuesday, May 14, 2013

    VIGOGO WILAYANI MBINGA WASHUSHIWA SHUTUMA NZITO, MKUU WA WILAYA ANYOSHEWA KIDOLE, MKURUGENZI MTENDAJI ADAIWA KUWA KINARA WA KUENDELEZA MGOGORO

    Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu.





















    Na Kassian Nyandindi,

    Mbinga.


    KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida baadhi ya viongozi Waandamizi wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, wamenyoshewa kidole na kulalamikiwa kwamba, wamekuwa wakifumbia macho malumbano yanayoendelea kushamiri katika idara ya elimu wilayani humo.

    Aidha vigogo hao wilayani humo, wametupiwa lawama kwamba wengine wamekuwa wakishiriki katika kuendeleza malumbano hayo, na hata kufikia hatua ya kukatisha tamaa kwa baadhi ya watendaji wa idara hiyo, ambao wanaonekana kufanya vizuri katika kukuza maendeleo ya sekta hiyo ya elimu.

    Kwa ujumla hivi sasa kumekuwa na mgogoro mzito katika idara ya elimu wilayani Mbinga, hasa kwa kitengo cha elimu ya msingi jambo ambalo linazua malalamiko kutoka miongoni mwa wadau wa elimu.

    Friday, May 10, 2013

    USAFIRI WA DALADALA LEO HII IRINGA, NI HUU HAPA

    Abiria wakiwa wamebebwa kwenye pikipiki aina ya Toyo, kutokana na madereva wa daladala katika Manispaa ya Iringa, kugoma kusafirisha abiria.(Picha na Francis Godwin)

    ABIRIA MJINI IRINGA WAKIHANGAIKA KUTAFUTA USAFIRI

    Jinsi gani hali ilivyokuwa tete mjini Iringa, baada ya madereva wa daladala kugoma kusafirisha abiria, hapa abiria wakionekana wakibadilishana mawazo namna ya kupata usafiri wa kwenda katika maeneo yao ya kazi.(Picha na Francis Godwin)

    MADEREVA WA DALADALA KATIKA MJI WA IRINGA WAGOMA KUSAFIRISHA ABIRIA, POLISI WAINGILIA KATI KUWATULIZA

    Baadhi ya abiria wakiwa wamepanda gari ya mizigo mjini Iringa, kwa lengo la kuwahi katika maeneo yao ya kazi leo, baada ya madereva wa daladala kugoma kusafirisha abiria.

    Na Mwandishi wetu,
    Iringa.

    KWA siku ya leo kadhia za hapa na pale zimeanza kujitokeza katika mji wa Iringa, mkoani Iringa kufuatia mgomo wa daladala ambao umeanza kwa kasi na kuchukua sura mpya, hali ambayo imesababisha wananchi, kutembea kwa mguu umbali mrefu wakielekea katika maeneo yao ya kufanyia kazi.

    Mgomo  wa  daladala  umeanza  kwa  kasi katika mji  wa Iringa baada ya daladala  zote  kugoma  kufanya kazi, huku wanafunzi na wafanyakazi wa iadara mbalimbali wakichelewa kwenda katika vituo vyao vya kazi.

    Tuesday, May 7, 2013

    BAADHI YA WAJUMBE WA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YA MKOA WA RUVUMA, NAYO IKIFUATILIA KWA UMAKINI SEMINA YA RUSHWA ILIYOHUSISHA VIONGOZI WA DINI WA NYANDA ZA JUU KUSINI

    Kushoto ni Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Deusdedith Nsimeki, akiwa na safu ya Kamati ya ulinzi na Usalama ya huo katika semina ya Rushwa ya viongozi wa Dini wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, iliyoendeshwa na Mkurugenzi wa TAKUKURU nchini Edward Hosea. Wa tatu kutoka kushoto ni Afisa kutoka idara ya uhamiaji mkoa wa Ruvuma Koku Rwebandiza.(Picha na Mwandishi wetu)