Na Steven Augustino, 
Tunduru.

MKUU wa  wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma Chande Nalicho, amewataka vijana na makundi mengine yanayonufaika kwa kupatiwa mafunzo mbalimbali wilayani humokuzingatia mafunzo hayo  ili yaweze kuwanufaisha na kuwa chachu ya kujiletea maendeleo miongoni mwao.
 
Nalicho alitoa kauli hiyo wakati akifunga mafunzo ya siku 10 yaliyotolewa kwa washiriki 55 juu ya uhifadhi wa udongo, maji na mazingira yaliyofanyika katika ukumbi wa chuo cha maendeleo ya jamii kilichopo kijiji cha  Nandembo wilayani humo.

Pamoja na mambo mengine mkuu huyo wa wilaya, aliahidi kufanya ziara ya ufuatiliaji wa utekekelezaji wa mafunzo hayo kwa vitendo ifikapo Mei 31 mwakani na pia aliwasisitiza washiriki hao kueneza elimu waliyoipata kwa wengine na kuwawezesha kushiriki pamoja katika mapambano hayo ya uhifadhi wa mazingira.