Na Steven
Augustino,
Songea.
ROBERT Mkika (26) ambaye ni askari wa kikosi cha Jeshi la
Kujenga Taifa (JKT) Mlale mkoani Ruvuma, anatafutwa na Jeshi la Polisi mkoani humo
ili aweze kujibu tuhuma ya kumtesa mtoto wa ndugu yake, ambaye alikuwa akiishi
naye.
Mtoto huyo ambaye anafahamika kwa jina la Frank Kiria (9) anasoma
darasa la tatu katika shule ya msingi mkombozi, Manispaa ya Songea mkoani hapa.
Kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msikhela
amethibitisha juu ya tukio hilo na kueleza kuwa katika kuhakikisha mtoto huyo
anapata uangalizi salama hivi sasa wapo katika mchakato wa kufanya mawasiliano
na vituo vya kulea watoto yatima, ili waweze kumkabidhi huko hadi taratibu za kumrejesha
kwao Bukoba kwa wazazi wake zitakapokamilika.
Msikhela alifafanua kuwa Frank alikimbia nyumbani kwa askari
huyo wa JKT Mei 27 mwaka huu, na kwenda kwa rafiki yake Jackson Malekela
kutokana na manyanyaso aliyokuwa akiyapata.




