Na Steven Augustino,
Tunduru.
WILAYA ya Tunduru mkoani Ruvuma imeanza kutekeleza mpango wa kuwapatia chanjo mpya ya kuzuia ugonjwa vichomi na kuharisha kwa kuwapatia chanjo hiyo jumla ya watoto 12,372 walio chini ya umri wa mwaka mmoja ikiwa ni juhudi ya serikali kupambana na vifo vitokanavyo na magonjwa hayo.
WILAYA ya Tunduru mkoani Ruvuma imeanza kutekeleza mpango wa kuwapatia chanjo mpya ya kuzuia ugonjwa vichomi na kuharisha kwa kuwapatia chanjo hiyo jumla ya watoto 12,372 walio chini ya umri wa mwaka mmoja ikiwa ni juhudi ya serikali kupambana na vifo vitokanavyo na magonjwa hayo.
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Chande Nalicho alisema hayo alipokuwa akizundua chanjo hizo katika ukumbi wa kutolea huduma ya mama na mtoto hospitali ya serikali ya wilaya hiyo iliyopo mjini hapa.
Katika hilo Nalicho aliwahimiza wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao bila kukosa, ili wapatiwe chanjo hizo zikiwa ni juhudi za mapambano dhidi ya magonjwa hayo.
Alisema endapo kutatokea wazazi na walezi kuzembea katika kuzingatia kupeleka watoto wao kupatiwa chanjo ya magonjwa hayo kunaweza kusababisha vifo vingi visivyo vya lazima.





