Tuesday, February 16, 2016

WAZIRI WA NCHI OFISI YA WAZIRI MKUU JENISTA MHAGAMA ATEMBELEA WAHANGA WA MAFURIKO RUFIJI

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Mayuyu, wilayani Rufiji wakati alipofika kijijini humo kukagua athari za maafa ya mafuriko.
Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama akieleza maamuzi ya serikali kupeleka chakula cha msaada kwa waathirika wa maafa ya mafuriko wa kijiji cha Ikwiriri wilayani Rufiji, Februari 16 mwaka huu alipokuwa katika ziara ya kukagua athari za maafa hayo wilayani humo.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu)

SERIKALI YAPELEKA TANI 200 ZA MAHINDI KWA AJILI YA CHAKULA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO RUFIJI

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu), Jenista Mhagama akiangalia sehemu ya njia iliyokuwa ikitumiwa na wananchi wa kijiji cha Utete wilayani Rufiji ambayo kwa sasa wanatumia mitumbwi kuvuka kuelekea kijijini humo kutokana na njia hiyo kufurika maji, wakati akikagua athari za maafa ya mafuriko wilayani humo Februari 16 mwaka huu.


Na Mwandishi Maalum,
Rufiji.

SERIKALI imepeleka tani 200  za mahindi ya chakula cha msaada kwa waathirika wa maafa waliokumbwa na mafuriko wilayani Rufiji mkoa wa Pwani, yaliyotokea huko na kuathiri jamii ikiwemo uharibifu wa mashamba na chakula cha akiba cha wananchi waishio tarafa ya  Mkongo, Ikwiriri na Mhoro wilaya humo.

Akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo wakati wa ziara ya kukagua athari za maafa hayo Februari 16 mwaka huu, Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu sera, bunge, ajira na wenye ulemavu, Jenista Mhagama alibainisha kuwa jukumu la serikali ni kuhakikisha kwamba inawajengea uwezo wananchi wake, pindi maafa yanapotokea.

“Ndugu zangu wanarufiji awali maafa yalipotokea hapa wilayani, tulitanguliza tani 100 za mahindi na sasa tunaongeza nyingine 200 hivyo tutakuwa tumeleta jumla ya tani 300 lakini hatutaishia hapo, tumewaleta sasa na mbegu za mahindi tani 3 na mtama tani 2 lengo la serikali tumieni mbegu hizi kuzalisha mazao kwani yenyewe haiwezi kuwalisha katika kipindi cha mwaka mzima, mkitumia mahindi haya mtaweza kukabiliana na upungufu wa chakula unaowakabili”, alisema Mhagama.

Mkazi wa kijiji cha Mayuyu wilayani Rufiji, Suleiman Idd akiishukuru serikali kwa msaada huo.
Waziri Mhagama aliongeza kuwa pamoja na serikali kupeleka mahindi hayo katika wilaya ya Rufiji, bado wataalamu wake wanaendelea na tathimini ya kina ili kuweza kufanya upembuzi yakinifu juu ya mahitaji halisi ya chakula na mbegu wilayani humo, lengo ikiwa ni kuhakikisha kwamba wananchi wa wilaya hiyo wanakuwa na chakula cha kutosha.

Monday, February 15, 2016

SERIKALI KUPELEKA MADAKTARI BINGWA MAENEO YA PEMBEZONI IKIWEMO MKOA WA RUVUMA

 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla akiangalia moja ya vitanda vinavyotumika katika upasuaji Hospitali ya mkoa wa Ruvuma, ambapo aliambiwa changamoto kubwa baadhi ya taa za vitanda hivyo kuwa na hitilafu.


Na Mwandishi wetu,
Songea.

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Dkt. Hamis Kigwangalla amesema wizara yake itahakikisha inapeleka Madaktari bingwa katika mikoa mbalimbali hapa nchini, ikiwemo hospitali ya mkoa wa Ruvuma, ili kuweza kuleta ufanisi mzuri wa utendaji kazi katika sekta hiyo ya afya.

Hayo yalisemwa na Dkt. Kigwangalla wakati alipokuwa katika ziara yake mkoani humo, aliyoifanya mapema hivi karibuni Februari 13 mwaka huu.

WATUMISHI WANNE HALMASHAURI SONGEA WATUMBULIWA MAJIPU



Na Kassian Nyandindi,
Songea.

WATUMISHI wanne waliopo katika Halmashauri ya wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, wamesimamishwa kazi na Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo kutokana na utovu wa nidhamu, wakidaiwa kufanya ubadhirifu wa fedha na kushindwa kusimamia kikamilifu majukumu yao ya kazi za utumishi wa umma.

Imefafanuliwa kuwa waliosimamishwa kazi kuwa ni wa idara ya ujenzi, maji, ushirika pamoja na Mwanasheria wa Halmashauri hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Songea, Rajabu Mtiula alisema kuwa baraza lake limefikia maamuzi hayo baada ya kuridhika na taarifa ya kamati ya fedha, uchumi na mipango kwamba watumishi hao, wanatuhumiwa kutumia vibaya madaraka yao na kuisababishia hasara halmashauri hiyo.

Mtiula aliwataja  watumishi waliosimamishwa kuwa ni mhandisi wa ujenzi Daud Basilio, mhandisi  wa maji John Undili, ofisa ushirika Sheken Masawe pamoja na Mwanasheria wa Halmashauri hiyo, Hotay Thuway ambapo kila mmoja alikuwa na tuhuma zake za ubadhirifu.

SERIKALI MKOANI IRINGA YAAGIZA KUFUNGWA KWA SHULE ZA MSINGI KUTOKANA NA MLIPUKO WA KIPINDUPINDU



Iringa.

SERIKALI mkoani Iringa imeagiza kufungwa kwa  shule zote za msingi, katika kata tatu za tarafa ya Pawaga baada ya moja ya vijiji vyake, kukumbwa na mlipuko wa ugonjwa kipindupindu.

Mpaka jana idadi ya watu waliopatwa na maambukizi ya ugonjwa huo, iliongezeka hadi 161 kutoka watu 85 walioripotiwa juzi huku mapambano dhidi ya ugonjwa huo, yakiendelea pamoja na baadhi ya wananchi wa vitongoji vya tarafa hiyo kuzingirwa na maji kutokana na mafuriko.

Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza.
Mbali na kuagiza shule hizo zifungwe, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amewataka wenye mashamba ya mpunga katika kijiji cha Mboliboli  ambacho ugonjwa huo umelipuka, kujitokeza mara moja ili kuisadia serikali  kuwaondoa vibarua waliobaki katika mashamba yao ili wasalimike na maambukizi yake.

Alisema vibarua katika mashamba hayo wanatoka katika wilaya za Kilolo mkoani Iringa, huku wengine wakiripoti kutoka katika mikoa ya Mbeya na Morogoro. 

MKURUGENZI WA KANDA MSD NA WENZAKE WASIMAMISHWA KAZI

Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.


Dar es Salaam,

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Kanda, huduma kwa wateja  Bohari kuu ya Dawa (MSD) hapa nchini, Cosmas Mwaifwani (pichani juu) na wenzake watatu kwa tuhuma za ubadhirifu wa shilingi bilioni 1.5.

Sunday, February 14, 2016

TASAF MBINGA YAJIVUNIA MAFANIKIO YAKE WANUFAIKA WAISHUKURU SERIKALI



Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

WANUFAIKA waliopo kwenye mpango wa uhaulishaji fedha, kaya maskini katika wilaya ya Mbinga vijijini na Halmashauri ya mji wa Mbinga mkoani Ruvuma, ambao unatekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF) awamu ya tatu, wameishukuru serikali ya awamu ya nne kwa kubuni na kuwapelekea mradi huo katika maeneo yao mbalimbali wilayani humo.

Jumla ya kaya 10,436 zilizopo katika kata zote za wilaya hizo, zimewezeshwa fedha shilingi milioni 394,972,000 kwa ajili ya huduma za afya, elimu na kupewa ruzuku ya msingi ambayo huwawezesha kujiongezea kipato katika maisha yao ya kila siku.

Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF nchini, Ladislaus Mwamanga.
Aidha wanufaika hao, wametaja baadhi ya miradi ambayo wameianzisha na kuanza kuwaletea maendeleo katika maisha yao baada ya kupokea fedha hizo kutoka TASAF kuwa ni ufugaji wa mbuzi, nguruwe, samaki, kuku, na matibabu huku wengine wakinunua vifaa vya ujenzi wa nyumba zao.

Wananchi hao walitoa shukrani hizo, walipokuwa kwenye mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi aliyetembelea vijiji vya Lazi, Mpapa, Ruanda, Mkwaya na Chunya wilayani humo.

Wakifafanua maelezo yao kwa nyakati tofauti, wanufaika hao walisema tangu kuanzishwa kwa mradi huo hadi sasa baadhi yao wameweza kumudu gharama za maisha yao ikiwemo kujikwamua na umaskini waliokuwa nao, hususani katika suala zima la kupeleka watoto wao shule.

WASIOPELEKA WATOTO WAO SHULE SONGEA WATAFUTIWA MWAROBAINI



Na Kassian Nyandindi,
Songea.

MKUU wa wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, Benson Mpesya amewataka wazazi ambao hawajapeleka watoto wao shule wilayani humo watekeleze agizo la serikali la kupeleka watoto hao shule haraka iwezekanavyo, ifikapo mwishoni mwa mwezi huu kabla hawaja chukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kufikishwa Mahakamani.

Rai hiyo ilitolewa na Mkuu huyo wa wilaya, alipokuwa kwenye ziara yake ya kikazi katika kata ya Mpitimbi na Litapwasi wilayani humo akizungumza na wazazi, walimu, watendaji wa vijiji na kata pamoja na madiwani.

Aidha aliwataka watendaji wa kata na vijiji wakiwemo maofisa tarafa wilayani Songea kwamba, ifikapo mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu wahakikishe watoto wote waliochaguliwa kuanza elimu ya msingi na sekondari ambao hawaja ripoti shule, wakamatwe mara moja na kuchukuliwa hatua za kisheria. 

Saturday, February 13, 2016

JIPU LATUMBULIWA SONGEA MHANDISI WA UJENZI ASIMAMISHWA KAZI



Na Kassian Nyandindi,

Songea.

HALMASHAURI ya wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, kupitia baraza lake la Madiwani wa Halmashauri hiyo limemsimamisha kazi Mhandisi wa idara ya ujenzi Daud Basilio, kwa sababu ya uzembe wa kutokuwa kazini kwa muda mrefu, ubadhirifu wa fedha na kutokuwa makini katika kusimamia miradi mbalimbali ya idara hiyo.

Akitoa taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari ofisini kwake, Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Rajabu Mtiula alisema, pia wamechukua hatua hiyo baada ya mhandisi huyo, kuisababishia halmashauri hasara ya shilingi milioni 38,186,400.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Mtiula alisema kuwa katika kikao chake cha dharula kilichoketi juzi mjini hapa, kimeamua kumweka pembeni mhandisi Basilio kutokana na licha ya kuonywa mara kwa mara na baraza hilo la madiwani, amekuwa akipuuza na kushindwa kutekeleza wajibu wake ipasavyo, ikiwemo kushindwa kusimamia kikamilifu miradi mbalimbali ya wananchi inayotekelezwa katika idara ya ujenzi.

Alifafanua kuwa mhandisi huyo, amekuwa akitumia taaluma yake vibaya ambapo amekuwa akishirikiana na wakandarasi kuihujumu halmashauri na kuisababishia hasara kubwa ya fedha, kitendo ambacho kinawakosesha wananchi kupata huduma stahiki.

MIEZI SITA JELA KWA KUMILIKI SILAHA KINYUME NA TARATIBU ZA NCHI



Na Steven Augustino,
Tunduru.

MKAZI mmoja anayeishi mtaa wa Misufini Tunduru mjini hapa mkoani Ruvuma, Mohamed Rashid Linyama (42) amehukumiwa kutumikia kifungo cha miezi sita jela baada ya kupatikana kosa la kukutwa na silaha kinyume cha  sheria na taratibu za nchi, juu ya umiliki halali wa silaha na risasi zake.

Adhabu hiyo imetolewa na Mahakama ya wilaya ya Tunduru, na kutoa amri ya kutaifishwa kwa bunduki hiyo na kuwa mali ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hakimu wa  Mahakama ya wilaya hiyo, Gladys Barthy alitoa hukumu hiyo baada ya mtuhumiwa kukiri kufanya kosa hilo na kuifanya Mahakama kumtia hatiani kwa kosa lililokuwa likimkabili.

Awali akisoma shikata hilo lenye jinai namba 4/2016 mwendesha mashtaka  wa Mahakama hiyo, mkaguzi msaidizi wa Polisi Inspekta Songelael Jwagu alisema kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Disemba 31 mwaka jana, akiwa na  bunduki katika kijiji cha Likweso majira ya asubuhi.

Katika hati ya mashtaka hayo mtuhumiwa  Linyama pia alikuwa na shitaka namba 2/2016 lililokuwa likimkabili juu ya wizi wa pikipiki aina ya Sunlg, yenye namba za usajili MC 670 ACG aliyokutwa akiwa anaitumia siku alipokamatwa na bunduki hiyo, kosa ambalo nalo liliondolewa baada ya mmliki wa pikipiki hiyo, kujitokeza na kukabidhiwa.

WATENDAJI WAPANDISHWA KIZIMBANI TUNDURU KWA WIZI WA PEMBEJEO ZA KILIMO



Na Steven Augustino,
Tunduru.

HALMASHAURI ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, imewafikisha Mahakamani watendaji wake sita wa wilaya hiyo, wakituhumiwa kuhujumu mfumo wa ugawaji wa pembejeo za kilimo kwa wakulima.

Watendaji hao wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya wilaya hiyo, na kwamba kila mmoja wao, anatuhuma ya kujibu makosa mawili yanayowakabili Mahakamani hapo.

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka yao, watuhumiwa hao wanakabiliwa na makosa ya kula njama kinyume na kifungu cha sheria namba 384 cha sheria za kanuni ya adhabu sura ya 16, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Vilevile kwa kosa la pili linalowakabili ni kwamba, watendaji hao wametumia mbinu za wizi kuiba vocha za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilizopangwa kuwapelekea wanufaika yaani wakulima, kupitia mfumo wa ruzuku wa pembejeo za kilimo.

Friday, February 12, 2016

SERIKALI YAWASIMAMISHA KAZI WATENDAJI WAKALA WA VIPIMO HAPA NCHINI

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitaka maelezo kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo na Mizani, Bibi Magdalena Chuwa  kuhusu sababu zilizomfanya azuie matumizi ya flow Meter katika kuhakiki kiwango cha mafuta yanayoingia nchini kupitia bandari ya Dar es salaam, wakati alipofanya ziara ya kushitukiza kwenye badanri hiyo Februari 11, mwaka huu. 


Dar es Salaam,

SERIKALI imeamua kuwasimamisha kazi watendaji wawili kutoka Wakala wa Vipimo nchini (WMA) kuanzia leo hii, ili kupisha uchunguzi wa upotevu wa mafuta bandarini kutokana na zuio la kufunga kwa mita kwa zaidi ya miaka mitano.

Waliosimamishwa kazi ni Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo nchini (WMA), Bi. Magdalena Chuwa na Meneja Vipimo Kitengo cha Bandari, Bi. Bernadina Mwijarubi. Bi. Mwijarubi ndiye anashughulikia kitengo cha mafuta bandarini.

Akitangaza uamuzi huo kwenye kikao cha Makatibu Wakuu kilichofanyika leo (Ijumaa, Februari 12, 2016) ofisini kwake Magogoni jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemwagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Dk. Adelhelm Meru awaandikie barua za kuwasimamisha kazi ili kupisha uchunguzi huo.

“Katibu Mkuu Viwanda, waandikie barua za kuwasimamisha kazi ili kupisha uchunguzi. Katika kipindi hiki hawatatakiwa kusafiri kwenda popote hadi uchunguzi utakapokamilika. Pia utafute mtu wa kukaimu nafasi hiyo ili kazi ziendelee,” alisema.

MKUU WA WILAYA MBINGA AWATAKA VIONGOZI KUACHA TABIA YA KUJIKWEZA NA KUWA MIUNGU WATU



Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

SENYI Ngaga ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, amewataka viongozi wa wilaya hiyo kuacha tabia ya kujikweza na kuwa miungu watu badala yake wajenge ushirikiano na wananchi katika kutatua kero mbalimbali kwa wakati, ili waweze kuendana na kasi ya utendaji kazi wa serikali hii ya awamu ya tano.

Ngaga alisema kuwa ni jukumu la kila kiongozi wilayani humo kujituma kikamilifu katika utekelezaji majukumu ya wananchi, huku akisisitiza suala la ukusanyaji wa mapato kikamilifu na kuzuia mianya ya upotevu wa mapato hayo.
Mkuu wa wilaya ya Mbinga, Senyi Ngaga.

“Mkurugenzi na wataalamu wako, nawaagiza simamieni kikamilifu kipengele hiki cha ukusanyaji mapato kwa kutumia mifumo ya kisasa ambayo serikali imeagiza, pia kuweni  wabunifu wa vyanzo vipya vya mapato ili kuweza kuongeza kiasi cha fedha ambazo zitaweza kuhudumia jamii katika shughuli mbalimbali za maendeleo”, alisisitiza Ngaga.

Mkuu huyo wa wilaya ya Mbinga, alitoa rai hiyo juzi alipokuwa akitoa salamu za serikali katika kikao cha kawaida cha baraza la madiwani la wilaya hiyo, kilichoketi kwenye ukumbi wa Umati uliopo mjini hapa.

Thursday, February 11, 2016

WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA YA KUSHITUKIZA BANDARINI AMPA MASAA MANNE MTENDAJI MKUU WAKALA WA VIPIMO AANDIKE BARUA YA KUJIELEZA

Dar es Salaam,

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amefanya ziara ya ghafla kwenye kitengo cha upimaji mafuta bandarini (Oil Flow Metres) na kukuta zimejaa kutu baada ya kutelekezwa kwa miaka zaidi ya mitano. Pia alitembelea mita za kupimia mafuta zinazoendelea kujengwa Kigamboni. 
 
Aidha, Waziri Mkuu amempa saa nne tu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo nchini (WMA), Bi. Magdalena Chuwa aandike barua ya kujieleza ni kwa nini aliamua kufunga mita hizo zisitumike kwa zaidi ya miaka mitano iliyopita na amletee barua hiyo ofisini kwake ifikapo saa 11 leo jioni. 
 
“Nataka unieleze ni kwa nini ulitoa maelekezo ya kufunga mita hizo, na kwa nini jana uliamua kubadili uamuzi huo? Ni kwa nini umeamua kuchukua maamuzi haya baada ya kupokea ujumbe wa simu ya mkononi (sms) wakati mita zimekaa bila kufanya kazi kwa miaka mitano? Ni kwa nini umeamua kufanyia kazi ujumbe wa sms wakati unajua Serikali inafanya kazi kwa maandishi rasmi?” alisema Waziri Mkuu. 
 
“Umesema mlikuwa mnatumia utaratibu wa kupima kwa kijiti. Huu hauna uhakika na huwezi kutegemea taarifa ya mtu mwingine au kuingia kwenye meli ya mtu na kuanza kuchukua vipimo hadi ujiridhishe. Nataka kujua ni kwa nini mlikuwa na utaratibu wa ku-bypass mafuta ili yasipite kwenye mita za kupimia mafuta? Ni kwa nini umetoa amri zianze kutengenezwa jana na siyo mwaka 2012 au 2013?” alihoji Waziri Mkuu. 

MADIWANI SONGEA WATUMBUA JIPU WAMSIMAMISHA KAZI MHANDISI MAJI KUTOKANA NA UZEMBE KAZINI

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Said Thabit Mwambungu.

Na Kassian Nyandindi,

Songea.

BARAZA la Madiwani Halmashauri wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, limemsimamisha kazi Kaimu Mhandisi wa idara ya maji wilayani humo, John Undili kwa sababu ya uzembe na kutokuwa makini katika kusimamia miradi mbalimbali ya maji na kuisababishia Halmashauri hiyo, hasara ya mamilioni ya fedha.

Akitoa taarifa hiyo kwenye baraza hilo lililoketi mjini hapa, Mwenyekiti wake Rajabu Mtiula alisema mhandisi huyo licha ya kuonywa mara kwa mara na baraza lake, amekuwa akipuuza kutekeleza wajibu wake wa utumishi wa umma na maelekezo anayopewa na viongozi wake wa ngazi ya juu ndani ya halmashauri hiyo.

Mwenyekiti huyo alifafanua kwamba waliona ni vyema achukuliwe hatua hiyo ya kinidhamu, ili kuweza kunusuru hali hiyo isiweze kuendelea na iwe fundisho kwa watumishi wengine wa wilaya hiyo, wenye tabia ya kuzembea kutimiza majukumu yao ya kazi ipasavyo.

Mtiula ambaye pia ni Diwani wa kata ya Litapwasi, alibainisha kuwa Mhandisi huyo alishindwa kusimamia miradi ya maji katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Disemba mwaka jana, kitendo ambacho kimesababisha hata wananchi wake wakose huduma ya maji safi na salama.

MAHABUSU ALIYEJINYONGA NAMTUMBO UTATA MTUPU



Na Kassian Nyandindi,
Songea.

MTUHUMIWA mmoja ambaye aliwekwa rumande katika mahabusu ya kituo kidogo cha Polisi kata ya Lusewa wilayani Namtumbo mkoa wa Ruvuma, amekutwa akiwa amejinyonga na kufariki dunia, ndani ya chumba cha mahabusu hiyo.

Taarifa za tukio hilo zinafafanua kuwa, Vumi Issa Kasumali (30) ambaye ni mkazi wa kata ya Msisima wilayani humo, ndiye aliyepoteza uhai wake kwa kujinyonga kwa kutumia suruali, aliyokuwa amevaa mwilini  mwake.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Zuberi Mwombeji amethibitisha juu ya tukio hilo na kueleza kwamba, lilitokea majira ya mchana Februari 9 mwaka huu.

Mwombeji alieleza kuwa mtuhumiwa huyo, alikuwa anakabiliwa na tuhuma ya kuvunja nyumba na kuiba na kwamba wakati anachukua maamuzi magumu ya kujiua, askari Polisi walikuwa wanajiandaa kumsafirisha kwenda Mahakama ya wilaya Namtumbo ili aweze kujibu tuhuma zinazomkabili.

MADIWANI MBINGA WAPITISHA BAJETI SHILINGI BILIONI 49.4 KWA AJILI YA UTEKELEZAJI MAENDELEO YA WANANCHI KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga vijijini mkoani Ruvuma, Venance Mwamengo (upande wa kulia) akisisitiza jambo katika kikao cha baraza la madiwani la wilaya hiyo. Katikati ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Ambrose Nchimbi na Makamu wake Bernad Komba. 


Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

HALMASHAURI ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, katika rasimu yake ya bajeti ya mwaka 2016/2017 imekisia kukusanya na kutumia kiasi cha shilingi bilioni 49.4 kwa ajili ya utekelezaji na kuboresha shughuli mbalimbali, za maendeleo ya wananchi wilayani humo.

Katika fedha hizo shilingi bilioni 32.5 zinalenga kulipa mishahara ya wafanyakazi wake, bilioni 3.9 matumizi mengine, bilioni 9.0 ni fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Aidha imekisia kukusanya na kutumia shilingi bilioni 3.8 ambazo ni fedha zitakazotokana na makusanyo ya ndani, katika halmashauri ya wilaya hiyo. 

Tuesday, February 9, 2016

WANAFUNZI NAKAPANYA TUNDURU WAISHI KWA HOFU KUTOKANA NA KUSUMBULIWA NA HOMA YA MATUMBO

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Said Thabit Mwambungu.


Na Steven Chindiye,
Tunduru.

WANAFUNZI wanaosoma katika shule ya Sekondari Nakapanya Wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, wanaishi kwa hofu kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa homa ya matumbo ambayo imezuka shuleni hapo.

Hayo yalibainishwa na wananafunzi hao, walipokuwa wakizungumza na mwandishi wa habari hizi na kuongeza kuwa, hofu hiyo imetokana na wenzao 56 kuanza kuugua ugonjwa wa kuharisha mfululizo.

Walisema kufuatia mlipuko huo, timu ya wataalamu wa afya kutoka hospitali ya wilaya hiyo ikiongozwa na Kaimu mganga mkuu wa wilaya, Dkt. Bernad Mwamanda walienda huko na kutoa huduma kwa wagonjwa walioathirika ambapo pamoja na mambo mengine, timu hiyo pia ilichukua sampuli kwa ajili ya kwenda kufanyia uchunguzi zaidi ili kuweza kutafuta na kupatikana ufumbuzi wa tatizo hilo.

MVUA ILIYOAMBATANA NA UPEPO MKALI YABOMOA NYUMBA ZA WANANCHI TUNDURU WAKOSA MAHALI PA KUISHI



Na Steven Chindiye,
Tunduru.

MVUA iliyoambatana na upepo mkali iliyonyesha katika vijiji vya Marumba na Morandi, wilaya ya Tunduru mkoa wa Ruvuma imeezua na kubomoa nyumba 62 za wananchi na kuwaacha wakiwa hawana mahali pa kuishi.

Taarifa za tukio hilo zinafafanua kwamba mvua hiyo ilianza kunyesha majira ya saa 10 za jioni February 6 mwaka huu, ambazo ziliambatana na radi huku upepo mkali ukianza kuezua mapaa ya nyumba hizo.

Walisema kufuatia hali hiyo, watu waliokumbwa na adha hiyo walianza kukimbia huku na huko wakiwa wanapita kuomba msaada wa kujihifadhi kwa majirani na ndugu zao.

Monday, February 8, 2016

AHADI YA MAGUFULI SHILINGI BILIONI 12.3 UENDESHAJI MAHAKAMA YATIMIA LEO

Waziri wa Fedha na Mipango, Philip Mpango (Katikati) akiwakabidhi Naibu waziri wa katiba na sheria, Amon Mpanju (kulia) na Mtendaji mkuu wa Mahakama Tanzania, Hussein Kattanga cheki ya shilingi Bilioni 12 na milioni mia tatu ikiwa ni kutimiza ahadi  ya Rais Dkt. John Pombe Josef Magufuli aliyoahidi siku alipokuwa mgeni rasmi siku ya Mahakama hapa nchini ikiwa ni siku tano tangu alipotoa ahadi hiyo.


MAGUFULI ATANGAZA KIAMA KWA WATU HAWA, AWATAKA WAJISALIMISHE HARAKA


Sunday, February 7, 2016

ATIWA MBARONI KWA KUFANYA MAPENZI NA WANAFUNZI WATATU



Na Kassian Nyandindi,
Songea.

JESHI la Polisi mkoani Ruvuma, limemtia mbaroni Kassim Millinga (52) ambaye ni mkazi wa Lizaboni Manispaa ya Songea mkoani humo, kwa tuhuma za kuwabaka wanafunzi watatu wanaosoma darasa la sita shule ya msingi ya Kibulang`oma iliyopo mjini hapa.

Akizungumza na gazeti hili Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Zuberi Mwombeji alisema kuwa tukio hilo limetokea kwa nyakati tofauti katika eneo la Lizaboni jirani na shule hiyo wanayosoma wanafunzi hao, ambao wote wana umri wa miaka 12 kila mmoja na majina yao yamehifadhiwa.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma, Zuberi Mwombeji.
Kamanda huyo wa Polisi alisema kuwa Millinga ambaye pia anafanya kazi ya ulinzi kwenye kampuni ya ulinzi ya Ilonjezi iliyopo mjini Songea, anatuhumiwa kwamba kwa nyakati tofauti tangu mwaka jana amekuwa akiwarubuni wanafunzi hao kwa kuwapa pesa, chakula na nguo kisha kuwalazimisha kufanya nao mapenzi kwenye nyumba anayoishi huku akiwatishia kutosema kwa mtu yeyote kuhusiana na kitendo hicho anachowafanyia.

VURUGU ZAKWAMISHA UCHAGUZI CHUO KIKUU SONGEA



Na Mwandishi wetu,

Songea.

UCHAGUZI Mkuu wa serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Mtakatifu Joseph tawi la Songea mkoani Ruvuma, umeshindwa kufanyika kwa kile kinachodaiwa kuwa uongozi husika wa chuo hicho umekuwa ukiingilia na kutaka kupanga safu ya uongozi wanaoutaka wao, huku wanachuo wakishindwa kuwa huru kuchagua kiongozi wanayemtaka.

Kufuatia kuwepo kwa hali hiyo, kumesababisha vurugu za hapa na pale katika eneo hilo la chuo, ambazo zilipelekea mmoja wa viongozi wa chuo hicho ambaye ni mtawa aliyefahamika kwa jina moja la Magdalena, raia wa kutoka nchi ya India kunusurika kipigo kutoka kwa wanafunzi wakati alipokuwa akitangaza uchaguzi huo hautafanyika.

Habari zaidi kutoka kwenye chuo hicho zinaeleza kuwa, mapema miezi mitatu iliyopita wanafunzi wa chuo hicho walitangaziwa kuwa mwanachuo yeyote anayetaka uongozi achukue fomu ya kugombea, na hili lilitokana baada ya uongozi uliokuwa madarakani kuisha muda wake wa utawala.

Wanachuo hao ambao waliomba majina yao yahifadhiwe, waliwaambia waandishi wa habari kuwa baadaye mchakato wa kuwapata viongozi uliendelea ambapo wagombea walijitokeza na kuanza kufanya kampeni za kuomba wachaguliwe kwa nafasi walizoomba.

Friday, February 5, 2016

WALIOBOMOLEWA NYUMBA TUNDURU KUPISHA UJENZI WA BARABARA KULIPWA FIDIA ZAO

Rais mstaafu Dokta Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) na aliyekuwa balozi mdogo wa Japan hapa nchini Kazuyoshi Matsunaga (wa tatu kushoto) wakishirikiana kukata utepe ikiwa ni ishara ya kuzindua ujenzi wa barabara ya Tunduru-Mangaka Matemanga mradi unajengwa na Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano wa serikali ya Japan kupitia shirika lake la kimataifa la maendeleo JICA. Tukio hilo lilifanyika mwaka 2014.

Na Steven Augustino,
Tunduru.

IMEELEZWA kuwa wahanga 280 ambao walibomolewa nyumba zao, kwa lengo la kupisha ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami katika vijiji vilivyopo kwenye tarafa ya Nakapanya wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, hivi sasa wameweza kutimiza vigezo vya kuishawishi serikali kulipwa fidia zao.

Kwa mujibu wa taarifa iliyoufikia mtandao huu, imefafanuliwa kuwa wahanga hao ni kati ya wananchi 352 ambao walipeleka malalamiko yao, ya kuomba kuongezewa fidia kwa madai kwamba awali hawakuridhishwa na malipo ya fidia waliyolipwa awamu ya kwanza.

Taarifa hiyo ilitolewa na mwakilishi wa dawati la kusikiliza migogoro kutoka makao makuu ya Wakala wa barabara hapa nchini (TANROADS), Gibson Mwaya wakati alipokuwa akitoa taarifa kwa wahanga hao, waliokuwa wamekusanyika katika viwanja vya ofisi ya Mkuu wa wilaya hiyo, kwa ajili ya kufuatilia hatima ya   madai yao.

JE INAWEZEKANA HATI KUWA NA MAJINA YA WANANDOA WOTE ?



Na Bashir Yakub,

HAKIMILIKI katika  masuala  ya  ardhi, huhusisha  umiliki  wa ardhi  zenye hati. Umiliki huu  hutoa  wajibu  na haki  fulani  kwa mmiliki  katika  ardhi husika, na sio rahisi kudai  kwamba una hakimiliki  katika  ardhi kama  hauna  hati.  

Aidha  tumezoea  kuona  hati  zilizo na  jina  la  mtu  mmoja mmoja. Hii  ni  hata  kwa  wanandoa ambao  hudai   mali  husika zinatokana  na  jasho lao wote. Lakini  je  unajua  kuwa  inawezekana   hati miliki  ikawa  na  majina  ya wanandoa  wote  badala  ya  kuwa na  jina la mmoja tu hasa baba ambao  ndio  wengi  hupenda  majina yao  yaonekane  hapo ?.  Jambo  hili  linawezekana na  linaruhusiwa.

1. HAKIMILIKI  YA  PAMOJA  KUONDOA  MGOGORO.

Kutoelewana  ambako  mara  kadhaa  hutokea  baada  ya  kifo  cha  mmoja  wa  wanandoa,  kunaweza   kuondolewa  na  umiliki  wa  ardhi  wa  pamoja. Ikiwa una  wasiwasi  juu  ya  mustakabali  wa  mali  hasa  ardhi huko  mbele,  ni  vyema  basi  ukachukua  hatua ya  kusajili  kwa umiliki  wa  pamoja.

Kama kiwanja / nyumba  ina  hati  yenye majina mawili, la baba na  mama halafu mmoja  wao akafariki itakuwa   ni  vigumu  ndugu  au  mwingine  yeyote  mwenye  nia  mbaya kudai  umiliki  wa kiwanja / nyumba hiyo.

Lakini hali  itakuwa  tofauti iwapo  hati  ina  jina  la  mmoja  na  huyo huyo mmoja  ndiye  aliyefariki. Hivyo pale  pote  ambapo  ndugu  walidhulumu  mali za marehemu  hasa  ardhi,  ni  pale  ambapo  kuna jina  la mmoja.

Mara  nyingi  fitina  huingia pale penye  mwanya  wa  kufanya  hivyo. Sio  rahisi  fitina kuingia  pasipo na  mwanya. Kuweka majina  ya  wanandoa wote  kwenye  hati  za  ardhi  ni  hatua  ya  kuziba  mwanya  wa  fitina.

Itawezekanaje  ndugu au mwingine  mwenye  nia  ovu kudai umiliki  wa  ardhi  ya marehemu huku  akijua  kuwa,  hati husika  inalo  jina  la  mke  pia.  Sio  rahisi  hata kidogo.

Lakini  pia  umiliki  wa  pamoja  huondoa  mgogoro  pale  panapokuwa na  talaka. Swali la kujiuliza je,  mwanandoa  fulani  amechangia  chochote  katika  kupatikana  kwa  mali  huwa  halipo  ikiwa  majina  yote  mawili  ya  wanandoa  yameonekana  kwenye  hati.