Thursday, November 7, 2013

MADIWANI TUNDURU WALIA NA SEHEMU YA KUJIFUNGULIA AKINA MAMA WAJAWAZITO, WENGINE WAJIFUNGULIA SAKAFUNI

Na Steven Augustino,
Tunduru.

MADIWANI wa viti maalumu katika halmashauri ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, wameomba kuridhia na kuruhusu kufunguliwa kwa wodi mpya iliyojengwa katika hospitali ya Wilaya hiyo kwa ajili ya kujifungulia akina Mama wajawazito, wanaoenda kupata huduma hiyo muhimu hospitalini hapo kwa kuanza. 


Kilio hicho kilianza kuwasilishwa na Diwani wa Viti maalumu wa Tarafa ya Matemanga Stawa Omari huku akiungwa mkono na Swema Kalipungu wa Tarafa ya Mlingoti na Alus Yunus wa Nalasi walisema hivi sasa hali ya akina mama hao ni tete kutokana na wengine hujifungua wakiwa wamelala chini sakafuni.
  

Madiwani hao walisema kuna wakati akina mama wajawazito wamekuwa wakijifungulia katika chumba cha kupokelewa wagonjwa. 


Walidai kuwa imefikia hatua wakati mwingine hata wagonjwa wanaoenda kupata matibabu hospitalini hapo hupata shida pale wanapohitaji huduma za vipimo choo ndogo na kubwa ambapo hulazimika kwenda vyoo vya nyumba za jirani kutokana na miundo mbinu ya hospitali hiyo kutotosheleza.


Walisema kila wanapohitaji maelezo kwa wataalamu husika wamekuwa wakiambiwa kuwa tatizo linalo wa kwaza ni kutokana na wodi hizo mpya kutokamilika miundo mbinu husika.

  
Aidha madiwani hao waliendelea kuiomba halmashauri kutenga eneo jingine la kujifungulia akina mama, ambao wanaenda kujifungua katika hospitali hiyo kujisitiri mahali pa zuri. 

No comments: