Wednesday, June 28, 2017

UZINDUZI WA SHUGHULI ZA CHUO KIKUU SOKOINE RUVUMA WAFANYIKA LEO MJINI SONGEA

Washiriki kutoka sekta mbalimbali wakishuhudia uzinduzi wa shughuli za Chuo Kikuu Cha Kilimo (SUA) ambazo zimefanyika leo Songea mjini mkoani Ruvuma. 
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Dkt. Binilith Mahenge upande wa kulia, akipeana mkono na mwakilishi wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) Profesa Peter Gillah leo mjini Songea wakati wa uzinduzi wa shughuli za SUA mkoani Ruvuma.
Na Mwandishi wetu,

Songea.

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Dkt. Binilith Mahenge amezindua shughuli za Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) mkoani Ruvuma, ambazo zinatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa baada ya taratibu husika kukamilika.

Uzinduzi huo umefanyika leo kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea uliopo mjini hapa ambapo ulishirikisha mwakilishi wa Mkuu wa chuo hicho, Profesa Peter Gillah.

Vilevile kulikuwa na Mkuu wa ndaki ya misitu, wanyamapori na utalii Profesa John Kessy.

RAIS MAGUFULI AKUTANA NA WATAALAMU WA NISHATI KUTOKA ETHIOPIA NA TANZANIA PAMOJA NA KAMATI YA UCHUNGUZI MCHANGA WA MADINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa maji, umwagiliaji na umeme wa Ethiopia Dkt. Seleshi Bekele anayeongoza ujumbe kutoka kwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo iliyopo hapa nchini kusaidia mchakato wa ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme la Steigler’s Gorge leo Ikulu Jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri wa maji, umwagiliaji na umeme wa Ethiopia Dkt. Seleshi Bekele na ujumbe kutoka kwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo iliyopo nchini kusaidia mchakato wa ujenzi wa Bwawa la kuzalisha umeme la Steigler’s Gorge leo  Ikulu Jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wajumbe wa Kamati mbili alizoziteua za uchunguzi wa mchanga wa Madini (Makinikia) leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa maji, umwagiliaji na umeme wa Ethiopia Dkt. Seleshi Bekele na ujumbe kutoka kwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo iliyopo nchini kusaidia mchakato wa ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mkono na Waziri wa maji, umwagiliaji na umeme wa Ethiopia Dkt. Seleshi Bekele baada ya kupata picha ya pamoja na ujumbe wake kutoka kwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo iliyopo nchini kusaidia mchakato wa ujenzi wa bwawa hilo wakiwa pamoja na jopo la wataalamu wa Tanzania wanaosimamia mradi huo leo Ikulu Jijini Dar es salaam. (Picha zote na Ikulu)


WAUMINI WA KIISLAMU WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MAMBO YANAYOKWENDA KINYUME NA MAFUNDISHO YA DINI YAO

Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu mtaa wa Making’inda Manispaa ya Songea wakifuatilia nasaha kutoka kwa Imamu wa Msikiti wa Making’inda Shehe Bashiru Matembo (hayupo pichani) wakati wa swala ya Ed el Fitri jana ambapo waumini hao waliaswa kuendeleza mambo mema waliyokuwa wakifanya wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Waumini wa Kiislamu kutoka mtaa wa Making’inda Manispaa ya Songea, wakitoka nje baada ya kuswali swala ya Ed el Fitri.
Na Muhidin Amri,    
Songea.

IKIWA ni siku chache zimepita katika kusherehekea sikukuu ya Idd el Fitri, Waislamu hapa nchini wametakiwa kujiepusha na mambo  yanayokwenda kinyume na mafundisho ya dini yao, ikiwemo matendo ya uzinzi na tabia ya  kujengeana fitina badala yake wanapaswa kuendelea kutenda mambo  mema waliyokuwa wakiyafanya wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Aidha wameombwa kudumisha upendo, undugu na mshikamano miongoni mwao na hata kwa watu wasiokuwa Waislamu hatua ambayo itasaidia kuwa na jamii ya watu wastaarabu ambao wakati wote wataishi na kumcha Mungu.

Imamu wa Msikiti wa Making’inda kata ya Msamala Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, Shehe Bashiru Yahay Matembo alisema hayo jana wakati akitoa nasaha kwa waumini wa kiislamu huku akisisitiza kuwa Waislamu wanapaswa kutumia sikukuu ya Idd el Fitri, kwa ajili ya kusameheana na kuomba msamaha kwa yule aliyemkosea  badala ya kuendeleza chuki na uhasama kati yao.

Sunday, June 25, 2017

KAMPUNI YA MANTRA TANZANIA LIMITED YATOA MSAADA SHULE ZA SEKONDARI NAMTUMBO

Na Kassian Nyandindi,    
Namtumbo.

SHULE ya Sekondari Korido iliyopo katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma imepata msaada wa shilingi milioni 18.7 kutoka Kampuni ya Mantra Tanzania Limited, ambazo zimetumika kukarabati chumba cha Maktaba na kununua vitabu kwa ajili ya kuweza kuinua na kuongeza kiwango cha taaluma kwa wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo.

Kampuni hiyo ambayo inafanya kazi ya kutafiti madini aina ya Uranium One katika mto Mkuju wilayani humo, ndiyo ambayo imetoa msaada huo ikiwemo sehemu ya fedha hizo zimetumika pia kununua vitabu 8,000 vya masomo ya aina mbalimbali.

Khadija Palangyo ambaye ni Afisa mahusiano wa Mantra Tanzania Limited, alisema hayo jana wakati alipokuwa akihojiwa na waandishi wa habari mjini hapa.

Vilevile alisema kuwa wamekuwa wakifanya shughuli za kimaendeleo wilayani humo katika jamii ikiwemo utoaji wa misaada kama vile ujenzi wa madarasa shuleni, visima vya maji na utengenezaji wa madawati.

SUPER FEO YAUA TENA SONGEA NA ABIRIA KUJERUHIWA VIBAYA


Na Mwandishi wetu,    
Songea.

HASSAN Ngonyani (25) mkazi wa kijiji cha Likalangiro wilaya ya Songea mkoani Ruvuma ambaye ni Kondakta wa basi la Kampuni ya Super Feo amefariki dunia, huku baadhi ya abiria waliopanda gari hilo nao wamejeruhiwa vibaya baada ya kupata ajali katika eneo la Hanga Ngadinda halmashauri ya wilaya ya Madaba mkoani humo.

Basi hilo ambalo lilikuwa limebeba zaidi ya abiria 40 likitokea Mbeya kwenda Songea mjini, kati ya hao abiria wanne ndiyo waliojeruhiwa vibaya.

Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Gemin Mushi alisema kuwa tukio hilo lilitokea Juni 24 mwaka huu majira ya mchana katika eneo hilo, ambapo aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni Winde Philipo (16) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya sekondari ya wasichana Manyunyu iliyopo wilaya ya Ludewa mkoa wa Njombe.

Saturday, June 24, 2017

DIWANI WA CHAMA CHA MAPINDUZI HALMASHAURI WILAYA YA MBINGA AFARIKI DUNIA

Na Kassian Nyandindi,     
Mbinga.

DIWANI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Mhongozi, Emeran Cyprian Mapunda (54) katika Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma amefariki dunia katika Hospitali ya Misheni Peramiho iliyopo mkoani humo, ambako alikuwa akipatiwa matibabu.

Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo, Ambrose Nchimbi alimweleza mwandishi wetu kuwa diwani huyo amefikwa na mauti usiku wa Juni 23 mwaka huu wakati alipokuwa katika hospitali hiyo.

Nchimbi alifafanua kuwa kufariki kwa diwani Mapunda kumesababishwa na tukio la kuanguka Juni 22 mwaka huu akiwa amepanda juu ya mti, wakati alipokuwa akisafisha shamba lake la kahawa katika kijiji cha Mhongozi kilichopo kwenye kata hiyo.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWATAKA TRA WASIWATOZE KODI YA MAJENGO WAZEE WENYE UMRI WA MIAKA 60

Na Mwandishi maalum,
Chato.

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewataka maafisa wa Mamlaka ya Mapato hapa nchini (TRA) wakusanye kodi za majengo kwa kuzingatia sheria na wasiwatoze kodi ya majengo Wazee wenye umri zaidi ya miaka 60.

Alitoa agizo hilo juzi wakati alipokuwa akizungumza na wananchi na viongozi wa wilaya ya Chato mkoa wa Geita ambao walihudhuria uzinduzi wa jengo la Mamlaka ya mapato wilayani humo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

“TRA ijipange upya namna ya kukusanya kodi za majengo kuanzia Julai Mosi mwaka huu, katika kutekeleza jukumu hili zingatieni sheria na taratibu husika zilizowekwa tusisikie mnawadai kodi ya majengo wazee wenye umri zaidi ya miaka 60 kwa majengo ambayo wanayatumia kama makazi yao,” alisisitiza Majaliwa.

Waziri Mkuu Majaliwa aliwataka pia maafisa hao wakusanye kodi ya majengo kwenye maeneo ya mjini na siyo vijijini kwani kodi hiyo haiwahusu.

DEREVA APOTEZA MAISHA ABIRIA WAJERUHIWA VIBAYA BAADA YA BASI KUGONGANA USO KWA USO NA LORI LILOBEBA MAKAA YA MAWE

Na Mwandishi wetu,   
Songea.

DEREVA wa Kampuni ya Super Feo, Ismail Shaban Nyami (38) mkazi wa Bombambili Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, amefariki dunia papo hapo baada ya basi alilokuwa akiendesha kugongana uso kwa uso na lori ambalo limebeba makaa ya mawe na kusababisha abiria kumi na moja kujeruhiwa vibaya.

Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Gemin Mushi alisema hayo wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari mjini hapa huku akieleza kuwa tukio hilo lilitokea Juni 22 mwaka huu majira ya jioni katika eneo la Msalaba, lililopo katika kijiji cha Mbangamawe barabara ya kutoka Songea kwenda Njombe na kwamba abiria hao wamelazwa katika hospitali ya mkoa Songea.

Alilitaja gari ambalo lilikuwa limebeba abiria hao kuwa ni lenye namba za usajili T 213 BNU aina ya Yutong ambapo liligongana na gari lenye namba za usajili T 159 CEX aina ya Iveco Stralis likiwa lenye tela namba za usajili T 206 CHS mali ya Kampuni ya Trank Link Limited ya Jijini Dar es Salaam.

Thursday, June 22, 2017

RAIS DOKTA MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI KIWANDA CHA MATUNDA SAYONA CHALINZE MKOANI PWANI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua kiwanda cha Viuadudu cha Kibaha mkoani Pwani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kiwanda cha Matunda cha Sayona Fruits, kilichopo Mboga Chalinze mkoani Pwani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wakazi wa Kiwangwa wakati akielekea kufungua barabara ya Bagamoyo - Msata mkoani Pwani. (Picha na Ikulu)

RAIS DOKTA MAGUFULI AFUNGUA BARABARA YA BAGAMOYO MSATA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe pamoja na Mama Salma Kikwete (Mbunge), Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge miundombinu Profesa Norman Sigala, Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, kuashiria ufunguzi wa barabara ya Bagamoyo - Makofia Msata yenye urefu wa kilometa 64 katika eneo la daraja la Ruvu chini Bagamoyo mkoani Pwani. Wengine katika picha ni Mkuu wa mkoa wa Pwani Injinia Evarist Ndikilo, Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Injinia Joseph Nyamhanga, Mbunge wa Chalinze Ridhiwan Kikwete, Katibu wa itikadi na uenezi CCM Hamphrey Polepole pamoja na viongozi wengine wa Serikali.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na viongozi wengine wa serikali na Wabunge, akivuta kitambaa kuashiria jiwe la ufunguzi wa barabara ya Bagamoyo - Makofia Msata yenye urefu wa kilometa 64 katika eneo la daraja la Ruvu chini, Bagamoyo mkoani Pwani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Waziri wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Profesa Makame Mbarawa mara baada ya kuweka jiwe la ufunguzi wa barabara ya Bagamoyo - Makofia Msata yenye urefu wa kilometa 64 katika eneo la daraja la Ruvu chini, Bagamoyo mkoani Pwani.
Sehemu ya barabara hiyo ya Bagamoyo - Makofia Msata kama inavyoonekana katika picha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza kabla ya kufungua barabara ya Bagamoyo - Makofia Msata katika eneo la daraja la Ruvu chini, Bagamoyo mkoani Pwani.(Picha zote na Ikulu)

KATIBU MKUU UTUMISHI WA UMMA ASISITIZA NIDHAMU KWA VIONGOZI NA WATENDAJI WA SERIKALI HAPA NCHINI

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Singida (hawapo pichani) kama sehemu ya maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma.
 Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Singida, wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro alipowatembelea katika kuadhimisha wiki ya utumishi umma.
Na Mwandishi wetu,
Singida.

KATIBU Mkuu Ofisi ya Rais Menejiment ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro amewataka viongozi na watumishi wote hapa nchini, kuzingatia nidhamu na maadili ya utumishi wa umma ikiwa ndiyo msingi bora wa utendaji kazi ili utumishi wao uweze kuwa mzuri.

Dkt. Ndumbaro alisema hayo leo alipokutana na watumishi wa mkoa wa Singida na kusikiliza matatizo, kero, changamoto pamoja na kupata maoni ya namna ya kuboresha utumishi wa umma kama sehemu ya maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma nchini.

Alisema kuwa kila mtumishi anapaswa kufanya kazi kwa bidii na nidhamu ya hali ya juu huku akisisitiza viongozi hasa wa watumishi wa umma, kuwasikiliza watumishi wao pale wanapotoa maoni yao bila kuyapuuza au kuwakatisha tamaa kwa vitisho.

Wednesday, June 21, 2017

DOKTA MWAKYEMBE AKUTANA NA WASANII WA FILAMU NA WAANDISHI WA HABARI WA A FM BUNGENI DODOMA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (Katikati) akiwa na Waandishi wa habari wa A Fm Radio walipomtembelea leo Bungeni Dodoma.
Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura wakiwa katika picha ya pamoja na wasanii wa Filamu Nice Mtunze na Bi Lydia Mgaya walipowatembelea leo Bungeni.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura wakiwa katika picha ya pamoja Waandishi wa habari wa A Fm Radio walipomtembelea leo Bungeni Dodoma.

WAPOTEZA MAISHA BAADA YA GARI NA TELA LAKE KUACHA NJIA NA KUPINDUKA

Na Mwandishi wetu,    
Songea.

WATU   watatu wamefariki dunia katika matukio mawili tofauti likiwemo la wawili kufa papo hapo, baada ya gari lililokuwa na tela lake likiwa limesheheni makaa ya mawe kuacha njia na kupinduka kisha kutumbukia katika mto Nakatete uliopo Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Akizungumza na Waandishi wa habari Ofisini kwake, Kamanda wa Polisi wa mkoa huo Gemin Mushy aliwataja waliofariki dunia kuwa ni Shaban Msangi (39) ambaye alikuwa ni dereva wa gari hilo lililobeba makaa ya mawe, Haji Yusuph (18) alikuwa ni tingo wa gari hilo wote ni wakazi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani na Cosmas Thadei (80) mkazi wa eneo la Sanangula Manispaa ya Songea.

Alifafanua kuwa katika tukio la kwanza inadaiwa kuwa Juni 20 mwaka huu majira ya usiku katika kijiji cha Utwango kata ya Namabengo wilayani Namtumbo, gari lenye namba za usajili T 767 DKS lililokuwa na tela lake lenye namba za usajili T 324 DKS aina ya HOWO mali ya Kampuni ya Dangote lilikuwa limebeba tani 25 za makaa ya mawe likitokea Songea kwenda Mtwara.

SONGEA WAMPONGEZA RAIS DKT. MAGUFULI KATIKA KUDHIBITI WIZI WA RASILIMALI ZA NCHI

Na Mwandishi wetu,     
Songea.

JITIHADA zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli katika kudhibiti vitendo vya wizi wa rasilimali za nchi yakiwemo madini, zimepongezwa na baadhi ya Wananchi wa Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma akiwemo Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa kata ya Mateka katika Manispaa hiyo, Kazira Hussein.

Rais Dkt. John Magufuli.
Wananchi hao kwa nyakati tofauti walisema kuwa kitendo cha Rais Dkt. Magufuli kubaini mbinu chafu zilizokuwa zinafanywa na viongozi ambao siyo waaminifu, ambao walikuwa wakiidanganya serikali kwamba wanasafirisha mchanga usiokuwa na madini na kuupeleka nje ya nchi, wakati mchanga huo ulikuwa na madini ni jambo ambalo linasikitisha na kudhihirisha kuwa kwa muda mrefu Watanzania walikuwa wanaibiwa.

Joseph Milanzi mkazi wa Lizaboni alieleza kuwa kazi inayoendelea kufanywa na Rais huyo katika kuwabaini wahalifu hao, inapaswa kuungwa mkono kwa nguvu zote ili kuweza kulifanya taifa liweze kukua kiuchumi kupitia rasilimali zake na sio muda mwingi kutegemea misaada kutoka nje ya nchi.

Sunday, June 18, 2017

WATOTO WALIONUSURIKA AJALI YA LUCKY VINCENT KUREJEA HAPA NCHINI BAADA YA MIEZI MIWILI

WATOTO watatu ambao walinusurika katika ajali iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na Dereva wa shule ya Lucky Vincent mjini Arusha, huenda wakaruhusiwa kurejea hapa nchini baada ya miezi miwili.

Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu ametoa taarifa hiyo katika ukurasa wake kwenye mtandao wa kijamii yaani Facebook.

WAZIRI MKUU AONGOZA HARAMBEE UJENZI WA KANISA KATOLIKI ZUZU DODOMA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa upande wa kushoto akiwa ameongozana na Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda na mkewe Tunu Pinda walipokuwa wakimpokea katika makazi yao yaliyopo Zuzu nje kidogo mjini Dodoma June 17 mwaka huu wakati wa kuhudhuria Misa ya kumbukumbu ya marehemu mzee Exavery Pinda, Baba mzazi wa Mizengo Pinda, pamoja na kuongoza uchangiaji wa ujenzi wa nyumba ya Paroko na ukarabati wa Kanisa la Parokia ya Zuzu.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwa niaba ya familia yake akimkabidhi mchango wa shilingi milioni kumi, Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa nyumba ya Paroko pamoja na kufanyia ukarabati wa Kanisa Parokia ya Zuzu Dodoma. Upande wa kushoto ni msaidizi wa Askofu Jimbo la Dodoma Baba Chesco Msaga. Harambee hiyo ilifanyika June 17 mwaka huu katika makazi ya Waziri Mkuu mstaafu Pinda, yaliyopo Zuzu nje kidogo mjini Dodoma.
Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda akiwaonyesha Wageni waalikwa ambao hawapo pichani shilingi milioni 10 ambao ni mchango aliokabidhiwa na Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa kwa niaba ya familia yake kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa nyumba ya Paroko pamoja na kufanyia ukarabati wa Kanisa Parokia ya Zinje (Zuzu) Dodoma. Kushoto ni msaidizi wa Askofu Jimbo la Dodoma Baba Chesco Msaga. (Picha zote na Ofisi ya Waziri Mkuu)

DIWANI KATA YA KITANDA AOMBA RADHI NA KUKIRI KUFANYA UBADHIRIFU MALI ZA WANANCHI MBELE YA VIONGOZI WA CCM


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mbinga, Christantus Mbunda.
Na Kassian Nyandindi,    
Mbinga.

HATIMAYE Diwani wa kata ya Kitanda, Zeno Mbunda Halmashauri ya mji wa Mbinga mkoani Ruvuma amejikuta akiendelea kuwa katika wakati mgumu baada ya kusimama mbele ya kikao maalumu na kuwaomba radhi baadhi ya Wananchi na Wajumbe wa Baraza la maendeleo la kata hiyo, huku akikiri kwamba tuhuma anazotuhumiwa kufanya ubadhirifu wa mali na fedha za wananchi hao kuwa ni za kweli.

Zeno Mbunda, Diwani kata ya Kitanda.
Pamoja na diwani huyo kukubali makosa hayo mbele ya kikao hicho kilichofanyika Juni 17 mwaka huu kwenye Ofisi za makao makuu ya kata ya Kitanda, aidha alieleza kuwa ifikapo Julai Mosi mwaka huu atakuwa amelipa mali na fedha zote ambazo anadaiwa kutofikisha katani humo.

Radhi hiyo ambayo alikuwa akiiomba mbele ya ushuhuda wa viongozi wa CCM wilaya ya Mbinga, akiwemo na Mwenyekiti wa Chama hicho Christantus Mbunda ambaye alikuwa akiongoza kikao hicho.

Licha ya kuwaomba radhi bado Wajumbe wa baraza hilo la maendeleo la kata walionekana kutoridhishwa na hali hiyo huku wengine wakisema kuwa hawawezi kuchukua hatua ya kumsamehe, kwani ni mapema mno mpaka pale atakaporejesha mali na fedha za wakulima wa kahawa anazotuhumiwa kuzitafuna kwa manufaa yake binafsi.

“Hatuwezi kuchukua hatua ya kumsamehe mpaka pia tupate majibu ya hatua zilizochukuliwa kutoka Ofisi ya Mkuu wa wilaya, ambako malalamiko haya tuliyapeleka kwa njia ya maandishi na bado hatujajibiwa mpaka sasa”, alisema Mwenyekiti wa kata ya Kitanda Philibert Mkolwe.

Saturday, June 17, 2017

MLEMAVU WA MIGUU APEWA MSAADA WA BAISKELI NA MBUNGE WA JIMBO LA MBINGA MJINI

Baadhi ya wananchi wa kata ya Mbinga mjini jana wakishuhudia tukio la kukabidhi baiskeli maalumu (Wheel chair) kwa mtoto mwenye ulemavu wa miguu, Batazari Ndunguru ambayo imetolewa na Mbunge wa Jimbo la Mbinga mjini Sixtus Mapunda.
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Mbinga mjini, Geddy Ndimbo naye akijaribu kumwendesha mtoto mlemavu Batazari Ndunguru ambaye ameketi kwenye baiskeli maalumu (Wheel chair) ambayo amepewa msaada na Mbunge wa jimbo hilo.
Mwenyekiti wa kata ya Mbinga mjini, Kalistus Mwamanga akimwendesha mlemavu Batazari Ndunguru ambaye amekaa kwenye baiskeli maalumu (Wheel chair) ambayo amepewa msaada na Mbunge wa Jimbo la Mbinga mjini, Sixtus Mapunda. (Picha zote na Gwiji la Matukio Ruvuma)
Na Kassian Nyandindi,        
Mbinga.

BATAZARI Ndunguru (17) ambaye ni mlemavu wa miguu mkazi wa kata ya Mbinga mjini A Halmashauri ya mji wa Mbinga mkoani Ruvuma, amepewa msaada wa baiskeli maalumu ya kutembelea (Wheel chair) kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Mbinga mjini, Sixtus Mapunda.

Akikabidhi msaada huo mbele ya uongozi wa kata hiyo kwa niaba ya Mbunge huyo, Geddy Ndimbo ambaye ni Katibu wa Mbunge Mapunda alisema kuwa baiskeli hiyo ya kutembelea mtoto huyo imepatikana kwa thamani ya shilingi 500,000 kutokana na jitihada zilizofanywa na Mbunge wa jimbo hilo.

Ndimbo alisema kuwa jitihada hizo zimefanywa kwa lengo la kumsaidia mtoto huyo ili aweze kuondokana na taabu alizokuwa akizipata kwa siku nyingi, ikiwemo kutambaa kwa mikono na magoti, hivyo aliona kuna kila sababu ya kumtafutia chombo hicho ili kuweza kumrahisishia kutembea vizuri na asiweze kuendelea kupata mateso kama hayo.

“Baiskeli hii nakukabidhi ili iweze kukusaidia na kukurahisishia kutembea vizuri, nawaomba ndugu mnaomtunza endeleeni kuitunza na kumtunza vizuri mtoto huyu kama walivyo wenzake ambao hawana matatizo ya ulemavu, baiskeli itunzwe vizuri itumike kwa matumizi yaliyokusudiwa itakuwa ni ajabu kuona anaitumia mtoto mwingine ambaye hana matatizo ya ulemavu”, alisema Ndimbo.

RUHUWIKO SONGEA WAONDOKANA NA KERO YA MAJI SAFI NA SALAMA

Na Muhidin Amri,    
Songea.

WAKAZI wanaoishi katika mtaa wa Ruhuwiko Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, wameondokana na kero ya muda mrefu ya upatikanaji wa maji safi na salama baada ya kukamilika kwa mradi mkubwa wa ujenzi wa tanki la maji katika mtaa huo ambalo sasa husambaza maji hayo katika maeneo mbalimbali wanayoishi.

Abdul Mshaweji.
Aidha katika hatua nyingine wametakiwa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali hii ya awamu ya tano katika kumaliza kero wanazokabilianazo wananchi wake.

Sambamba na hilo wamekumbushwa pia wajibu wao wa kuisaidia serikali juu ya mkakati wa kuinua uchumi wao kwa kubuni miradi ya maendeleo ambayo itawaingizia kipato kuanzia ngazi ya familia.

Meya wa Manispaa ya Songea, Abdul Mshaweji alitoa kauli hiyo jana wakati alipokuwa akizungumza na wakazi wa mtaa huo, katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na wananchi hao wakilenga kuishukuru serikali kwa kukamilisha ujenzi wa mradi huo wa maji katika mtaa huo wa Ruhuwiko.

KAYA MASKINI SONGEA KUPOKEA RUZUKU KWA MFUMO WA KIELEKTRONIKI

Na Julius Konala,    
Songea.

KAYA maskini 615 ambazo zimeibuliwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) awamu ya tatu katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, wanatarajia kunufaika na utaratibu mpya uliowekwa na Serikali namna ya kupokea ruzuku zao kwa njia ya mfumo wa Kielektroniki, mapema mwezi Julai mwaka huu.

Aniceth Kyaruzi ambaye ni Afisa ufuatiliaji wa mfuko huo katika Manispaa hiyo, alisema kuwa utaratibu huo mpya utaanza kwa majaribio kwa kaya ambazo zitakuwa tayari kujiunga na mfumo huo.

Kyaruzi alisema kuwa Manispaa ya Songea ina jumla ya walengwa 4,968 ambapo kati ya hao waliojitokeza mpaka sasa kujiunga na utaratibu huo wa malipo kwa njia ya Kielektroniki ni 615 wanatoka katika mitaa 53 iliyopo mjini hapa ambayo utekelezaji wa mpango wa kunusuru kaya maskini umekuwa ukifanyika.

Friday, June 16, 2017

MATUKIO KATIKA PICHA: MIUNDOMBINU CHAKAVU YA MAJENGO SHULE YA MSINGI MALOMBE TUNDURU MKOANI RUVUMA

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, Brawn Mwangomale (Katikati) aliyenyoosha mkono akipokea maelekezo kutoka kwa walimu wa shule ya msingi Malombe iliyopo katika kata ya Mlingoti wilayani humo, wakati alipotembelea katika shule hiyo kwa lengo la kujionea miundombinu ya madarasa ya shule hiyo.
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chama hicho katika ngazi ya kijiji na kata hiyo, wakati walipotembelea miongoni mwa nyumba ambazo wanaishi walimu hao wanaofundisha katika shule ya msingi Malombe wilayani Tunduru.
Baadhi ya walimu wa shule ya msingi Malombe wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma wakiwa katika picha ya pamoja mbele ya nyumba anayoishi mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Malombe. (Picha zote na Steven Augustino)

MADABA WATAKIWA KUONGEZA UZALISHAJI WA MAZAO SHAMBANI

Na Muhidin Amri,    
Madaba.

WAKULIMA katika Halmashauri ya wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma wametakiwa kuchangamkia fursa na mkakati uliowekwa na serikali ambao unataka nchi kufikia katika uchumi wa kati, kupitia ujenzi wa viwanda vya aina mbalimbali ifikapo mwaka 2020 hadi 2025.
Shafi Mpenda.

Vilevile katika kufanikisha hilo imeelezwa kuwa wanapaswa kuongeza uzalishaji wa mazao mashambani ili viwanda hivyo vitakapoanzishwa, viweze kusonga mbele na kusaidia kuongeza thamani ya ubora wa mazao hayo.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, Shafi Mpenda alisema hayo juzi wakati alipokuwa akikagua mradi wa shamba la mahindi la vijana, ambao hujishughulisha pia na uendeshaji wa Pikipiki maarufu kwa jina la Boda boda katika kijiji cha Lutukira wilayani humo ili waweze kujipatia kipato.

WANAWAKE KIGONSERA WANUFAIKA NA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI

Na Muhidin Amri,      
Mbinga.

WANAWAKE zaidi ya 150 kutoka katika vijiji vitatu kata ya Kigonsera Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, wamepata mafunzo ya ujasirimali na kufanikiwa kujiunga kwenye vikundi vinavyowawezesha kujijenga kiuchumi kwa lengo la kuboresha maisha yao.

Akizungumza  jana wakati wa kufunga mafunzo hayo Diwani wa viti maalum  wa tarafa  ya Kigonsera wilayani humo, Amina Kapinga  alieleza kuwa mbali na wanawake hao kunufaika na elimu hiyo ya ujasirimali pia baadhi yao wameanza kupewa mikopo ya fedha na pembejeo za kilimo kupitia vikundi hivyo.

Kapinga alifafanua kuwa mikopo na fedha hizo wamepata kutoka kwenye taasisi mbalimbali na vyama vya akiba na mikopo (SACCOS).

Alisema kuwa katika kata hiyo tayari vikundi vitatu vya Mwongozi na Kitumbalomo ambavyo hujishughulisha na shughuli za kilimo na vingine vinavyotengeneza sabuni na nguo aina ya batiki vimeweza kunufaika na mikopo hiyo.

WAZIRI TAMISEMI AWAONYA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA

WAZIRI wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene amewaonya Wakuu wa mikoa na wilaya, ambao wanatumia vibaya madaraka yao ya kukamata watu walio kwenye himaya zao.

Alitoa onyo hilo leo wakati alipojibu maswali ya wabunge waliotaka kufanyika marekebisho ya sheria inayowapa mamlaka wakuu hao ya kuwakamata na kuwaweka ndani wananchi wanaowatuhumu kwa lolote.

Licha ya kubainisha kwamba sheria hiyo haina tatizo, Waziri huyo amesisitiza kwamba, ukamataji unatakiwa ufanywe kwa mtu aliyetenda kosa la jinai au anayehatarisha usalama, “isiwe kwa show-off tu”, alisema.

Thursday, June 15, 2017

BREAKING NEWS: AFISA MAENDELEO YA JAMII WILAYA SONGEA AFUKUZWA KAZI KWA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA ZA SERIKALI

Na Mwandishi wetu,       
Songea.

BARAZA la Madiwani Halmashauri ya wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, limemfukuza kazi Afisa maendeleo ya jamii wa wilaya hiyo, Wenisalia Swai kutokana na kubadili matumizi ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya halmashauri hiyo bila kufuata taratibu husika.

Aidha Swai anadaiwa kutenda kosa la kubadili fedha shilingi milioni 130 zilizotolewa na ubalozi wa Japan hapa nchini, kwa ajili ya kuboresha kituo cha afya Mhukuru kilichopo wilayani humo kwa kumlipa mkandarasi aliyejenga jengo la halmashauri katika kijiji cha Lundusi kata ya Maposeni, wakati fedha kwa ajili ya ujenzi huo zilikwishatolewa na serikali.

Pia mtumishi huyo imeelezwa kuwa alibadili matumizi ya fedha nyingine zaidi ya shilingi milioni 156 zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa Skimu ya umwagiliaji katika kijiji cha Nakahuga na kuzielekeza kwenye utengenezaji wa madawati na ujenzi wa jengo la maabara, jambo ambalo limesababisha wakulima wa kijiji hicho kushindwa kuendesha na kunufaika na mradi huo wa umwagiliaji.

Wednesday, June 14, 2017

RAIS DOKTA MAGUFULI AMTEUA MWENYEKITI WA BODI KITUO CHA UWEKEZAJI TANZANIA


RAIS DOKTA MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWENYEKITI MTENDAJI WA KAMPUNI YA BARRICK GOLD CORPORATION

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mazungumzo yake na Mwenyekiti wa Barrick Gold Corporation ya Canada aliyekuwa upande wa kushoto, leo Ikulu Jijini Dar es salaam. Kutoka kulia ni Balozi wa Canada hapa nchini Ian Myles na Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi.
Mwenyekiti wa Barrick Gold Corporation ya Canada Profesa John Thornton akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mazungumzo na Rais Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu Jijini Dar es salaam. Upande wa kushoto ni Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi.

HALMASHAURI YA NYASA IMEANZA UJENZI WA BARABARA ZAKE KWA KIWANGO CHA CHANGARAWE

Ziwa Nyasa.
Na Muhidin Amri,     
Nyasa.

HALMASHAURI wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, imeanza kazi ya ujenzi wa barabara zake za mitaa kwa kiwango cha changarawe ikiwa ni mpango wa kuboresha barabara hizo, ili ziweze kuwa katika hali nzuri na kurahisisha kukua kwa maendeleo katika wilaya hiyo hususan usafirishaji mazao kutoka shambani hadi sokoni.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Dkt. Oscar Mbyuzi alisema hayo juzi wakati wa zoezi la ufunguzi rasmi ujenzi wa barabara hizo zenye urefu wa kilometa nane katika kijiji cha Kilosa wilayani hapa.

Dkt. Mbyuzi alisema kuwa mradi huo ulianza tangu mwezi Februari mwaka huu na kwamba utakuwa endelevu kila halmashauri yake itakapokuwa na fedha za kutosha kutoka kwenye vyanzo vyake vya ndani.

Tuesday, June 13, 2017

RAIS DOKTA MAGUFULI AKUTANA NA WAKUU WA MIKOA WOTE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikutana na Wakuu wa mikoa wote katika kikao kilichohudhuriwa pia na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi na baadhi ya mawaziri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju leo Ikulu Jijini Dar es salaam.