Thursday, April 30, 2015

MBIO ZA MWENGE RUVUMA KUZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 10.3

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dokta Alli Mohamed Shein akikabidhi Mwenge wa uhuru kwa mmoja wa wakimbiza Mwenge kitaifa, jana mara baada ya kuzindua mbio hizo katika uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma.


Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu akikabidhi Mwenge wa uhuru kwa Mkuu wa wilaya ya Songea mkoani humo, Profesa Norman Sigalla kwa ajili ya kuanza mbio zake katika wilaya ya Songea.
Na Kassian Nyandindi,
Ruvuma.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dokta Alli Mohamed Shein amekemea kitendo kinachofanywa na baadhi ya watu kuwagawa Watanzania, jambo ambalo linahatarisha amani ya nchi yetu.

Dokta Shein alisema kumekuwa na makundi ambayo huwagawa kwa misingi ya dini, rangi na ukabila jambo ambalo amekemea vikali na kutaka hali hiyo iachwe mara moja.

Vilevile alikemea vitendo vya biashara ya madawa ya kulevya, ambapo alieleza kuwa kundi la vijana ndilo kwa kiasi kikubwa linahusika na vitendo hivyo na kuwataka waachane na tabia hiyo badala yake wafanye shughuli za kimaendeleo, kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Rais huyo alifafanua kuwa ni aibu kwa taifa hili vijana kujihusisha na biashara hiyo, kwani wao ndio nguvu kazi katika kusukuma gurudumu la maendeleo hivyo serikali itaendelea kupambana na vitendo hivyo vya uuzaji wa madawa hayo, ili visiweze kuendelea.

OFISA USALAMA WA TAIFA ALETA KIZAZAA KWENYE UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU KITAIFA RUVUMA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo Dokta Fenera Mukangara kushoto akimuongoza Rais wa Zanzibar Dokta  Alli Mohamed Shein, kwenda kuzindua mbio za Mwenge wa uhuru jana, katika uwanja wa michezo wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma. (Picha na Muhidin Amri)
Na Mwandishi wetu,
Songea.

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, Waandishi wa habari mkoani Ruvuma jana wamejikuta wakifanya kazi katika mazingira mgumu, baada ya mmoja wa Ofisa kutoka idara ya usalama wa taifa hapa nchini, kuwazuia waandishi hao wasitekeleze majukumu yao ya kazi ipasavyo.  

Ofisa usalama huyo aliwazuia wasiweze kupiga picha, na kuandika taarifa za uzinduzi wa Mwenge wa Uhuru kitaifa, zilizofanyika jana kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma.

Aidha aliwashangaza waandishi hao pale alipofikia hatua ya kutamka kwamba wasitekeleze majukumu yao ya kazi, mpaka mgeni rasmi Dokta Alli Mohamed Shein atakapokwenda kuketi jukwaani jambo ambalo wanahabari hao walimpuuza na kutumia mbinu mbadala katika kuandika habari, na kupiga picha za tukio hilo.

MWAMBUNGU ATAKA WANANCHI WA KITONGOJI CHA MANGAWAGA NYASA WASIHAMISHWE

Na Kassian Nyandindi,
Nyasa.

MKUU wa mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu ametoa agizo la kuutaka uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Nyasa mkoani humo, kusitisha mara moja mchakato wa kuwahamisha wakazi wa kitongoji cha Mangawaga kijiji cha Mkalole kata ya Kilosa wilayani humo, mpaka serikali itakapotoa maelekezo mengine.

Agizo hilo la Mkuu huyo wa mkoa, liliwasilishwa na Kamanda wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilayani humo, Cassian Njowoka alipokuwa akizungumza na wananchi wa kitongoji hicho, katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini humo.

“Ndugu zangu nimeagizwa na mkuu wa mkoa wa Ruvuma, ni marufuku kuhama endeleeni kuishi hapa kijijini mpaka serikali itakapotoa maelekezo mengine, hivyo ondoeni wasiwasi katika jambo hili ninalowaambia”, alisema Njowoka.

DEREVA WA PIKIPIKI MBINGA APANDISHWA KIZIMBANI KWA KULAWITI

Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

LAURENT Kibasa (30) ambaye ni dereva wa pikipiki, mkazi wa mtaa wa Kiwandani Mbinga mjini mkoani Ruvuma, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya wilaya hiyo, kwa tuhuma ya kumlawiti mwanaume mwenzake (Jina tunalo) mwenye umri wa miaka 24 na kumdhuru mwili.

Mwendesha mashtaka msaidizi wa polisi, Inspekta Seif Kilugwe alidai mbele ya Hakimu Joachimu Mwakyolo wa Mahakama ya wilaya ya Mbinga, kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Aprili 23 mwaka huu majira ya mchana akiwa nyumbani kwake baada kushindwa kulipwa deni analodai shilingi 85,000.

Kibasa anadaiwa kufanya makosa hayo kwa dereva wa pikipiki mwenzake maarufu kwa jina la Boda boda, baada ya kumfuata kwenye eneo lake la kazi kisha kumkamata na kumpeleka nyumbani kwake ambako anadaiwa alimfunga kamba mikononi na kuanza kumpiga, kwa kutumia mkanda wake wa suruali.

Tuesday, April 21, 2015

SERIKALI YATAKIWA KUTOA KIBALI KWA TAASISI BINAFSI KUSAMBAZA RASIMU YA PILI YA KATIBA

Na Kassian Nyandindi,
Ruvuma.

SERIKALI hapa nchini, imetakiwa kutoa kibali kwa taasisi binafsi ziweze kushiriki kikamilifu kuchapisha nakala za rasimu ya pili ya katiba inayopendekezwa, ili zisambazwe kwa wingi na kumfikia kila mwananchi kwa wakati, hatimaye waweze kuisoma na kuielewa na baadaye waipigie kura ya maoni wakiwa na taarifa sahihi.

Hayo yalisemwa na mtafiti wa maswala ya katiba hapa nchini, Gelin Fuko kutoka kituo cha sheria na haki za binadamu wakati alipokuwa kwenye mkutano wa hadhara Mbinga mjini mkoani Ruvuma, uliofanyika kwenye viwanja vya soko kuu mjini humo.

Aidha Fuko aliwataka wananchi wakati utakapofika katika maeneo yao, wajiandikishe kwenye daftari la wapiga kura jambo ambalo litawafanya waweze kuingia kwenye mchakato huo, wa kuipigia kura rasimu hiyo.

Saturday, April 18, 2015

WAFARIKI DUNIA NA WENGINE 20 KUJERUHIWA VIBAYA KATIKA AJALI YA GARI WAKIELEKEA MNADANI

Na Kassian Nyandindi,
Songea.

WATU wawili wamefariki dunia na wengine 20 kujeruhiwa vibaya, kufuatia ajali ya gari aina ya Mitsubishi Fuso kupinduka katika kijiji cha Burma wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, baada ya dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo kumshinda kona za milima ya Ambrose zilizopo katika kijiji hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi wa mkoa huo Mihayo Msikhela alisema kuwa ajali hiyo, imetokea leo majira ya saa 3:30 asubuhi katika kijiji hicho wilayani humo.

Msikhela alifafanua kuwa gari hilo lilikuwa likitokea Songea kwenda Mbamba bay, wilaya ya Nyasa huku likiwa limebeba watu hao, pamoja na mizigo kwa ajili ya kwenda kufanya shughuli za mnada.

Friday, April 17, 2015

KAMANDA UVCCM AISAMBARATISHA CHADEMA NYASA

Na Kassian Nyandindi,
Mbamba bay.

BAADHI ya wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wilayani Nyasa mkoa wa Ruvuma, wamekiasi chama hicho na kuhamia Chama Cha Cha Mapinduzi (CCM) kwa kile walichoeleza kuwa, wamechoshwa na sera za Chadema ambazo zimekuwa zikichochea machafuko mara kwa mara hapa nchini.

Wafuasi hao ambao walikuwa 67 walieleza kuwa, hawana sababu ya kuendelea kuwa katika chama hicho cha upinzani badala yake waliona ni heri warejee kwenye chama mama, CCM ambako walikuwa tokea awali.

Hali hiyo ilitokea leo katika viwanja vya mji mdogo wa Mbamba bay wilayani humo, kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Kamanda wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Nyasa, Cassian Njowoka.

Thursday, April 16, 2015

AWEZAE AFARIKI DUNIA KWA KUGONGWA NA LORI TUNDURU

Na Mwandishi wetu,
Tunduru.

AWEZAE Mohamed (35) amefariki dunia kufuatia ajali mbaya iliyotokana na pikipiki ambayo alikuwa akisafiria, kugongwa na lori aina ya Steya lenye namba za usajili T 862BFW ambalo linatumiwa kubeba kifusi cha udongo.

Kadhalika mume wake Issa Swalehe naye amelazwa katika Hospitali ya wilaya ya Tunduru kufuatia ajali hiyo, ambaye ni mlinzi katika kampuni ya kichina ambayo inajenga barabara kutoka Tunduru mjini hadi kata ya Matemanga wilayani humo.

Tukio hilo lilitokea Aprili 3 mwaka huu, kijiji cha Amani katika kata ya Nandembo wilayani humo ambapo marehemu huyo alikuwa akisafiria pikipiki aina ya Sunlg yenye namba za usajili T 886 CTC ambayo ilikuwa ikiendeshwa na mumewe huyo.

WAKULIMA TUNDURU WALALAMIKIA WATENDAJI WA VIJIJI

Na Steven Augustino,
Tunduru.

WAKULIMA katika kata ya Muhuwesi, wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma wamewataka watendaji katika vijiji vya wilaya hiyo, kujenga ushirikiano wa karibu ili kuweza kusukuma mbele maendeleo yao. 

Rai hiyo ilitolewa na wakulima wa Chama cha ushirika cha Mumsasichema AMCOS, walipokuwa kwenye kikao chao cha wadau wa zao la korosho kilichofanyika katika ofisi za chama hicho kijiji cha Muhuwesi wilayani humo.

Mwenyekiti wa chama hicho, Issa Kambutu alifafanua kuwa kutokana na kuwepo kwa mmomonyoko mkubwa wa maadili ikiwemo kukithiri kwa vitendo vya wizi wa fedha za wakulima wa zao hilo, ukifanywa na baadhi ya viongozi hao sasa kuna kila sababu kujenga ushirikiano ili kuweza kudhibiti hali hiyo.

MUNDAU: FRELIMO ITAENDELEA KUDUMISHA USHIRIKIANO WETU

Na Kassian Nyandindi,
Nyasa.

IMEELEZWA kuwa ushirikiano uliopo kati ya wananchi wa vijiji vya Lunyere kilichopo wilayani Nyasa nchini Tanzania na Mpapa wilaya ya Lagunyasa jimbo la Lichinga Msumbiji, umetakiwa kudumishwa ili amani na utulivu uliopo mpakani kati ya nchi hizo mbili uweze kuendelea.

Hayo yalisemwa na Kamanda wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilayani humo, Cassian Njowoka alipokuwa akizungumza na wananchi mara baada ya kumwapisha kamanda wa jumuiya hiyo kata ya Mpepo Bosco Kihwili, sherehe ambayo ilifanyika katika kijiji cha Lunyere.

Njowoka alisema wananchi wa Lunyere, hususani vijana wamekuwa wakijihusisha na shughuli za uchimbaji madini ambapo kutokana na uhusiano  mzuri uliopo kwa muda mrefu baina ya nchi hizo mbili, wengi wao wamekuwa wakivuka mpaka na kwenda Msumbiji ambako pia hufanya shughuli za uchimbaji bila kikwazo hivyo ni vyema wakazingatia sheria zilizopo ambazo zinapaswa kufuatwa pindi wanapotaka kuingia nchi hiyo jirani.

Wednesday, April 15, 2015

KAMANDA WA VIJANA UVCCM NYASA ATOA MSAADA WA VITANDA KIJIJI CHA LUNYERE

Na Kassian Nyandindi,
Nyasa.

KITENDO cha akina mama wajawazito kulala na kujifungulia chini ya sakafu katika Zahanati ya kijiji cha Lunyere, kata ya Mpepo wilayani Nyasa mkoa wa Ruvuma, kimemshangaza Kamanda wa Jumuiya Umoja wa Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wa wilaya hiyo, Cassian Njowoka na kuwataka wadau mbalimbali kujitokeza kuchangia vifaa mbalimbali vinavyokosekana, hali ambayo itasaidia akina mama hao na wananchi kwa ujumla wapate huduma za afya katika mazingira salama.

Kushangazwa huko kulitokea baada ya kutembelea katika eneo hilo na kutoa msaada wa vitanda 20, magodoro 20, mito ya kulalia, mashuka na vyandarua vifaa ambavyo tokea ijengwe haikuwa navyo jambo ambalo lilisababisha wagonjwa wengi kupata huduma duni wanapokwenda kupata matibabu.

Akizungumza na wananchi wa kijiji hicho wakati akikabidhi vifaa hivyo, Njowoka alisema ameguswa na kero hiyo inayowakumba wananchi hao ambapo analazimika kuendelea kutoa mingine ikiwemo mabomba ya maji, umeme wa nguvu ya jua na kukamilisha ukarabati wa chumba cha kujifungulia akina mama hao wajawazito.

WANAFUNZI WASOMEA CHINI YA MTI VIONGOZI NYASA WALAUMIWA

Watoto wakisoma chini ya mti.
Na Kassian Nyandindi,
Nyasa.

KAMANDA wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Nyasa mkoa wa Ruvuma, Cassian Njowoka amesikitishwa na kitendo cha viongozi wa ngazi ya juu wilayani humo kushindwa kutatua tatizo la ujenzi wa shule ya msingi Linda, ambayo imeezuliwa na upepo kitendo ambacho kinasababisha wanafunzi kukosa masomo darasani.

Wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo hivi sasa wanalazimika kusomea chini ya miti ya mikorosho, hali ambayo imekuwa ikiwapa kero kubwa kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nyakati hizi za masika.

Masikitiko hayo aliyatoa wakati alipokuwa kwenye ziara yake ya kuwasimika makamanda wa kata wilayani humo, ambapo alipofika katika kata ya Kilosa alielezwa tatizo la shule hiyo kuezuliwa na upepo Julai 11 mwaka jana.

Monday, April 13, 2015

WANAFUNZI NYASA HATARINI KUANGUKIWA NA JENGO

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu.
Na Kassian Nyandindi,
Nyasa.

WATOTO wanaosoma katika shule ya msingi Nangombo wilayani Nyasa mkoa wa Ruvuma, wapo hatarini kuangukiwa na majengo ya shule hiyo kutokana na kuwa chakavu na kutofanyiwa ukarabati kwa zaidi ya miaka 80.

Akizungumza na wazazi wa shule hiyo, Kamanda wa umoja wa vijana (UVCCM) wa wilaya hiyo, Cassian Njowoka alielezwa na mkuu wa shule hiyo, Hyasint Hyera kuwa majengo hayo ni machakavu na yapo hatarini kuanguka kufuatia kuwepo kwa nyufa sehemu mbalimbali.

Hyera alisema kuwa shule ilianzishwa mwaka 1932 na kwamba inawanafunzi 290 kuanzia darasa la kwanza hadi la saba, lakini pamoja na kutolewa taarifa mara kwa mara kwa viongozi wa serikali hakuna hatua zilizochukuliwa jambo ambalo ni hatari kwa watoto hao.

Alifafanua kuwa changamoto mojawapo inayowakabili shuleni hapo, ni kukosekana kwa vitendea kazi ikiwemo chaki za kuandikia pale mwalimu anapokuwa darasani akifundisha wanafunzi, hali ambayo ilisababisha watoto hao kukaa katika kipindi cha wiki tatu bila kufundishwa.

NYASA KUMUENZI KAPTENI KOMBA

Na Kassian Nyandindi,
Nyasa.

JUMUIYA ya umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Nyasa mkoa wa Ruvuma, umeazimia kumuenzi aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi, Marehemu Kapteni John Komba kila mwaka ifikiapo Februari 28 wataandaa matamasha mbalimbali ikiwemo kuchangia maendeleo ya wilaya hiyo.

Aidha siku hiyo itakuwa maalumu kwa ajili ya kuwakusanya, wananyasa waishio nje ya Nyasa, kurejea kwao na kusaidia kuchangia ukuaji wa uchumi wa wilaya hiyo na maendeleo ya wananchi kwa ujumla ili waweze kuondokana na umasikini.

Kwa kutambua umuhimu na mchango mkubwa wa maendeleo uliofanywa na aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Kamanda wa jumuiya hiyo ya umoja wa vijana wilayani Nyasa, Cassian Njowoka alisema hayo alipokuwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo wakati alipokuwa akizungumza kwenye baraza la vijana kata ya Kilosa.

Thursday, April 9, 2015

KAYOMBO AIOMBA NMB KUONGEZA MASHINE ZA KUTOLEA FEDHA ILI KUPUNGUZA MSONGAMANO WA WATU

Mbunge wa jimbo la Mbinga Mashariki, Gaudence Kayombo akizungumza katika semina ya siku moja ya Wadau wa kahawa ukumbi wa Jimbo katoliki Mbinga mjini, ambayo inaendeshwa na benki ya NMB, ambapo aliiomba benki hiyo katika kuboresha huduma zake iongeze kwa kujenga mashine za kutolea fedha (ATM) katika maeneo mbalimbali mjini humo, ili kupunguza msongamano wa watu katika benki hiyo. Katikati ni Mkuu wa wilaya ya Mbinga, Senyi Ngaga na kushoto ni Meneja wa Kanda ya kusini wa NMB, Lillian Mwinula.

WAKULIMA MBINGA WATAKIWA KUONGEZA UZALISHAJI KATIKA ZAO LA KAHAWA

Mkuu wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Senyi Ngaga akifungua semina ya siku moja kwa Wadau wa kahawa wilayani humo kwenye ukumbi wa Jimbo katoliki uliopo mjini hapa, kushoto ni Meneja wa NMB Kanda ya kusini Lillian Mwinula na upande wa kulia ni Mbunge wa jimbo la Mbinga Mashariki, Gaudence Kayombo.

Baadhi ya Wadau wa kahawa wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, wakifuatilia mada kwa umakini katika semina ya wadau wa kahawa wa wilaya hiyo, iliyofanyika leo ukumbi wa Jimbo katoliki mjini hapa. 
Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

WAKULIMA wa kahawa wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, wametakiwa kuongeza uzalishaji katika zao hilo, ili waweze kujiongezea kipato na hatimaye waweze kuondokana na umasikini.

Aidha wameaswa kuzingatia kununi bora za kilimo kwa kushirikiana na wataalamu wa zao hilo, ili wafikie lengo la uzalishaji wa kahawa bora na yenye kupata soko na bei nzuri mnadani.

Mkuu wa wilaya ya Mbinga, Senyi Ngaga alitoa rai hiyo leo katika semina ya siku moja ya Wadau wa kahawa wa wilaya hiyo, iliyofanyika kwenye ukumbi wa Jimbo katoliki mjini hapa ambayo ilikuwa ikiendeshwa na benki ya NMB tawi la Mbinga.

Ngaga alisema kuwa wakulima wa zao hilo, wanakila sababu ya kuelimishwa juu ya kilimo bora cha kahawa ili waweze kuzalisha zaidi, na kuifanya wilaya hiyo na taifa kwa ujumla liweze kusonga mbele kimaendeleo.

BENKI YA NMB YATOA MAFUNZO KWA WADAU WA KAHAWA MBINGA

Upande wa kushoto, Mkuu wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Senyi Ngaga akikaribishwa leo katika ukumbi wa Jimbo Katoliki uliopo mjini hapa na Meneja wa benki ya NMB tawi la Mbinga Lugano Mwampeta, kwa ajili ya kufanya ufunguzi wa semina ya siku moja kwa wadau wa kahawa wa wilaya hiyo. Anayeshuhudia tukio hilo ni Meneja wa benki hiyo tawi la Litembo wilayani Mbinga, Victor Msoffe.

Meneja wa NMB Kanda ya kusini Lillian Mwinula, akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mashariki mkoani Ruvuma, Gaudence Kayombo ambaye alikuja kushiriki katika semina ya Wadau wa kahawa inayofanyika leo kwenye ukumbi wa Jimbo Katoliki mjini hapa. Kwa ujumla semina hiyo inaendeshwa na benki hiyo kwa manufaa ya kumuinua mkulima kiuchumi ili aweze kuondokana na umasikini. 

Wednesday, April 8, 2015

KUMBURU AZITAKA HALMASHAURI KUTUNGA SHERIA NDOGO ZA UENDESHAJI CPU

 
Adolph Kumburu, Mkurugenzi wa Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB) akisisitiza jambo katika moja ya vikao vyake na Wadau wa zao hilo, hapa nchini.
Na Kassian Nyandindi,

Mbinga.

MKURUGENZI wa Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB) Adolph Kumburu, amesema kuwa msimu wa mavuno ya zao hilo hapa nchini umefunguliwa mapema mwezi Aprili mwaka huu, kutokana na baadhi ya maeneo ambayo yanawahi kuiva zao hilo wakulima waweze kuuza kahawa yao mapema bila kuchelewa.

Aidha msimu huu wa mwaka 2015/2016 bodi imefanya makadirio ya kukusanya tani 60,000 tofauti na msimu wa mwaka 2014/2015 ilikadiria kukusanya tani 44,000 lakini haikufikia lengo hilo, badala yake ilikusanya tani 43,000 tu jambo ambalo alifafanua kuwa lilitokana na baadhi ya maeneo hapa nchini zao hilo kushambuliwa na wadudu waharibifu, na kusababisha kushindwa kufikia malengo husika.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi huyo, alipokuwa kwenye mkutano wa Wadau wa zao la kahawa mkoani Ruvuma, uliofanyika katika ukumbi wa Jumba la maendeleo wilayani Mbinga mkoani humo.

MTOTO APOTEZA MAISHA BAADA YA KUTAFUNWA NA WANYAMA

Na Steven Augustino,
Tunduru.

MTOTO wa mfugaji mwenye asili ya Kisukuma, walioweka makazi katika kijiji cha Twendembele kata ya Ligunga wilayani Tunduru mkoani Ruvuma, aliyefahamika kwa jina la Shija Luchoma (15) amefariki dunia na mwili wake kuliwa na wanyama wakali, baada ya kuvamiwa wakati akichunga ng’ombe porini katika kijiji hicho.

Taarifa za tukio hilo, zinafafanua kuwa marehemu huyo alikumbwa na mkasa huo baada ya kushambuliwa na mnyama ambaye bado hajafahamika, wakati akiwa machungani kwenye hifadhi ya Selou kijijini humo.   

Baba mzazi wa kijana huyo, Masanja Luchoma alisema tukio lilitokea Machi 26 mwaka huu ambapo marehemu alikuwa ameondoka nyumbani kwake na kundi la ng’ombe hao kwa ajili ya kwenda kuwachunga waweze kupata malisho, ambapo baadaye ilimshangaza mnamo majira ya jioni aliona ng’ombe wakiwa wanarudi peke yao.

APOTEZA MAISHA BAADA YA KUSHAMBULIWA NA VIBAKA

Na Mwandishi wetu,
Tunduru.

SAID Chalres ambaye ni mzee mwenye umri wa miaka 58, mkazi wa kitongoji cha Nanjati kata ya Muhuwesi wilaya ya Tunduru mkoani hapa, ameshambuliwa na baadhi ya vijana ambao wanadaiwa kuwa ni vibaka na kumsababishia afariki dunia.

Vibaka hao walimshambulia mzee huyo, kwa kumpiga mangumi na mateke, kwa lengo la kumpora shilingi 10,000, radio, simu na dagaa ambao alikuwa anatoka kuwanunua katika gene lililopo karibu na kitongoji hicho.

Mashuhuda wa tukio hilo wanaeleza kuwa, wakati anarudi akiwa njiani ndipo walimvamia na kumnyang’anya vitu hivyo na fedha hizo ambazo alikuwa nazo mfukoni.

Akizungumzia tukio hilo kwa njia ya simu, Diwani wa kata hiyo Nurdin Mnolela mbali na kuthibitisha juu ya tukio hilo aliongeza kuwa watuhumiwa baada ya kutimiza adhma yao, walitokomea kusikojulikana.

LITUNGURU AMCOS WASIOLIPA MIKOPO KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA

Na Steven Augustino,
Tunduru.

LITUNGURU Amcos, ambacho ni chama cha wakulima wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, kimewataka wanachama wake kurejesha deni wanalodaiwa na benki ya CRDB shilingi milioni 36 ambazo walikopeshwa kwa ajili ya kununua pembejeo, ili waweze kuboresha mashamba yao ya tumbaku.

Mwenyekiti wa chama hicho Zainabu Baisi alisema kuwa mkopo huo, ulitolewa na benki hiyo katika msimu wa mwaka 2011/2012, hivyo mwanachama ambaye hajajiandaa kurejesha hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Monday, April 6, 2015

RUSHWA YA FEDHA NA MIKAKATI YA UPOTOSHWAJI UFUFUO WA YESU

Padre Baptiste Mapunda.
 Na Padre Baptiste Mapunda,

PASAKA ni sikukuu ya kusherehekea “ushindi wa Yesu” dhidi ya mauti, dhidi ya maovu ya kila aina yanayomshambulia mwanadamu kwa wale wanaomwamini. Yesu amefufuka kweli, kweli kama alivyosema, hayupo kaburini yu hai.

Ujumbe huu ni mzito na wa kushitua ulimwengu wote, hasa kwa waliowakristo na wasiowakristo.

Jumapili ya Pasaka nilisherehekea Parokiani Manzese na ibada ilikuwa na mahudhurio makubwa, pamoja na hamasa ya hali ya juu. Ibada siku zote zinatujenga sana kama mashahidi wa ufufuko wa Kristo.

Jumatatu ya Pasaka nilikuwa na ratiba ya kuhudhuria misa ya saa tatu, ambayo ilikuwa ni ya ubatizo na ndoa. Lakini nikajikuta nasukumwa kwenda kuhudhuria misa ya saa moja, ambayo ilikuwa ni ya wanaumini wa kawaida. Nilipofika Kanisani nilimkuta Padre na mwanashirika mwenzangu, Padre Alex Mutasingwa  ambaye alikuwa kiongozi ibada. 

Sunday, April 5, 2015

TUNDURU WAPITISHA MAKISIO YA KUNUNUA TANI 300 ZA KOROSHO

Na Steven Augustino,
Tunduru.

WANACHAMA wa chama cha ushirika wakulima wa korosho, Litungunru AMCOS katika kijiji cha Mchoteka Wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, kimepitisha bila mabadiliko makisio ya kununua tani 300 katika msimu wa kununua zao hilo kwa mwaka 2015/2016.

Maamuzi hayo yalifikiwa na wanachama hao, kwenye mkutano mkuu uliofanyika kwenye ukumbi wa ghala la wakulima wa chama hicho kijijini humo, ambapo pamoja na mambo mengine walipitisha mapato na matumizi ya mradi wa mazaowenye thamani ya shilingi milioni 480,000,000.

Aidha katika mkutano huo, wanachama waliupatia meno na kuuagiza uongozi wao kuwa wakali katika utendaji na kuangalia uwezekano, wa kuwafuta uanachama wajumbe ambao wamekuwa hawajishughulishi na uzalishaji wa korosho, au kumaliza hisa zao kwa muda mrefu na hivyo kukihujumu chama katika mapato.

Saturday, April 4, 2015

MKURUGENZI MBINGA AHUSISHWA NA KASHFA YA UVUNAJI MSITU BILA KUSHIRIKISHA WANANCHI

Rais Jakaya Kikwete.
Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

WENYEVITI wa vitongoji vya kata ya Matarawe wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, wamejikuta wakiwa katika wakati mgumu baada ya wananchi wa kata hiyo kuwajia juu na kuwataka wajiuzuru katika nafasi zao za uongozi, kutokana na suala la uchanaji mbao katika msitu wao bila kuwashirikisha.

Aidha wananchi hao, wamemnyoshea kidole Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Hussein Ngaga kwa kile walichoeleza kuwa ndiye anayevuna msitu huo ambao unafahamika kwa jina la Mbambi, bila kutoa taarifa kwao.

Hayo yalijitokeza Aprili 2 mwaka huu, katika mkutano walioketi kwenye uwanja wa shule ya msingi Kipika mjini hapa, ambapo wananchi hao walionekana kujawa jazba huku wengine wakizomea na kutotaka kuelewa juu ya hoja iliyoletwa mbele yao na Afisa mtendaji wa kata ya Mbinga mjini, George Maliyatabu.

Kwa mujibu wa maelezo ya afisa mtendaji huyo alisema kuwa yeye alikuwa ametumwa na Mkurugenzi huyo mtendaji, awaeleze wananchi kwamba anawaomba samahani juu ya jambo hilo hivyo atafanya nao kikao cha pamoja ili aweze kuzungumza juu ya tukio hilo, kitendo ambacho kiliendelea kuamsha hasira na kumtaka aondoke katika mkutano huo yeye pamoja na wenyeviti wa vitongoji ambao alifuatana nao.

DEREVA TAKUKURU ASABABISHA MAUAJI MBINGA

Gari la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambalo lilisababisha mauaji, baada ya kumgonga dereva wa pikipiki na mtembea kwa miguu wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma. 
Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

DEREVA aliyekuwa akiendesha gari la Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) wilaya ya Mbinga mkoa wa Ruvuma, Emmanuel Millanzi amenusurika kuuawa na wananchi wenye hasira kali baada ya gari alilokuwa akiliendesha, kugonga na kuua watu watatu papo hapo.

Gari hilo ambalo ni aina ya Everest, lenye namba za usajili AAA 217 MN nalo limenusurika kuteketezwa kwa moto na wananchi hao ambao walishikwa na hasira kutokana na ajali hiyo, kwa kile kilichodaiwa kusababishwa na dereva huyo ambaye alikuwa akiliendesha kwa mwendo kasi.

Waandishi wa habari ambao waliwasili katika eneo la tukio, walielezwa na mashuhuda wa ajali hiyo kuwa gari hilo lilikosa mwelekeo kutokana na kuwa katika mwendo huo, hatimaye kwenda kumgonga mwendesha pikipiki na abiria wake na mtembea kwa miguu ambao wote walipoteza maisha.

Kaimu kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma, Revocatus Malinyi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo lilitokea Aprili Mosi mwaka huu, majira ya saa 3:15 asubuhi katika eneo la mtaa wa Ruhuwiko darajani Mbinga mjini.

Wednesday, April 1, 2015

TAMKO LA MAASKOFU NA WACHUNGAJI KUTOKA MADHEHEBU MBALIMBALI JUU YA TUKIO LA ASKOFU GWAJIMA

SISI maaskofu na wachungaji kutoka makanisa mbalimbali tumeshtushwa na kusikitishwa kwa taarifa ya ugonjwa wa Askofu na mtumishi mwenzetu Josephat Gwajima ambaye tarehe 27/03/2015 alifika kituo cha polisi cha kati kuitikia wito wa polisi uliomtaka kwenda kujibu shutuma za kutumia lugha ya matusi kwa kardinali Pengo.

Tumepata fursa ya kutafakari na kujadili kwa kina hali iliyompata Askofu mwenzetu hasa baada ya kuzingatia kuea Askofu Gwajima alifika polisi akiwa mzima na mwenye afya njema lakini wakati wa akihojiwa na polisi, hali yake ilibadilika ghafla kiasi cha kupelekea yeye kulazwa hospitali ya TMJ akiugua tena kwenye wodi ya wagonjwa mahututi yaani (ICU) katika chumba cha uangalizi maalum.

Maswali yetu makuu ni kitu gani kimempata mwenzetu? Tunajiuliza, je vyombo vya usalama vimekua sio sehemu salama kama zamani?

Tukiwa bado tunatafakari hill, tumeshtushwa tena baada ya kupata taarifa ya kuwa Wachungaji Wasaidizi wa Askofu Gwajima pamoja na walinzi wake waliokuwepo hospitalini hapo kwa ajili ya kumuuguza nao pia wamekamatwa kwa tuhuma za. kutaka kumtorosha Askofu Gwajima. 

GAUDENCE KAYOMBO ARUSHIWA KOMBORA NA WAPIGA KURA WAKE, WAMTAKA AFUTE KAULI KWAMBA HAKUNA MKULIMA ANAYELALAMIKA JUU YA WIZI WA KAHAWA

Gaudence Kayombo, Mbunge wa Mbinga Mashariki ambaye analalamikiwa na wapiga kura wake kwamba anatetea hakuna wizi wa kahawa uliofanyika kwa wakulima wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, jambo ambalo wanamshangaa na kumtaka afute kauli yake huku wakiiomba serikali iingilie kati ili waliohusika na hujuma hiyo wachukuliwe hatua za kisheria. 
Na Kassian Nyandindi,

WAKULIMA wanaozalisha zao la kahawa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma wamesema wanamshangaa Mbunge wao wa Jimbo la Mbinga Mashariki, Gaudence Kayombo kwamba hakuna mkulima anayelalamika juu ya wizi wa fedha baada ya kahawa yao kuuzwa mnadani Moshi, hivyo wamemtaka afute kauli hiyo na kushughulikia matatizo ya wananchi wa jimbo hilo, na sio kukaa kupinga malalamiko yanayotolewa na wananchi wake huku akijua fika kufanya hivyo ni kuendelea kuitesa jamii.

Kwa nyakati tofauti walisema wamekosa imani naye baada ya Mbunge huyo hivi karibuni kusikika kwenye vyombo vya habari, TV na Magazeti akikanusha na kusema wakulima hao wamenufaika na mkopo uliotolewa na Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) na hakuna aliyeibiwa fedha, ambapo ni muda mrefu sasa umepita pamoja na kufikishiwa malalamiko hayo mezani kwake juu ya wizi waliofanyiwa wakulima hao lakini hakuna hatua aliyochukua huku wakiongeza kuwa, huenda anamaslahi yake binafsi ndio maana amekuwa akitumia muda mwingi kutetea jambo hilo.

Walifafanua kuwa umefika wakati sasa, kiongozi aliyechaguliwa na wananchi kuacha tabia ya kutetea watendaji wa serikali ambao ni wezi wakiwaibia wakulima wanyonge na endapo ataendelea kufanya hivyo, ni sawa na kuwatesa wapiga kura wake na kuwanyima fursa za kimaendeleo kwa faida ya kizazi cha sasa na baadaye.

“Huyu Mbunge sisi tunamshangaa sana, anafikia hatua anadanganya watu kupitia vyombo vya habari kwamba hakuna mkulima anayelalamika katika jimbo lake ameibiwa fedha baada ya kahawa kuuzwa mnadani yeye anawezaje kuthibitisha hili, hivyo asubiri mwarobaini wake ataupata uchaguzi mkuu ujao”, walisema.

Utafiti uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini kuwa, Mbunge Kayombo amefikia hatua ya kutoa kauli hizo baada ya Mkurugenzi wake, Hussein Ngaga na viongozi wa vyama vya ushirika, kulalamikiwa na wakulima wa kahawa wilayani Mbinga kupitia vyombo vya habari kuwa wanadaiwa kuwaibia shilingi milioni 783,399,412 katika sehemu ya kahawa zao ambazo waliuza huko mnadani Moshi.

Wakulima hao ni wale ambao walikopeshwa fedha shilingi bilioni 2 na shirika hilo la NSSF kupitia vyama vyao vya ushirika (AMCOS) vilivyopo wilyani humo, ambapo lengo la shirika lilikuwa ni kutoa mikopo yenye gharama nafuu kwa wakulima wadogo wadogo ambao wamejiunga kisheria katika vikundi, hatimaye waweze kujikwamua kiuchumi na waondokane na umasikini.

Malalamiko haya yanafuatia pia, Mkurugenzi huyo kuingilia kati na kupangia matumizi ya fedha juu ya mkopo huo ambao wakulima walikopeshwa, jambo ambalo mpaka sasa amekuwa hataki kutoa hata mwenendo wa fomu ya mauzo ya kahawa zao (Account Sale) ili wakulima waweze kujua hatma ya kahawa yao jinsi gani ilivyouzwa huko mnadani.

“Tumekuwa tukinyimwa hata mwenendo wa matumizi ya fedha zetu tulizokopeshwa na NSSF ambazo ziliingizwa katika akaunti zetu za vyama vya ushirika (Bank Statement) ili tuweze kujua zimetumikaje, kwa sababu wakati wa manunuzi ya kahawa mkurugenzi huyu alikuwa akitupangia matumizi tunakwenda kuchukua fedha benki mpaka ruhusa itoke kwake na kiasi anachotaka yeye, sasa tunahoji hivi kweli hizi ndizo taratibu na sheria za vyama vya ushirika zinavyosema?”, walihoji.

Pamoja na mambo mengine, wakulima wanaolalamikia juu ya hali hiyo wanatoka katika vyama vinne vya ushirika ambavyo ni Mahilo, Ngaka, Ngima na Pilikano ambapo hata viongozi wao wa ushirika nao wanalalamikiwa kwamba wameshirikiana na Mkurugenzi Ngaga kwa namna moja au nyingine kuhujumu fedha hizo za wakulima wa kahawa, huku wakiiomba serikali kuingilia kati ili haki zao ziweze kupatikana.

KAYOMBO ARUSHIWA KOMBORA

Wakulima hao ambao walionekana kuendelea kujawa na jazba, waliibua jipya huku wakiendelea kumrushia kombora Mbunge wao Kayombo wakisema kuwa, mnamo mwezi Agosti mwaka 2012 alianzisha umoja wa wakulima wa kahawa unaofahamika kwa jina maarufu la; Mbinga Umoja Coffee Association, ambao ulilenga wakulima wa kahawa wilayani humo waweze kufanya biashara ya kuuza kahawa yao kwa bei nzuri nchi za nje.