Sunday, December 31, 2017

MADABA WALIA NA SOKO LA TANGAWIZI WAIOMBA SERIKALI IWASAIDIE WAKULIMA


Baadhi ya wakulima wa Tangawizi katika kijiji cha Magingo Halmashauri ya Madaba wakiandaa tangawizi kabla ya kuziweka ndani ya magunia na kusafirisha kwenda sokoni, hata hivyo zao hilo limekumbwa na changamoto ya kukosa soko la uhakika jambo linalowafanya wakulima hao kuuza zao hilo kwa bei ndogo.


Na Muhidin Amri,    
Madaba.

BAADHI ya Wakulima wanaozalisha zao la tangawizi katika kijiji cha Magingo na Mkongotema, kata ya Mkongotema Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Mkoani Ruvuma wameiomba Serikali kuwatafutia soko la kuuza zao hilo ili kuweza kukomesha vitendo vya walanguzi wanaokwenda kuwalaghai wakulima hao kununua tangawizi kwa bei ndogo.

Hali hiyo imefuatia kuporomoka kwa bei ya zao hilo katika jimbo la Madaba kutoka shilingi 4,000 mwaka 2015/2016 hadi kufikia shilingi 700 mwaka 2017 hivyo kuwafanya wakulima hao kuvunjika moyo wa kuendeleza kuzalisha.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari waliotembelea wakulima hao ili kujionea changamoto hiyo walisema kuwa wakati umefika sasa kwa Serikali kutambua matatizo ya wakulima wa zao la tangawizi na kuyatafuta ufumbuzi wa haraka.

NYAMAIGOLO AWAPA SOMO WAPIGA KURA UCHAGUZI MDOGO SONGEA



Na Dustan Ndunguru,       
Songea.

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka kata ya Butobela, Wilayani Geita Mkoa wa Geita, Robert Nyamaigolo amewataka wapiga kura katika uchaguzi mdogo unaotarajia kufanyika Januari 13 mwaka huu katika jimbo la Songea mjini Mkoani Ruvuma, kuhakikisha kwamba wanamchagua mgombea wa Chama hicho ili aweze kutekeleza ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015 kwa vitendo.

Pia amewaasa watendaji, viongozi na wanaCCM kuainisha maeneo ambayo wapinzani walishinda katika uchaguzi wa Serikali za mtaa uliofanyika mwaka 2014 na kuyapangia mkakati kabambe utakaopelekea kuyarejesha mikononi mwa chama mwaka 2019.

Nyamaigolo alisema hayo juzi wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa kampeni ya uchaguzi mdogo wa Ubunge uliofanyika viwanja vya Majengo mjini hapa.

WAKAZI 100 KIGONSERA WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUKATAA KUSHIRIKI SHUGHULI ZA MAENDELEO


Na Muhidin Amri,       
Mbinga.
 
JUMLA ya Wakazi 100 wa kijiji cha Kigonsera kata ya Kigonsera Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, wamefikishwa Mahakamani kwa kosa la kukataa kushiriki katika shughuli za maendeleo ikiwemo ujenzi wa mabweni ya wanafunzi.

Hayo yalisemwa juzi na Mtendaji wa kata ya Kigonsera, Raphael Kalembo wakati alipokuwa akizungumzia ujenzi wa nyumba moja ya walimu katika shule ya Sekondari ya Kigonsera ambayo ujenzi wake ukikamilika, itakuwa na uwezo wa kuishi walimu watakaoweza kufanya kazi ya kufundisha katika shule hiyo.

Ujenzi wa nyumba hiyo ni mkakati wa uongozi wa shule kwa kushirikiana na halmashauri hiyo kutatua kero ya nyumba za kuishi walimu hao katika halmashauri ya wilaya ya Mbinga.

MJI WA MBINGA WAENDELEA KULALAMIKIA UCHAFU WAMSUBIRI KWA HAMU WAZIRI MKUU


Uchafu ukiwa umezagaa katika baadhi ya maeneo ya makazi ya watu mji wa Mbinga mkoani Ruvuma kama ulivyokutwa leo na mpiga picha wetu ambapo baadhi ya wakazi wa mji huo wameonesha kukerwa na uchafu huo na kuutaka uongozi wa Halmashauri ya mji wa Mbinga kutatua kero hiyo haraka ambayo imedumu kwa muda mrefu kabla hayajatokea madhara makubwa. (Picha zote na Muhidin Amri)


Na Muhidin Amri,     
Mbinga.

BAADHI ya Wananchi wa Mji wa Mbinga mkoani Ruvuma, wameitaka Halmashauri ya mji huo kuongeza kasi katika suala la kufanya usafi wa mazingira ili kuweza kuepusha uwezekano wa kutokea magonjwa mbalimbali ya mlipuko ikiwemo kipindupindu hasa kipindi hiki cha masika.

Walisema kuwa kwa muda mrefu halmashauri hiyo imekuwa ikisuasua katika masuala ya utekelezaji wa usafi wa mazingira ya mji huo katika maeneo mbalimbali, huku watendaji wake wenye dhamana wakiona mlundikano wa uchafu mitaani na kushindwa kuchukua hatua madhubuti ya kumaliza tatizo hilo.

John Mapunda ambaye ni mkazi wa mtaa wa Kipika alisema kuwa kipindi hiki ni cha  masika na ndiyo muda ambao hatari zaidi kwa magonjwa ya mlipuko, hivyo Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Robert Kadaso Mageni kwa kushirikiana na wataalamu wake wa masuala ya usafi wa mji huo wanapaswa kuchukua hatua madhubuti ili kuepusha madhara yanayoweza kutokea hapo baadaye.

UZINDUZI KAMPENI ZA UCHAGUZI MDOGO SONGEA: NCHEMBA AWATAKA WANACCM KUVUNJA MAKUNDI



Na Dustan Ndunguru,     
Songea.

NAIBU Katibu Mkuu mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Mwigulu Nchemba amewataka wanachama wa Chama hicho jimbo la Songea mjini Mkoani Ruvuma, kuvunja makundi yaliyojitokeza wakati wa mchakato wa kura za maoni ili kuweza kukirahisishia ushindi CCM katika uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika Januari 13 mwaka huu.

Pia amewataka wananchi wa jimbo hilo kutofanya makosa kupigia kura upinzani kwani kitendo hicho huenda kikasababisha maendeleo waliyofikia kudumazwa kutokana na kudaiwa kuwa na uwezo mdogo wa kuongoza walionao baadhi ya viongozi wa kutoka kambi pinzani.

Mwigulu alisema hayo jana alipokuwa kwenye uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Ubunge uliofanyika kwenye viwanja vya Kibulang’oma kata ya Lizaboni mjini hapa.

Saturday, December 30, 2017

MADABA WATAKIWA KUSHIRIKI VYEMA KATIKA SHUGHULI MBALIMBALI ZA MAENDELEO

Na Mwandishi wetu,    
Madaba.

MKURUGENZI Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Madaba mkoani Ruvuma, Shafi Mpenda amewataka wananchi wa Jimbo la Madaba kuhakikisha kwamba wanashiriki vyema katika shughuli za maendeleo yao ili waweze kuondokana na baadhi ya kero zinazowakabili katika maisha yao ya kila siku.

Aidha Mpenda amewakumbusha wakulima kutumia mvua zilizoanza kunyesha msimu wa mwaka huu katika maeneo mbalimbali, wajikite zaidi katika shughuli za kilimo badala ya kutumia muda wao mwingi kukaa vijiweni na kuzungumzia mambo yanayoweza kuwarudisha nyuma kiuchumi.

Mpenda alitoa kauli hiyo juzi kwa nyakati tofauti wakati alipokuwa akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo  vijijini ambayo inatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali na wananchi katika vijiji mbalimbali.

Friday, December 29, 2017

UJENZI MABWENI MAHANJE MADABA KUSAIDIA KUMALIZA KERO WANAFUNZI WANAOSOMA MBALI NA SHULE


Mkuu wa shule ya Sekondari Mahanje Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Marcelino Kilewa upande wa kulia akimounesha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Madaba, Shafi Mpenda madawati yaliyotengenezwa ambayo ni kwa ajili ya maandalizi ya  kupokea wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza wanaotarajia kujiunga na shule hiyo mara shule zitakapofunguliwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Shafi Mpenda upande wa kushoto akiangalia ukuta wa jengo moja kati ya mabweni mawili yanayojengwa katika shule ya Sekondari Mahanje  kata ya Mahanje ambapo kulia kwake ni Mkuu wa shule hiyo, Marcelino Kilewa.

Na Muhidin Amri,      
Madaba.

UJENZI wa mabweni ya kulala Wanafunzi katika shule ya Sekondari Mahanje, Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Mkoani Ruvuma utasaidia kwa kiasi kikubwa kumaliza kero ya watoto wanaosoma katika shule hiyo kutembea umbali mrefu wa kilometa 12 kutoka majumbani kwao hadi shuleni.

Hivi sasa ujenzi huo ambao unaendelea kufanyika ni wa mabweni mawili makubwa yanajengwa ambayo kila moja litakuwa na uwezo wa kulaza watoto 80.

Shule hiyo ambayo ni ya wasichana na wavulana, yanajengwa majengo hayo kwa ajili ya kulaza watoto hao ambayo sasa yamefikia hatua ya mwisho kukamilika kwake na kwamba, yataweza pia kusaidia hata wanafunzi hao wasiweze kupoteza muda wao wa kuhudhuria ipasavyo vipindi vya masomo darasani.

Wednesday, December 27, 2017

RAIS MAGUFULI ATUNUKIWA TUZO YA AMANI

Dokta John Magufuli.


JOHANNESBURG, Afrika Kusini.

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dokta John Magufuli ametunukiwa tuzo ya amani ya Mandela (Mandela Peace Prize) kwa kuendeleza shughuli ya kulinda amani na kupigania usawa katika kijamii.

Kamati ya tuzo za Mandela kwa mwaka 2017 ilipokea maombi ya wa wania tuzo 4,956.
Wengine waliotunukiwa ni Rais Uhuru Kenyatta aliyeshinda tuzo ya Mandela ya Demokrasia kutokana na kuendeleza demokrasia nchini Kenya.

Kadhalika Mahakama ya juu nchini Kenya na Jeshi la Zimbabwe zimetunukiwa tuzo ya ujasiri (Mandela Boldness) kwa kufanya uamuzi kwa ujasiri kwa masilahi ya mataifa yao.

WATUMISHI WA UMMA HAPA NCHINI KITANZINI


Na Mwandishi wetu,

SERIKALI kupitia Sekretarieti yake ya Maadili hapa nchini, imewataka viongozi wote wa umma kujaza fomu ya tamko la maandishi ambalo linaorodhesha Mali au Rasilimali wanazomiliki, kabla ya kufikia Desemba 31 mwaka huu.

Rasilimali hizo ni zile zinazojumuisha mali za mke na mume pamoja na watoto wao ambao wamezidi umri kuanzia miaka 18 kuwasilisha kwa Kamishna wa maadili, ambapo kwenye tamko hilo litajumuisha mali na rasilimali za kiongozi husika.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 132 ya 1977 Sekretarieti hiyo ya maadili ya viongozi wa umma ni idara inayojitegemea chini ya Ofisi ya Rais, ambayo ilianzishwa kwa ajili ya kusimamia utekelezaji wa sheria ya maadili ya viongozi wa umma namba 13 ya mwaka 1995.

MATUKIO KATIKA PICHA SIKUKUU YA KRISMAS PAROKIA YA RUHUWIKO SONGEA MJINI

Baadhi ya Watawa waliohudhuria Ibada ya mkesha wa sikukuu ya Krismas katika Kanisa la Ruhuwiko Parokia ya Ruhuwiko mjini Songea wakifuatilia mahubiri.

Waimba kwaya wa Kanisa katoliki Ruhuwiko Parokia ya Ruhuwiko Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma, wakiimba wakati wa mkesha wa sikukuu ya Krismas iliyofanyika jumatatu wiki hii. (Picha zote na Muhidin Amri)

KITUO CHA MABASI YA ABIRIA MADABA WAOMBA ZIONGEZWE CHANGARAWE KATIKA MAENEO AMBAYO MAGARI YANASIMAMA

Baadhi ya wachuuzi wa ndizi na biashara nyingine wakiuza bidhaa zao kwa abiria wa gari linalofanya safari zake kati ya Njombe na Songea katika kituo cha mabasi Madaba halmashauri ya wilaya ya Madaba Mkoani Ruvuma.



Na Muhidin Amri,      
Madaba.

KITENDO kilichofanywa cha kukarabati kituo cha Mabasi ya abiria Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Mkoani Ruvuma, kimepongezwa huku baadhi ya abiria na wamiliki wa magari yanayobeba abiria hao wakiuomba uongozi wa halmashauri hiyo, kuongeza changarawe katika maeneo ambayo magari yanasimama katika kituo hicho.

Ombi hilo lilitolewa juzi kwa nyakati tofauti wakati abiria hao na watumiaji wengine wa kituo hicho walipokuwa wakizungumza kwa nyakati tofauti na waandishi wa habari.

Walisema kuwa kazi iliyofanywa ya kukarabati miundombinu ya kituo hicho ni nzuri, lakini wanaomba katika maeneo ambayo magari yanasimama ziongezwe changarawe ili kuondoa hali ya utelezi ambayo hutokea hasa kipindi hiki cha masika.

JAMII YATAKIWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU UJENZI WA MABWENI KIAMILI SEKONDARI MBINGA


Na Mwandishi wetu,
Mbinga.

BAADHI ya Wanafunzi wanaosoma shule ya Sekondari Kiamili iliyopo katika kata ya Kigonsera Halmashauri Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma, wameiomba jamii kuona umuhimu wa kushirikiana na Serikali yao ya awamu ya tano katika kutatua changamoto zinazoikabili shule hiyo hasa katika ujenzi miundombinu mbalimbali kama vile mabweni ya kulala wanafunzi.

Shule hiyo ambayo ina watoto zaidi ya 800 wa kidato cha kwanza hadi cha nne, inakabiliwa na changamoto kubwa ya upungufu wa vyumba vya kulala wanafunzi jambo ambalo limesababisha baadhi ya wanafunzi wa kike sita kwa nyakati tofauti kupata ujauzito na kukatisha masomo yao.

Wakizungumza na mwandishi wetu, baadhi ya wanafunzi waliokutwa shuleni hapo wakiendelea na masomo yao wakati huu wa likizo walisema kuwa, uhaba wa mabweni ni changamoto kubwa kwao hasa ikizingatiwa kuwa baadhi yao wanaishi mbali na eneo la shule na hujikuta wakiingia katika vishawishi vya ngono.

MAHANJE MADABA KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Shafi Mpenda akikagua chanzo cha maji ambacho kitatumika kwa ajili ya mradi mkubwa wa maji unaojengwa na Serika ili kuweza kuwanufaisha wakazi wa kijiji cha Mahanje wilayani humo waweze kuondokana na kero ya muda mrefu ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Madaba, Shafi Mpenda upande wa kulia, katikati Kaimu Mhandisi wa maji wa wilaya hiyo Makarius Nyoni wakiangalia mabomba yanayoendelea kusambazwa kwa ajili ya kukamilisha mradi wa maji katika kijiji cha Mahanje kata ya Mahanje ambao unalenga kumaliza kero ya maji kwa wakazi  wa kijiji hicho.


Na Muhidin Amri,       
Madaba.

WAKAZI 2,196 wanaoishi katika kijiji cha Mahanje kata ya Mahanje Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Mkoani Ruvuma, wanatarajia kunufaika na mradi mkubwa wa maji ambao ujenzi wake unagharimiwa na Serikali, ambapo mara baada ya kukamilika kwake unalenga kumaliza kero ya muda mrefu ya ukosefu wa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi hao.

Akizungumza katika eneo la mradi huo Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, Shafi Mpenda alisema Serikali imetoa shilingi milioni 275 kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo ambao ulianza kutekelezwa mwezi Juni mwaka huu na kwamba utakamilika mwishoni mwa mwezi Februari mwakani 2018.

Mpenda alisema kuwa hapo awali wananchi wa kijiji hicho walibuni mradi wao wa maji kwa ajili ya kumaliza kero ya maji, hata hivyo kutokana na ongezeko la kaya ilisababisha kuwepo kwa upungufu wa maji na Serikali ikaona ni vyema sasa kutoa fedha kwa ajili ya kuboresha huduma hiyo ili wananchi wengi waweze kunufaika na hatimaye kuondokana na kutumia muda wao mwingi kufuata huduma hiyo umbali mrefu.

Tuesday, December 26, 2017

MAGUFULI NA MAJALIWA WALIVYOTIKISA BANDARINI



KAMA kuna mashirika au taasisi za Serikali ambazo zilikuwa na wakati mgumu kwa mwaka huu unaomalizika, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) huwezi kuiweka kando.

Ugumu wake haukutokana tu na ziara za kushtukiza zilizofanywa na Rais John Magufuli na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika Bandari ya Dar es Salaam, bali yale ambayo viongozi hao wakuu wa nchi waliyabaini; wizi, upigaji dili na ubadhirifu wa mali za umma.

Waliibua zaidi ya matukio matano kwa nyakati tofauti bandarini hapo jambo lililoashiria kuwa kulikuwa na mchezo mchafu uliokuwa ukiendelea katika eneo hilo nyeti kwa uchumi wa nchi.

Sunday, December 24, 2017

MAJALIWA AWASHUKIA MADIWANI SONGEA ASISITIZA WASIPOMALIZA TOFAUTI ZAO ATAWAFUKUZA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Na Kassian Nyandindi,     
Songea.

MADIWANI katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, wametakiwa kuachana na makundi yanayoigawa Manispaa hiyo kwani endapo wakiendelea kufanya hivyo wamekuwa wakikwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alisema hayo jana wakati alipokuwa kwenye ziara yake ya siku moja katika mkoa huo.

Majaliwa alisema hayo alipokuwa akizungumza na watumishi pamoja na Madiwani hao mjini hapa, ambapo aliwaambia endapo kama watashindwa kumaliza tofauti zao yeye atawafukuza.

WAZIRI MKUU AMTAKA AFISA ARDHI MANISPAA SONGEA KUMALIZA TATIZO LA MAMA ALIYEDHULUMIWA NYUMBA YA URITHI


Mkazi wa Msamala katika Manispaa ya Songea, Monica Joseph Miti akitoa maelezo yake mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (Hayupo pichani) kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Mwengemshindo ambapo Bibi Miti aliomba asaidiwe kurejeshewa nyumba yake aliyotapeliwa na mtumishi wa Manispaa hiyo baada ya mumewe kufariki dunia.
Na Kassian Nyandindi,        
Songea.

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amemuagiza Afisa ardhi wa Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, Kundaeli Fanuel Ndemfoo afuatilie suala la Bibi Monica Joseph Miti na wanae ambao walidhulumiwa nyumba ya urithi na aliyekuwa mwanasheria wa Manispaa hiyo.

Alitoa agizo hilo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kata ya Mwengemshindo baada ya kupokea bango lililoandikwa na Bibi Miti kuomba arejeshewe umiliki wa nyumba ya marehemu muwewe.

Alipopewa nafasi ya kueleza tatizo lake, Bibi Miti ambaye alimtaja mwanasheria huyo kwa jina moja la Mwakasungura, alidai kuwa mwanasheria huyo alighushi hati ya nyumba na kuwatoa ndani ya nyumba yeye na watoto wa marehemu. 

ASIMAMISHWA KAZI AKIDAIWA KUTENGENEZA MBINU CHAFU ZA KUTAFUNA MAMILIONI YA KAYA MASKINI



Na Muhidin Amri,         
Tunduru.

KAIMU Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, Chiza Malando amemsimamisha kazi Mtendaji wa kijiji cha Chilundundu wilayani humo, Timamu Issa kwa tuhuma ya kutengeneza mbinu chafu ya kutafuna mamilioni ya fedha za Mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF) katika kijiji hicho.

Sambamba na kumsimamisha kazi mtendaji huyo, Mkurungezi huyo amevunja kamati ya watu 14 ambayo ilikuwa ikisimamia utekelezaji wa mpango huo.

Malando alilazimika kuchukua hatua hiyo wakati alipokuwa akizungumza juzi na wanufaika wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika ukumbi wa Chama cha ushirika, Chiliwena Amcos ikiwa ni siku chache tu baada ya mbinu za viongozi hao kutaka kutafuna fedha hizo kubainika na wataalamu wa wilaya hiyo.

WANAOTOA HUDUMA YA KUUZA CHAKULA TUNDURU KUPIMWA AFYA ZAO


Na Muhidin Amri,        
Tunduru.

MGANGA Mkuu wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, Dokta Wendy Robert amesema kuwa idara ya afya katika wilaya hiyo itaanza kupima afya za wananchi wanaotoa huduma ya kuuza chakula katika maeneo mbalimbali wilayani humo.

Akizungumza juzi na baadhi ya watoa huduma alisema kuwa lengo la mpango huo ni kuhakikisha  kuwa kila mtoa huduma anakuwa na afya njema, ili kuepusha uwezekano wa kuambukiza wateja wao hasa pale wanapowahudumia ili kupata watu wenye afya njema watakaoweza kushiriki moja kwa moja katika kazi za maendeleo.

Aidha alisema kuwa zoezi hilo litafanyika kwa wilaya yote ya Tunduru katika migahawa, hoteli na maeneo mengine kwani wapo baadhi ya watoa huduma kama vile kwenye migahawa bado hawajapimwa afya zao jambo linaloweza kuhatarisaha maisha ya watu wengine.

WAZIRI MKUU AWATOA HOFU WAKAZI WA SONGEA JUU YA KULIPWA FIDIA WANAYODAI BILIONI 3.8


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwahutubia jana wakazi wa kata ya Mwengemshindo katika Manispaa ya Songea ambako alienda kusikiliza kero yao ya muda mrefu ya kutolipwa fidia katika ardhi yao ambayo imetwaliwa kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda.
Na Kassian Nyandindi,       
Songea.

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amewatoa hofu wakazi 1,000 wa Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ambao wanadai fidia ya shilingi bilioni 3.8 ya eneo lao ambalo limechukuliwa na kuwa eneo la kiuchumi mkoani humo (Ruvuma SEZ) kwa ajili ya ujenzi wa viwanda.

Amewatoa hofu jana wakati alipokuwa akizungumza na wakazi wa kata ya Mwengemshindo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Manispaa hiyo.

Majaliwa alisema kuwa Serikali ya awamu ya tano inatambua kilio chao ambacho alisema ni cha muda mrefu na kwamba alishawahi kupata ombi maalum kutoka kwa Mbunge wao wa zamani, Leonidas Gama ambaye sasa ni marehemu ili kuweza kumaliza jambo hilo.

Saturday, December 23, 2017

KUTOPATIKANA UMEME WA UHAKIKA KIKWAZO CHA MAENDELEO TUNDURU

Juma Homera, Mkuu wa wilaya ya Tunduru.


Na Mwandishi wetu,    
Tunduru.

BAADHI ya wakazi wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma wameipongeza Serikali ya awamu ya tano kwa hatua  ya kumaliza ujenzi wa barabara ya kutoka Namtumbo hadi Tunduru mkoani humo kwa kiwango cha lami.

Wakizungumza jana kwa nyakati tofauti na mwandishi wetu Alli Mrope, Kassim Kassim na Rashid Uledi walisema kuwa kukamilika kwa barabara hiyo ni hatua moja mbele ya kuharakisha maendeleo ya wananchi wa wilaya hiyo.

Mrope alisema kuwa mbali na kuishukuru Serikali kwa ujenzi huo ameiomba pia kuendelea na mikakati ya kutekeleza miradi mingine ya maendeleo ambayo itasaidia kuharakikisha kukua kwa uchumi.

TUNDURU IDADI YA MAAMBUKIZI UKIMWI YAJA JUU



Na Muhidin Amri,       
Tunduru.

WATU 1,361 kati ya 54,698 sawa na asilimia 2.5 ambao wamefikiwa na huduma ya upimaji wa Virusi Vya Ukimwi (VVU) wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, wamegundulika kuwa na maambukizi ya virusi hivyo katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi kufikia Oktoba mwaka huu.

Imeelezwa kuwa idadi hiyo ni kubwa ikilinganishwa na ile ya mwaka 2016 kwani watu waliopimwa walikuwa 24,459 na 756 waligundulika kuwa na maambukizi mapya ya VVU.

Mratibu wa kudhibiti ugonjwa wa Ukimwi wilayani humo, Dokta Vitalis Lusasi alisema hayo juzi alipokuwa akitoa taarifa ya hali ya maambukizi hayo katika wilaya hiyo.

TUNDURU NA MKAKATI WA KUPUNGUZA VIFO VYA AKINA MAMA WAJAWAZITO



Na Muhidin Amri,    
Tunduru.

JUMLA ya akina mama 16 wamepoteza maisha katika kipindi cha mwaka mmoja, kutoka Januari mwaka jana hadi kufikia Desemba mwaka huu kutokana na matatizo mbalimbali wakati walipokuwa wakijifungua wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma.

Imefafanuliwa kuwa vifo hivyo vimesababishwa na mimba kutunga nje ya mirija ya uzazi, kutokwa damu nyingi wakati wa kujifungua na upungufu mkubwa wa damu kwa akina mama wanaokwenda kujifungua hospitali.

Hayo yalisemwa na Kaimu Mratibu wa huduma ya  afya, uzazi na mtoto wilayani humo, Salome Namlia alipokuwa akizungumza na mwandishi wetu Ofisini kwake.

Thursday, December 21, 2017

HALMASHAURI WILAYA YA MBINGA YAINGIA MKATABA MKOPO WA VIFAA VYA BILIONI 1.2 KUKAMILISHA UJENZI MIRADI YA WANANCHI VIJIJINI

Afisa mipango wa wilaya ya Mbinga, Onesmo Mapunda.


Na Kassian Nyandindi,    
Mbinga.

HALMASHAURI ya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, imeingia mkataba wa kukopa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.2 na Kampuni ya Kisarawe Cement Company Limited na M.M Intergrated Mills Company Limited, ili kuweza kukamilisha ujenzi wa miradi ya maendeleo ya wananchi vijijini.

Aidha imeelezwa kuwa makampuni hayo yapo jijini Dar es Salaam na kwamba mpaka sasa vifaa walivyoanza kuchukua baada ya kuingia mkataba huo ni vya shilingi milioni 462 na kwamba tayari vifaa vya shilingi milioni 150 vimesambazwa katika miradi ya wananchi wilayani humo.

Afisa Mipango wa halmashauri ya wilaya hiyo, Onesmo Mapunda alisema hayo juzi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake, juu ya jukumu la halmashauri hiyo kutoa huduma endelevu za kijamii na kiuchumi kwa wananchi wake.

TUNDURU KUWAPATIA MICHE BURE YA KOROSHO WAKULIMA WAKE



Na Muhidin Amri,    
Tunduru.

HALMASHAURI ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma kwa kushirikiana na bodi ya korosho nchini, imeotesha miche bora ya zao la korosho 638,000 kwa ajili ya kuwapatia miche hiyo bure wakulima wake wanaozalisha zao hilo katika maeneo mbalimbali wilayani humo.

Afisa kilimo wa halmashauri hiyo, Chiza Malando alisema miche hiyo imezalishwa kupitia vikundi vya wakulima ambavyo vilipatiwa elimu juu ya uzalishaji huo na mwitikio wake katika utekelezaji wa jambo hilo umekuwa mzuri.

Lengo la kufanya hivyo ni kuweza kuongeza uzalishaji wa zao hilo ambalo ni tegemeo kubwa kwa kukuza uchumi wa wananchi wa wilaya hiyo.

VYAMA TISA KUPAMBANA UCHAGUZI NAFASI YA UBUNGE SONGEA



Na Muhidin Amri,      
Songea.

VYAMA tisa vimejitokeza kuchukua fomu kwa ajili ya kushiriki uchaguzi mdogo wa nafasi ya Ubunge katika jimbo la Songea mjini mkoani Ruvuma.

Tina Sekambo.
Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, Tina Sekambo amevitaja vyama ambavyo hadi sasa tayari vimekwisha jitokeza kuchukua fomu hizo kuwa ni Chama Cha Mapinduzi (CCM), UPDP, Demokrasia Makini, AFP, TLP, CCK, NRA, ADA na TADEA.

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hadi kufikia jana bado hakikujitokeza kuchukua fomu kwa ajili ya kushiriki katika uchaguzi huo, ambao unafanyika kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo Leonidas Gama wa CCM kufariki dunia mapema mwezi uliopita.