Wednesday, February 28, 2018

WATUMISHI WAZEMBE HALMASHAURI WILAYA MBINGA KUENDELEA KULA KIBANO

Na Kassian Nyandindi,       
Mbinga.

MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga Mkoani Ruvuma, Gombo Samandito amesema kuwa amesikitishwa na utendaji kazi wa Ofisi ya Msimamizi na mdhibiti ubora wa elimu Wilayani humo kwamba Watendaji wa Ofisi hiyo, wamekuwa hawatekelezi majukumu yao ya kazi ipasavyo.
Gombo Samandito.

Samandito alieleza kuwa kutokana na hali hiyo anajiona kama vile anapwaya katika utendaji wake, hivyo atatoa kibano kwa wale wote ambao ni wazembe katika kazi.

Mkururugenzi huyo alisema hayo juzi baada ya kupokea taarifa ya hali ya ukaguzi wa maendeleo ya elimu ya Msingi na Sekondari katika kikao cha tathimini ya elimu kilichofanyika mjini hapa.

Alisema kuwa kumekuwa na visingizio ambavyo havina msingi wowote kwamba Ofisi hiyo inashindwa kutekeleza kikamilifu majukumu yake ya kazi kutokana na kukosa fedha na gari ili waweze kutimiza ipasavyo uendeshaji wa shughuli zao za kila siku.

NJALAMATATA NAMTUMBO WAKOSA MAHALI PA KUISHI BAADA YA NYUMBA ZAO KUEZULIWA NA UPEPO MKALI

Hii ni moja kati ya nyumba ambayo imeezuliwa na upepo mkali ulioambatana na mvua katika kijiji cha Njalamatata kata ya Mkongo Nakalawe Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma.


Na Yeremias Ngerangera,    
Namtumbo.

UPEPO mkali uliokuwa umeambatana na mvua katika kijiji cha Njalamatata kata ya Mkongo Nakalawe Wilayani Namtumbo Mkoa wa Ruvuma, umeleta maafa kwa baadhi ya wakazi wa kijiji hicho kuezuliwa nyumba zao na kukosa mahali pa kuishi.

Tukio hilo limetokea juzi majira ya mchana baada ya nyumba tano kuezuliwa kwenye kijiji hicho na kufanya wakazi hao, wakibaki wanahangaika kutafuta mahali pa kujihifadhi kwa majirani zao.

Kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya hiyo ikiwa imeongozana na Katibu tawala wa Wilaya ya Namtumbo, Adelin Nchimbi walikwenda katika eneo hilo la tukio na kuzungumza na waathirika ambao nyumba zao zimebomolewa na upepo huo uliokuwa umeambatana na mvua hiyo.

Tuesday, February 27, 2018

TARURA TUNDURU YAPONGEZWA KUPUNGUZA KERO VIJIJINI



Na Muhidin Amri,     
Tunduru.

WANANCHI wa kijiji cha Kalulu kata ya Kalulu Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma, wameipongeza Serikali kwa jitihada zake inayofanya katika kupunguza kero za muda mrefu zinazokwamisha kasi ya ukuaji wa maendeleo kwa wananchi vijijini Wilayani humo.

Aidha wananchi hao wamepongeza kazi kubwa zinazofanywa na Meneja wa Wakala wa Barabara (TARURA) Mhandisi, Cyprian Kimwaga kwa kutengeneza barabara inayoanzia kijiji cha Milonde hadi Kalulu Wilayani hapa, kwa kiwango cha changarawe jambo ambalo limewezesha magari kuanza kupita kwenda katika vijiji hivyo ambapo ni muda mrefu yalikuwa yanashindwa kwenda huko kutokana na barabara hiyo kuwa na hali mbaya.

Wakizungumza na kwa nyakati tofauti, jana baadhi ya wananchi walisema kuwa usimamizi na mipango ya TARURA Wilayani Tunduru imefanikisha kutengenezwa kwa barabara hiyo ambayo kwa muda mrefu ilikuwa kero kubwa katika jamii.

Monday, February 26, 2018

MBUNGE MBEYA MJINI NA MWENZAKE WATUPWA JELA KIFUNGO CHA MIEZI MITANO



Na Mwandishi wetu,

HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, imewatia hatiani Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu na Katibu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya nyanda za juu kusini, Emmanuel Masonga na kuwahukumu kifungo cha miezi mitano jela.

Aidha hukumu hiyo imetolewa leo Februari 26 mwaka huu na Hakimu Mkazi mfawidhi wa Mahakama hiyo, Michael Mteite ambapo Sugu na Masonga wamehukumiwa kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais Dokta John pombe Magufuli.

TLA YATOA VITABU VYA MASOMO SONGEA


Na Muhidin Amri,           
Songea.

CHAMA cha Wakutubi Tanzania (TLA) kimetoa vitabu 91 vya masomo ya aina mbalimbali kwa shule mbili za Sekondari katika Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma, ikiwa ni mkakati wa Chama hicho kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuboresha sekta ya elimu hapa nchini.

Shule zilizopata msaada huo ni shule ya Sekondari ya wasichana Songea na ile ya wavulana Songea, pamoja na Chuo cha Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA) Songea ambacho nacho kimepata vitabu.

Mwenyekiti wa TLA, Juliana Manyerere alisema kuwa chama hicho hapa Tanzania hakipo nyuma katika suala zima la elimu kwani mwaka jana 2017 kimeweza kutembelea vyuo vinavyoendesha mafunzo ya Ukutubi vya Tumaini, Slads Bagamaoyo na Dar es Salaam pamoja na kutoa mafunzo kwa walimu Wakutubi 41 wa shule za Sekondari zilizopo katika Manispaa ya Dodoma.

TAKUKURU RUVUMA YAOKOA MABILIONI YA FEDHA MISHAHARA HEWA

Yustina Chagaka, Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Ruvuma.


Na Muhidin Amri,     
Songea.

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Ruvuma, katika kipindi cha  kuanzia mwezi Julai hadi Desemba mwaka 2017 iliweza kuokoa kiasi cha shilingi Bilioni 25,174,375.00 ambapo katika sekta ya elimu fedha zilizookolewa ni shilingi 3,000,000.00 na sekta ya afya ziliokolewa shilingi 22,1743375.00 ikiwa ni mishahara hewa.

Pia taasisi hiyo katika kipindi hicho ilipokea taarifa 221 kutoka kwa wananchi kupitia vyanzo mbalimbali na kwamba idara zilizobainika kuongoza kulalamikiwa ni TAMISEMI malalamiko (57) Ardhi (41) Mahakama (25) Kilimo (15) Polisi (13) Vyama vya siasa (11) na Elimu malalamiko (12).

Mkuu wa TAKUKURU Mkoani hapa, Yustina Chagaka aliwaeleza Waandishi wa habari hivi karibuni kuwa idadi ya kesi zilizoenda Mahakamani ni 11 zilizopo katika Mahakama ya Hakimu mkazi Songea, katika kesi nne zilihusu TAMISEMI, Idara ya afya, TASAF na Sekta binafsi.

WAPOTEZA MAISHA NA WENGINE KUJERUHIWA VIBAYA KATIKA AJALI YA GARI NA PIKIPIKI



Na Kassian Nyandindi,      
Songea.
 
WATU Watano wamefariki dunia na wengine watano kujeruhiwa vibaya katika matukio mawili tofauti, akiwemo diwani wa kata ya Peramiho Issack Mwimba (37) amefariki papo hapo baada ya kugongwa na gari wakati akiwa anaendesha Pikipiki, akitokea Peramiho kuja Songea mjini. 

Kamanda wa Polisi Mkoani Ruvuma, Gemini Mushy akizungumza jana na mwandishi wa habari hizi aliwataja wengine waliofariki kuwa ni Ally Hamis Blanket (34) ambaye ni mkazi wa Songea mjini, Maria Njelwa (35), Seba Chichango (28) na abiria mwingine wa jinsia ya kiume ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja ambao wote ni wakazi wa kijiji cha Ng’ombo Wilaya ya Nyasa Mkoani hapa.

Alifafanua kuwa katika tukio la kwanza ambalo lilitokea Februari 24 mwaka huu majira ya asubuhi huko katika maeneo ya Ruhuwiko mabwawani nje kidogo ya Manispaa ya Songea, kwenye barabara ya kutoka Songea kwenda Wilaya ya Mbinga gari lenye namba za usajili T 604 CXV aina ya Toyota Cresta,

Friday, February 23, 2018

PROFESA NDALICHAKO KUMSOMESHA MDOGO WAKE AKWILINA MPAKA CHUO KIKUU



Na Mwandishi wetu,

ULINZI na Usalama umeimarishwa katika eneo alilozikwa mwanafunzi wa chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline katika kijiji cha Olele Wilayani Rombo.

Mwandishi wetu ambaye aliwasili katika eneo la tukio leo Ijumaa wakati mazishi ya mwanafunzi huyo yanafanyika, alibaini uwapo wa askari wengi wakiwamo wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) na askari kanzu.

Mbali na askari kanzu, walionekana maofisa usalama wa Taifa na Polisi waliovalia kiraia, wakiwa wameegesha magari kimkakati, mita kati ya 100 hadi 150 kutoka nyumbani kwa wazazi wa marehemu.

Wednesday, February 21, 2018

SERIKALI YATAKIWA KUONGEZA KIASI CHA FEDHA UJENZI WA BARABARA TUNDURU


Na Kassian Nyandindi,   
Tunduru.

KATIKA kuchochea kasi ya ukuaji wa maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma, Serikali imeombwa kuongeza fedha kwa ajili ya ujenzi na uimarishaji wa miundombinu ya barabara hasa vijijini Wilayani humo, ambazo hazifanyiwa matengenezo kwa muda mrefu.

Imeelezwa kuwa endapo litatekelezwa hilo hata shughuli za kiuchumi ambazo zinazofanywa na wananchi wataweza kutekeleza kwa urahisi na hatimaye Wilaya nayo kuweza kunufaika na kupiga hatua katika ukuaji wa mapato yake.

Hivi sasa kiasi cha fedha kinachotolewa na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa barabara hizo imeelezwa kuwa ni kidogo ikilinganishwa na mahitaji halisi yanayotakiwa, kwa kuwa Wilaya hiyo ni kubwa na imekuwa na mtandao mkubwa wa miundombinu ya barabara wenye urefu wa Kilometa 1,261.2 sawa na Mkoa jirani wa Mtwara.

MANIAMBA SONGEA KUCHIMBWA MAKAA YA MAWE MIAKA 40 WANANCHI 600 KUPATA AJIRA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Walemavu Jenista Mhagama wa pili upande wa kulia akiangalia kipande cha mkaa wa mawe wakati alipotembelea mgodi wa utafiti wa makaa ya mawe wa Kambas Group Of Companies katika kijiji cha Maniamba kata ya Muhukuru Wilaya ya Songea, wa kwanza upande wa kushoto ni Mwenyekiti wa Kambas Group of Companies Yahaya Yusuf na upande wa kulia ni Mhandisi wa madini wa Kampuni hiyo, Timoth Malima.


Na Mwandishi wetu,           
Songea.

WANANCHI zaidi ya 600 wa kutoka katika vijiji mbalimbali Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma, wanatarajia kupata ajira katika mgodi wa makaa ya mawe uliopo kwenye kijiji cha Maniamba kata Muhukuru Wilayani humo, ambao unatarajiwa kuanza shughuli zake za uchimbaji wakati wowote kuanzia sasa.

Kampuni ya Kambas Group of Companies ambayo imeanza shughuli ya utafiti wa madini hayo tokea mwaka 2017 na kubaini uwepo wa makaa kiasi cha takribani tani milioni 20 ambapo baada ya kukamilisha utafiti huo yataweza kuchimbwa kwa muda wa miaka 40 kwa uzalishaji wastani wa tani 500,000 kwa mwaka.

Yahaya Yusufu ambaye ni Mwenyekiti wa Kampuni hiyo alisema hayo juzi kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge Ajira na Walemavu Jenista Mhagama wakati Waziri huyo alipokuwa ametembelea kujionea shughuli zinazoendelea kufanyika katika mgodi huo ambapo Mhagama alikuwa katika ziara yake ya kuhimiza, kuangalia na kushiriki kwenye shughuli mbalimbali za kimaendeleo katika jimbo lake la Peramiho Wilayani hapa.

Tuesday, February 20, 2018

SERIKALI YATOA SOMO KWA WALIMU SHULE ZA SEKONDARI NCHINI



Na Mwandishi wetu,

SERIKALI imesema kuwa Mwalimu wa shule ya Sekondari kufundisha shule ya Msingi, maana yake sio kwamba kushushwa cheo na kwamba jambo hilo sio la ajabu.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Ofisi ya Rais (Utumishi), Florence Lawrence imesema kuwa Serikali kuwapangia baadhi ya walimu wa Sekondari kufundisha shule za Msingi ni moja ya hatua za kuongeza ufanisi na kuleta mgawanyo sawa wa walimu katika shule hizo.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dokta Laurean Ndumbaro amenukuliwa katika taarifa hiyo ambayo ilitolewa leo Februari 20 mwaka huu.

WAZIRI JENISTA MHAGAMA ATAKA WAWEKEZAJI KUTHAMINIWA


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Walemavu ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Peramiho Wilayani Songea Jenista Mhagama akiangalia sehemu ya makaa ya mawe yaliyochimbwa na Kampuni ya Kambas Group of Companies katika kijiji cha Maniamba kata ya Muhukuru Halmashauri ya Wilaya hiyo, upande wa kulia kwake ni Mwenyekiti wa Kampuni hiyo Yahaya Yusuphu na wa kwanza kulia ni Mhandisi wa madini wa Kampuni, Timoth Malima.


Na Muhidin Amri,        
Songea.

JENISTA Mhagama ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera Bunge, Ajira na Watu wenye ulemavu ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma kuhakikisha wanatumia vizuri asilimia tatu ya mapato yatokanayo na shughuli zitakazoanza za uchimbaji wa makaa ya mawe katika kijiji cha Maniamba kata ya Muhukuru Wilayani humo.

Aidha amesema wanapaswa kuweka mazingira bora yatakayoweza kuwavutia wawekezaji, ambapo hatua hiyo itaweza kutoa fursa kwa wawekezaji wengi kuweza kuwekeza ili mradi huo wa makaa ya mawe uweze kusonga mbele.

Hivi sasa Kampuni ya Kambas Group of Companies imeweza kuanza kuwekeza katika kijiji hicho ili kuweza kufanya kazi zake katika mazingira rafiki ya uchimbaji wa makaa hayo, hivyo Halmashauri hiyo ameitaka pia kuweka mazingira mazuri ambayo hawataweza kukimbiwa na wawekezaji hao.

Monday, February 19, 2018

MAZISHI YA MWANAFUNZI AKWILINA KUFANYIKA IJUMAA NDUGU WAKUSANYIKA MUHIMBILI

Akwilina Akwiline.


HATIMAYE Mazishi ya mwili wa aliyekuwa Mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwiline yatafanyika siku ya Ijumaa Februari 23 mwaka huu Mkoani Kilimanjaro.

Moi Kiyeyeu akizungumza na mwandishi wetu alisema kwamba baada ya kikao cha familia, wamekubaliana kuwa Akwilina atazikwa Mkoani humo baada ya kuagwa Februari 22 mwaka huu katika viwanja vya chuo hicho Mabibo jijini Dar es Salaam.

Akwilina alifariki dunia Februari 16 mwaka huu baada ya kupigwa risasi akiwa kwenye daladala, wakati Polisi wakiwatawanya waandamanaji ambao ni wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendelea (CHADEMA).

VIONGOZI WAANDAMIZI CHADEMA WATAKIWA POLISI



Na Mwandishi wetu,

VIONGOZI Waandamizi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wameitwa na Jeshi la Polisi wakitakiwa kwenda kuripoti leo jioni Februari 19 mwaka huu.

John Mrema ambaye ni kiongozi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje kwa chama hicho alithibitisha hilo kwamba wameitwa kwa barua hiyo ambayo wameipokea makao makuu ya chama majira ya saa kumi jioni.

Ambapo barua hiyo inawataka kwenda kuripoti kwa Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum Dar es Salaam katika Ofisi yake.

Sunday, February 18, 2018

DOKTA MAGUFULI ASIKITISHWA KIFO CHA MWANAFUNZI AKWILINA SERIKALI KUGHARIMIA TARATIBU ZA MAZISHI

Dokta John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Na Mwandishi wetu,

DOKTA John Pombe Magufuli, ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametoa kauli yake akizungumzia juu ya kifo cha mwanafunzi aliyepigwa risasi na Polisi, Februari 16 mwaka huu.

Katika ukurasa wake wa twitter, Rais Magufuli ameandika ujumbe kuhusu kusikitishwa kwake na kifo cha Akwilina Akwiline na kuagiza vyombo vya dola kuwachukulia hatu waliohusika kufanya hivyo.

“Nimesikitishwa sana na kifo cha mwanafunzi Akwilina Akwiline wa Chuo cha Usafirishaji (NIT),

TUNDURU WANUFAIKA NA KIWANDA CHA KUBANGUA KOROSHO


Wafanyakazi wa kiwanda cha kubangua korosho kinachofahamika kwa jina la Korosho Africa Limited kilichopo katika Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma, wakiendelea na kazi zao kama walivyonaswa na kamera yetu ambapo wakazi zaidi 750 kutoka ndani ya Wilaya hiyo wameweza kupata ajira katika kiwanda hicho kinachotajwa ndiyo mkombozi mkubwa hasa kwa watu maskini Wilayani hapa.

KUKAMILIKA UJENZI WA DARAJA MTO NANYUNGU TUNDURU KUMALIZA KERO ZA WANANCHI

Daraja  linalojengwa na Serikali chini ya Wakala wa ujenzi Mjini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya Tunduru, kwa gharama ya shilingi bilioni 115.804 lenye urefu wa mita 45 katika mto  Nanyungu kijiji cha Fundimbanga Wilayani humo kama linavyoonekana katika picha ambapo kukamilika kwake kutasaidia kukua kwa maendeleo  ya wananchi wa Wilaya hiyo.


Na Kassian Nyandindi,    
Tunduru.

UJENZI wa daraja kubwa la kisasa katika mto Nanyungu litakalounganisha kijiji cha Fundimbanga na vijiji vingine Wilayani Tunduru Mkoa wa Ruvuma, limeanza kujengwa ili kuweza kuondoa kero mbalimbali zilizodumu kwa muda mrefu ambazo walikuwa wakipata wananchi wa Wilaya hiyo.

Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) Wilayani hapa, ndiye ambaye ameanza kazi ya usimamizi wa ujenzi huo na kwamba kukamilika kwa daraja hilo, imeelezwa kwamba kutarahisisha mawasiliano kati ya pande hizo mbili kwa maeneo ya vijiji hivyo.

Meneja wa TARURA Wilaya ya Tunduru, Mhandisi Cyprian Kimwaga alisema kuwa kujengwa na kukamilika kwa daraja hilo kutamaliza pia kero ya wananchi kuvuka kwa kutumia daraja la miti lililopo katika mto huo.

Thursday, February 15, 2018

MKE NA MUME WAKAMATWA CHINA NA DAWA ZA KULEVYA MTOTO ARUDISHWA TANZANIA



Baadhi ya dawa za kulevya.
Na Mwandishi wetu,

WATANZANIA wawili wamekamatwa nchini China, January 19 mwaka huu wakiwa wamemeza dawa za kulevya tumboni kwenye uwanja wa ndege wa Baiyun Guangzhou.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na kupamba na dawa za kulevya nchini, Rogers Siang’a aliwataja watuhumiwa hao ni Baraka S. Malali na Mkewe Ashura H. Mussa ambapo wamekamatwa wakiwa na mtoto wao mdogo mwenye umri wa miaka 2 na miezi 9.

Kamishna Siang’a alisema kuwa baada ya kukamatwa walihifadhiwa kwenye chumba maalum kwa muda, ndipo Baraka alitoa Pipi 47 kwa njia ya haja kubwa huku Ashura akitoa Pipi 82.

ASKOFU DALLU AVITAKA VYOMBO VYA DOLA KUZINGATIA UTOAJI HAKI



Na Kassian Nyandindi,    
Songea.

ASKOFU wa Kanisa Katoliki Jimbo kuu la Songea, Damian Dallu amesema kwamba suala la kuombea amani hapa nchini halitaweza kufanikiwa, endapo kama vyombo vya dola havitazingatia utoaji wa haki kwa wananchi wake.

Dallu alisema hayo jana wakati alipokuwa akihubiri kwenye ibada ya misa takatifu ya Jumatano ya majivu, iliyofanyika katika Kanisa kuu la kiaskofu la mtakatifu Mathias Kalemba mjini Songea.

Alisema kuwa amani haiwezi kupatikana katika taifa lolote lile kama vyombo vya dola havitatenda haki kwa wananchi wake, huku akidai kuwa ili amani iweze kudumishwa na kuwa endelevu ni lazima vyote viwili viende kwa pamoja.

Tuesday, February 13, 2018

SERIKALI YABAINI NJIA ZINAZOTUMIKA KUPITISHA DAWA ZA KULEVYA

Upande wa kushoto ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikabidhi gari kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Rogers Sianga katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi wetu,

KASSIM Majaliwa ambaye ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amesema kuwa Serikali imebaini kwamba maeneo ya bahari kuu, bandari, vituo vya mabasi pamoja na viwanja vya ndege hapa nchini ndiyo yanatumika zaidi kupitisha dawa za kulevya.

Wafanyabiashara, wasambazaji na watumiaji wa dawa hizo alisema kuwa wamekuwa wakikamatwa lengo ikiwa ni kuhakikisha kwamba biashara hiyo inakomeshwa na kumalizika kabisa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Ofisi ya Waziri Mkuu imesema kuwa Waziri huyo ametoa kauli hiyo wakati akikabidhi gari kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Rogers Sianga katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

WAZIRI JAFFO AGOMA KUZINDUA MRADI WA MAJI CHAMWINO DODOMA


Na Mwandishi wetu,

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (TAMISEMI) Seleman Jaffo, amegoma kuzindua mradi wa maji katika kijiji cha Itiso Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma kutokana na baadhi ya wananchi kuharibu kwa makusudi miundombinu hiyo.
Seleman Jaffo.

Akizungumza na wananchi wa kijiji hicho, Waziri huyo alisema kuwa awali mkandarasi aliyekuwa akijenga mradi huo alikuwa akisuasua na kwamba Halmashauri ya Chamwino iliamua kumbadilisha Mhandisi wa maji, ili kuweza kukamilika kwa haraka ujenzi wake na wa kiwango chenye bora.

Imeelezwa kuwa wananchi wa kijiji cha Itiso wamekuwa hawana ushirikiano mzuri na viongozi wao na wale waliokuwa wakijenga mradi jambo ambalo limekuwa likisababisha uwepo wa uharibifu wa miundombinu hiyo ya maji.

ROTALY CLUB NA MIKAKATI YA UTUNZAJI MAZINGIRA SONGEA

Baadhi ya viongozi wa Rotaly Club, tawi la Songea Mkoani Ruvuma wakiangalia kitalu kimojawapo cha miche ya miti kilichooteshwa na Club hiyo, ili miti iweze kusambazwa katika shule za msingi na sekondari katika Manispaa ya Songea Mkoani hapa.

Rais wa Rotaly Club tawi la Songea, Albert Kessy wa pili kushoto akiwa pamoja na baadhi ya viongozi wenzake wa Club hiyo wakikabidhi miche ya miti kwa Mratibu wa asasi isiyokuwa ya kiserikali aliyekuwa katikati ya Roots and shoots, Oddo Ngatunga inayofanya kazi ya uelimishaji kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari Mkoani Ruvuma juu ya masuala ya uhifadhi wa mazingira kwa jamii.


Na Muhidin Amri,     
Songea.

BAADHI ya shule za Msingi na Sekondari zilizopo katika Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma, zimekabidhiwa aina mbalimbali ya miche ya miti kutoka kwa Rotaly Club tawi la Songea iliyopo mjini hapa ili waweze kuipanda kwenye maeneo yao, ikiwa ni lengo pia la kurudisha uoto wa asili na utunzaji wa mazingira katika shule hizo.

Miche hiyo ambayo imekabidhiwa ni ile ambayo imeoteshwa katika vitalu kwa shule hizo ambayo ni miti 4,000 kati ya 15,000 wanayotarajia kuiotesha katika msimu wa mwaka huu.

Rais wa Club hiyo tawi la Songea, Albert Kessy alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na mwandishi wetu ambapo alidai kuwa miti ambayo wanaizalisha kwenye vitalu hivyo ni ile aina ya matunda, mbao, kivuli na mapambo.

Sunday, February 11, 2018

SHIRIKA LA MAENDELEO LA PETROLI TANZANIA LATOA MSAADA WA SHILINGI MILIONI 25 KWA HALMASHAURI YA TUNDURU UJENZI KITUO CHA AFYA NAKAYAYA

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma Juma Homera, upande wa kulia akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 25 kutoka kwa Meneja mawasiliano wa Shirika la Maendeleo la Petroli Nchini (TPDC) Marie Msellemu kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha afya Nakayaya Wilayani humo.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Juma Homera, katikati akiwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Chiza Malando aliyekuwa upande kulia wakifurahia mfano wa hundi ya shilingi milioni 25 iliyotolewa na Shirikala Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha afya Nakayaya ambacho kinatajwa mara kitakapokamilika kitasaidia kusogeza huduma karibu za matibabu kwa wakazi wa maeneo yanayozunguka  kituo hicho, upande wa kushoto ni Meneja mawasiliano wa TPDC Marie Msellemu.

BARAZA LA MAASKOFU TANZANIA LATOA UJUMBE MZITO WA KWARESMA



BARAZA la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limetoa ujumbe wa Kwaresma wa mwaka 2018 ndani yake likitoa msimamo kuhusu masuala ya kisiasa, kiuchumi na kijamii nchini.

Ujumbe huo ulioandikwa na maaskofu wote 35 wa TEC wakiongozwa na Rais wake, Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa upo katika kitabu cha kurasa 20 ikiwa ni maandalizi ya ibada hiyo ya siku 40, kipindi ambacho ni cha mfungo wa sala kukumbuka siku 40 za Kristo kufunga na kwenda jangwani.

Hali ya kisiasa 

Katika ujumbe huo, TEC imesema kwamba uamuzi wa Serikali kuzuia maandamano, mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa ni kwenda kinyume cha Katiba ya nchi.

MAMBO YALIYOLITIKISA BUNGE HAYA HAPA



Na Mwandishi wetu,
Dodoma.

LICHA ya Mkutano wa 10 wa Bunge la 11 uliomalizika juzi kuwa mahsusi kwa ajili ya kamati za kudumu kuwasilisha taarifa zake ambazo hufuatiwa na mijadala mizito hasa ya ufisadi, safari hii haikuwa hiyo pekee kwani kuna mambo matano makubwa yaliyoibuka na kutikisa chombo hicho, baadhi yakiwa hayatokani na taarifa hizo.

Katika mkutano huo uliofanyika kwa siku 12 na kumalizika juzi, kamati zilizowasilisha taarifa zake ni; Hesabu za Serikali (PAC); Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC); Bajeti; Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC); Viwanda, Biashara na Mazingira.

Nyingine ni Kamati ya Ardhi, maliasili na utalii; Kilimo, Mifugo na Maji; Miundombinu; Katiba na Sheria; Utawala na Serikali za Mitaa; Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama na ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.

SERIKALI YA TANZANIA KUJIONDOA KATIKA MPANGO WA KUSAIDIA WAKIMBIZI



SERIKALI ya Tanzania imesema kwamba inajiondoa katika mpango wa Umoja wa mataifa wa kusaidia wakimbizi kuanza maisha mapya katika mataifa yanayowahifadhi.

Tanzania limekuwa eneo salama kwa wakimbizi wengi na sasa inahifadhi zaidi ya wakimbizi 250,000 wa nchi ya Burundi ambao walitoroka mzozo.

Rais Dokta John Pombe Magufuli amesema kwamba taifa lake linajiondoa kutokana na tatizo la usalama pamoja na lile la kifedha.

Saturday, February 10, 2018

TAKUKURU RUVUMA YAOKOA MAMILIONI YA FEDHA MISHAHARA HEWA

Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Ruvuma, Yustina Chagaka.


Na Kassian Nyandindi,      
Songea.

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Ruvuma, imeokoa zaidi ya shilingi milioni 25 ambazo zilitaka kutumika kama mishahara hewa na idara mbalimbali za Serikali Mkoani humo.

Yustina Chagaka ambaye ni Mkuu wa taasisi hiyo Mkoani hapa alisema hayo juzi wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari mjini hapa.

Chagaka alikuwa akitoa taarifa ya Mkoa wa Ruvuma katika kipindi cha miezi tisa iliyopita, ambapo alisema kuwa kati ya fedha zilizookolewa zaidi ya shilingi milioni 22 ni za sekta ya afya na milioni 3 ni kutoka sekta ya elimu.

Friday, February 9, 2018

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI ATOA AGIZO KWA JESHI LA POLISI NCHINI

Waziri wa mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba.

Na Mwandishi wetu,

WAZIRI wa Mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba amelitaka Jeshi la Polisi hapa nchini kuziachia Pikipiki zote ambazo wamezishikilia kwa muda mrefu, na zile zenye makosa madogo pia waziachie wasikae nazo kwa muda mrefu mpaka zinafikia hatua ya kuwa vyuma chakavu.

Mwigulu alisema yale yenye makosa makubwa kama uhalifu wa kivita, madawa ya kulevya na wale wanaotelekeza wabaki nazo wafanye utaratibu wa kuwapeleka Mahakamani au kuziteketeza, na zile zenye makosa madogo watatue haraka na kuwarudishia wenye zao huku wakiwapatia elimu wamekosea wapi.

“Wapeni masomo wamekosea wapi waelekezeni na waliowabishi warekebisheni lakini tusirundike tukatengeneza vyuma chakavu kwa hivi vitu ambavyo utatuzi wake tunao, tutumie huu mkono kutatua kwa yale ambayo yapo ndani ya mamlaka yetu”, alisema Mwigulu.

DOKTA KIGWANGALLA AWAPATIA MTIHANI WAMILIKI WA HOTELI



Na Mwandishi wetu,

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dokta Hamis Kigwangalla amewataka wamiliki na waendeshaji wa hoteli za daraja la kati kumwandikia mapendekezo yatakayomwezesha kutoa uamuzi sahihi, juu ya namna wanavyoweza kuchangia mapato ya nchi.
Dokta Hamis Kigwangalla.

Akizungumza jijini hapa leo Dokta Kigwangalla alisema kuwa uchunguzi umebaini kuwa hoteli zenye hadhi ya kati na nyumba za kulala wageni maarufu 'Guest House' zimekuwa zikipokea watalii wengi kutokana na ubora wake unaochangiwa na unafuu wa bei.

Waziri huyo alieleza kuwa tafsiri ya watalii haimaanishi Wazungu pekee bali ni wageni wowote wanaotumia nyumba za kulala wageni, kutoka nje ya eneo hilo wakiwemo wanaofika kwa ajili ya mikutano na shughuli za biashara.

“Mnaweza kuniambia hoteli zetu zina hadhi ya chini kwa sababu bei ya chumba ni kati ya Shilingi 40,000 hadi 70,000 lakini tunafahamu hizi hoteli Wazungu wameshazijua na wanalala kwenye hoteli zenu na mnaweza kuanza kuwatoza kwa dola”, alisema Kigwangalla.

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA ZA KISHERIA WANAOUZA MBOLEA BEI JUU MBINGA


Na Kassian Nyandindi,     
Mbinga.

SERIKALI Wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma, imetoa onyo kali kwa Wafanyabiashara wanaojishughulisha na uuzaji wa Mbolea ya kukuzia mazao shambani Wilayani humo, kuzingatia bei elekezi iliyotolewa na Serikali na sio vinginevyo.

Mhandisi Gilbert Simya.
Aidha imeelezwa kuwa msako mkali unaendelea kufanyika ili kuweza kuwakamata na kuwachukulia hatua kali za kisheria, watu wanaodaiwa kuficha mbolea ya ruzuku ambayo ni ya kukuzia mazao aina ya UREA na baadaye huuza bei ya juu kwa wakulima tofauti na maelekezo yaliyotolewa na Serikali.

Katibu tawala wa Wilaya hiyo, Mhandisi Gilbert Simya alisema hayo leo wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari Ofisini kwake juu ya tatizo la uhaba wa mbolea za kukuzia mazao shambani lililopo Wilayani hapa.

ASILIMIA 54 TASAF MANISPAA SONGEA WANALIPWA KWA NJIA YA MTANDAO

Baadhi ya Wanufaika wa TASAF mtaa wa Mtendewawa Manispaa ya Songea wakipokea fedha za Ruzuku zinazotolewa na mfuko huo kwa kaya maskini.


Na Kassian Nyandindi,    
Songea.

HALMASHAURI ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma, imeanza kutoa malipo kwa njia ya Mtandao kwa kaya maskini zipatazo 4,880 zilizopo katika mpango wa kunusuru kaya maskini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Mratibu wa Mfuko huo katika Manispaa hiyo, Christopher Ngonyani alisema kuwa kati ya kaya hizo kaya 2,638 sawa na asilimia 54 zinapokea fedha kwa njia ya mitandao ya simu na kaya 2,242 sawa na asilimia 46 bado zinapokea fedha kwa njia ya fedha taslimu. 

Alisema kuwa katika kipindi cha mwezi Januari hadi Februari mwaka huu kaya 2,242 zimelipwa fedha taslimu zaidi ya shilingi milioni 88 na kaya 2,638 zimelipwa kwa mtandao zaidi ya shilingi milioni 88 na kufanya jumla ya zaidi ya shilingi milioni 176 zimetolewa kwa wanufaika wote katika kipindi hicho.

Wednesday, February 7, 2018

KIPINDUPINDU CHATOKEA MBINGA NA KUATHIRI WATU 28 KIJIJI CHA ULIMA UKATA



Na Kassian Nyandindi,      
Mbinga.

MLIPUKO wa Ugonjwa wa Kipindupindu umetokea katika kijiji cha Ulima, kata ya Ukata Wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma na kuathiri watu 28 Wakazi wa kijiji hicho, ambao wote wamenusurika kupoteza maisha baada ya timu ya wataalamu kuwahi kutoa tiba katika eneo la tukio.

Taarifa zilizomfikia Mwandishi wetu kutoka kwa Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya hiyo, Hussein Sepoko alisema kuwa tukio la ugonjwa huo liliambatana na watu hao kuugua vimelea vilivyoambatana na dalili za kuhara na kutapika, ambapo kati ya hao wagonjwa 19 walikuwa wanawake na 9 wanaume.

Sepoko alisema kuwa chanzo kikubwa cha ugonjwa huo kilitokana na kuchafuliwa kwa vyanzo vya maji na uhaba wa vyoo katika kijiji hicho, ambapo wananchi wengi wamekuwa wakitumia mto uliopo kijijini humo ambao ndiyo mpaka unaotenganisha Wilaya ya Mbinga na Nyasa.