Thursday, December 20, 2012

KELVIN MAPUNDA: ZINGATIENI ELIMU MNAYOPEWA NA WALIMU WENU

Diwani wa Kata ya Mbinga mjini Kelvin Mapunda(Aliyevaa koti jeusi) akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Mbambi, Mbinga na Nyerere zilizopo katika kata hiyo wakati akiwa katika ziara yake ya kutembelea vituo vya masomo wakati wa likizo vilivyopo katika kata hiyo. Lengo la wanafunzi hao kuwa pamoja katika kituo hicho ni kuwaongezea ujuzi na maarifa katika masomo yao, na huu ni mpango ambao umwekwa na uongozi wa wilaya ya Mbinga, ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi kwa mitihani ya darasa la nne na la saba. Hata hivyo Diwani huyo aliwataka wanafunzi hao kuzingatia masomo yao. Vilevile katika ziara hiyo alitembelea vituo vinne vinavyotumika kufundishia watoto hao katika kata hiyo, ambavyo vipo shule ya msingi Mbinga, Makita sekondari, Lupilisi english medium school na shule ya msingi Mahela.(Picha na Kassian Nyandindi)

AKUTWA NA MAUTI BAADA YA KUIBA MATITA YA NYASI


Na Steven Augustino,
Tunduru.

MKAZI  wa kijiji cha Tingunya  wilayani Tunduru Ruvuma, anayefahamika kwa jina la Matatizo Mohamedi(27) anashikiliwa na Jeshi la polisi kwa tuhuma za mauaji ya kukusudia katika tukio lililotokea kijijini hapo Desemba 12 mwaka huu.

Kamanda wa polisi wa mkoa huo Deusidedith Nsemeki alisema

kuwa mtuhumiwa huyo  anashikiliwa kwa tuhuma za kumuua kwa kumpiga kichwani kwa kutumia mguu(Tendegu) la kitanda baada ya kutokea ugomvi kati yao.

Kamanda Nsemeki alimtaja aliyefariki dunia katika
  tukio hilo kuwa ni mtu aliyefahamika kwa jina la Maulio Tikiri(14) aliyedaiwa kupigwa na Tendegu hilo Kichwani, na kupoteza maisha muda mfupi baada ya kufikishwa katika kituo cha afya cha Nakapanya kwa matibabu wilayani Tunduru.

KATIBU WA JUMUIYA YA WAZAZI RUVUMA NUSURA AZICHAPE NA KATIBU WAKE WA WILAYA


Na Steven Augustino,
Songea.

KATIBU wa Jumuiya ya wazazi mkoa wa Ruvuma na wa wilaya ya Tunduru mkoani humo, wamenusurika kuchapana makonde, kwa kile kinachodaiwa kutokana na katibu wa jumuiya hiyo kutoka Tunduru, kumpelekea barua ya uhamisho katibu wa jumuiya hiyo mkoani humo.

Katibu wa jumuiya hiyo mkoani humo Lotali Mbawala na katibu huyo wa Tunduru Deogratias Lweyemamu ndio waliotaka kuzua kizaa zaa hicho, baada ya Lweyemamu kudaiwa kumpelekea barua ya uhamisho  Mbawala, kwenda makao makuu ya jumuia ya wazazi taifa.

Kizaa zaa hicho pia kilichoonesha kuwashitua wajumbe wa kamati ya utendaji  ya mkoa, ilifikia hatua kumtaka Mbawala atii taratibu zilizoamriwa na ngazi husika na kumtaka akabidhi ofisi hiyo kwa Lweyemamu ambaye alionesha barua ya uteuzi wake kuwa Kaimu katibu wa jumuiya ya wazazi wa mkoa wa Ruvuma.

Saturday, December 15, 2012

MCB YASISITIZA WATEJA WAKE KUNUNUA HISA KWA WINGI, LENGO KUKUZA MTAJI WA BENKI



 Baadhi ya Wanahisa wa Benki ya wananchi Mbinga (MCB) wakiwa katika picha ya pamoja leo, mara baada ya kufanya mkutano wao maalum wa kujadili namna ya kukuza mtaji wao wa benki, uliofanyika kwenye ukumbi wa Mbiku hoteli Mbinga mjini. (Picha na Kassian Nyandindi)





Na Kassian Nyandindi,


Mbinga.

MWENYEKITI wa bodi ya Benki ya Wananchi Mbinga mkoani Ruvuma(MCB) Altemius Millinga, amewataka wateja wa benki hiyo, kuendelea kununua hisa kwa wingi ili kukuza mtaji wa ndani wa benki.

Hivi sasa benki hiyo tokea ianzishwe mwaka 2003 imeweza kujiendesha na kufikia kuwa na mtaji wa shilingi milioni 347,238.

Rai hiyo ilitolewa leo na Mwenyekiti huyo katika mkutano maalum wa wanahisa wa MCB, ulioketi kwenye ukumbi wa Mbiku hoteli uliopo mjini hapa.

“Ndugu zangu hisa zilizonunuliwa hadi sasa ni 32,555 tu, hizi ni kidogo tunaomba tuongeze juhudi ya kuendelea kuzinunua kwa wingi, ili tufikie malengo yetu tuliyojiwekea na benki iweze kusonga mbele”, alisisitiza.

Millinga alisema mafanikio ya kimaendeleo ya benki ya wananchi Mbinga hayawezi kusonga mbele, kama Wanahisa hawatakuwa tayari kununua hisa kwa wingi ambazo zitaifanya benki iweze kukuza mtaji wake wa ndani.

Thursday, December 13, 2012

KUSHINDWA KUTOA TAARIFA YA MAENDELEO YA WANANCHI NI ISHARA GANI ?

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu.




















Na Kassian Nyandindi,                         Uchambuzi.              

NIMEKUWA nikitafakari kwa kina juu ya tukio lililojitokeza siku kadhaa zilizopita katika ziara ya Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, iliyofanyika hapa wilayani Mbinga na Nyasa mkoani humo.

Tafakari zangu zinaenda sambamba na mkuu wa mkoa huo Said Mwambungu kuwajia juu viongozi wa wilaya hizo, baada ya kushindwa kumuandalia taarifa iliyo katika misingi ya upembuzi yakinifu.

Binafsi namuunga mkono Mwambungu, kwa kuligundua hili mapema na sitakosea nikisema hivi sasa Taifa hili linahitaji viongozi walio makini kama yeye na wenye kupembua mambo kwa haraka, ili tuweze kusonga mbele kimaendeleo.

Tuesday, December 11, 2012

UONGOZI WA WILAYA YA MBINGA NA NYASA LAWAMANI, NI BAADA YA MKUU WA MKOA WA RUVUMA KUIKATAA TAARIFA YA MAENDELEO YA WILAYA HIZO

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma(Kushoto) Said Mwambungu, akiwa katika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Mbinga leo, majira ya saa 3:15 asubuhi wakati alipokuwa akiikataa taarifa ya maendeleo ya wilaya ya Nyasa na Mbinga kutokana na kutoandaliwa kwa misingi ya upembuzi yakinifu. Upande wa kulia aliyevaa suti nyeusi ni mkuu wa wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga na kati kati ni mkuu wa wilaya ya Nyasa Ernest Kahindi.(Picha na Kassian Nyandindi)

Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.


MKUU wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu, amewajia juu viongozi wa wilaya ya Nyasa na Mbinga kwa kushindwa kuandaa taarifa sahihi za maendeleo ya wilaya hizo.



Sambamba na hilo mkuu huyo wa mkoa amekataa kupokea taarifa ya maendeleo ya wilaya hizo leo, wakati alipokuwa katika ziara yake ya siku nne ya kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kitendo cha mkuu huyo wa mkoa kukataa taarifa hizo kilijitokeza katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Mbinga, baada ya kusomewa na ofisa mipango wa wilaya hiyo, Seleman Mwamba na kuwapa muda wa nusu saa kuandaa taarifa nyingine kabla hajaanza ziara yake rasmi.

Sunday, December 9, 2012

MATANKI HAYA YANATUMIKA KUSAFIRISHIA UDONGO WENYE URANI

Baadhi ya waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma(Pichani) wakimsikiliza Mjiolojia mkuu wa Mantra Tanzania, Emmanuely Nyamsika, wakati alipokuwa akitoa maelezo juu ya matanki yanayotumika kusafirishia udongo wenye madini ya Uran kwa kutumia ndege aina ya Helkopta kwa ajili ya kwenda kufanyiwa utafiti katika maabara zilizopo Mwanza hapa nchini na nje ya nchi za Australia, Afrika Kusini na Uingereza. Baada ya kufanyiwa utafiti udongo huo wenye madini hurejeshwa tena katika eneo hilo la utafiti wilayani Namtumbo. (Picha na Kassian Nyandindi)

HII NI RAMANI HALISI INAYOONESHA ENEO LA MRADI



Waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma na wataalamu wa Mantra Tanzania, wakiwa wameizunguka ramani(Iliyowekwa chini) ambayo inaonesha eneo halisi linalofanyiwa utafiti na litakalochimbwa madini hayo mara baada ya serikali kutoa kibali chake.(Picha na Kassian Nyandindi)

HIVI NDIVYO TUNAVYOCHORONGA MADINI YA URANI



Waandishi wa habari wakipokea maelezo kutoka kwa mjiolojia mkuu wa Mantra Tanzania Emmanuely Nyamsika, namna madini ya Urani yanavyochorongwa na kuhidhiwa katika mifuko maalum.(Picha na Kassian Nyandindi)

MADINI YA URANI NAMTUMBO BADO HAYAJAANZA KUCHIMBWA WATANZANIA TUSIPOTOSHWE

Madini ya Urani yakionekana kujitokeza juu ya ardhi katika eneo la mto Mkuju hifadhi ya Selous, wilayani Namtumbo.(Picha na Kassian Nyandindi)
Na Kassian Nyandindi,
Namtumbo.

UVUMI na kauli zilizokuwa zikielezwa na watu mbalimbali kwamba kazi ya uchimbaji wa madini aina ya Urani katika mto Mkuju uliopo pori la hifadhi ya Selous, wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma kwamba umeanza sio kweli, badala yake kinachofanyika ni kukamilisha kazi ya utafiti wa madini hayo.

Waandishi wa habari wa wa mkoa huo wamefanya ziara maalumu ya kutembelea mradi wa mto huo ambako kampuni ya Mantra Tanzania inatarajia kuanza ujenzi wa mgodi wa madini hayo.

Kauli zinazotolewa na watu mbalimbali ambapo wamekua wakidai mradi huo haufai kwa kuwa unahatarisha maisha ya binadamu kutokana na athari za mionzi na uharibifu wa mazingira.

MJIOLOJIA: ENEO MOJAWAPO LILILOFANYIWA UTAFITI HILI HAPA

 


Waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma, wakiwa pamoja na baadhi ya wataalamu wa kampuni ya Mantra Tanzania, katika eneo mojawapo ambalo utafiti unafanyika kwa kuchukuliwa udongo wenye madini ya Urani.(Picha na Kassian Nyandindi)

NYAMSIKA: ENEO LILE NDILO LITAKALOCHIMBWA URANI

Waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma, wakioneshwa eneo la mto Mkuju ambalo hapo baadaye mara baada ya serikali kutoa kibali cha kuruhusu kuchimba madini hayo, yataanza kuchimbwa. Anayeonesha kwa mkono ni Mjiolojia mkuu wa kampuni ya Mantra Tanzania, Emmanuel Nyamsika. Waandishi hao walifanya ziara hiyo leo ili kujiridhisha juu ya uvumi uliojitokeza kuwa madini hayo yameanza kuchimbwa lakini imebainika kwamba kazi ya uchimbaji bado haijaanza kutokana na serikali bado haijatoa kibali cha kuruhusu kazi hiyo kuanza kufanyika.

WAANDISHI WA HABARI RUVUMA NA UTAFITI WA MADINI YA URANI NAMTUMBO

Mjiolojia mkuu wa kampuni ya Mantra Tanzania, upande wa kushoto anayezungumza, Emmanuely Nyamsika akiwapa maelezo waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma juu ya mapipa yanayotumika kusafirishia URANI kwenda katika maabara za kufanyia utafiti zilizopo Jijini Mwanza na nchi za Afrika Kusini, Australia na Uingereza.Waandishi hao walitembelea leo katika eneo ambalo utafiti huo unafanyika mto Mkuju wilayani Namtumbo mkoani humo. (Picha na Kassian Nyandindi).

MTUHUMIWA WA MAUAJI AACHIWA HURU



Na Steven Augustino,
Tunduru.

MAHAKAMA Kuu kanda ya Songea mkoani Ruvuma kupitia vikao vyake vinavyoendelea wilayani Tunduru, imemuachilia huru Suzana Kapinga(28) aliyekuwa anakabiliwa na shauri  namba Rm11/2012 la mauaji ya kukusudia, kinyume cha sheria kifungu namba 196 sura ya 16 cha kanuni ya adhabu.

Pamoja na kumuachilia huru pia mahakama hiyo imetoa masharti ya kuomba mtuhumiwa huyo kuwa chini ya uangalizi wa maafisa tabibu wa magonjwa ya akili katika hospitali iliyopo Gereza la ISANGA mjini Dodoma.

Akifafanua hukumu hiyo msajili wa mahakama Kuu mwenye mamlaka ya kijaji Wilifred Peter Ndyansobera alisema kuwa, maamuzi hayo yaliyofanyika na mahakama hiyo imebaini na kuzingatia taarifa iliyotolewa na Daktari wa hospitali ya Milembe, alikopelekwa kwa ajili ya uchunguzi kubaini kuwa pamoja na  mtuhumiwa huyo kutenda kosa hilo la mauaji hayo lakini mtuhumiwa huyo hakuwa amedhamiria kufanya kosa hilo.

ACHOMWA MOTO NA KUFARIKI DUNIA BAADA YA KUIBA SIMU

 






Picha ya marahemu aliyeiba simu na mwili wake kuchomwa moto na kutupwa porini kijiji cha Mbesa wilayani Tunduru.(Picha na Steven Augustino)










Na Steven Augustino,
Tunduru.

Mkazi wa Kijiji cha Mbesa wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, aliyejulikana kwa jina la Seif Jaffari(18) ameuawa kikatili na wananchi wenye hasira kali baada ya kumtuhumu ameiba simu.

Mauaji hayo ya kinyama yalifuatia na kipigo kikali alichokipata na wananchi hao walimchoma moto na mwili wake kuteketezwa kwa porini.

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa kabla ya kifo hicho marehemu akiwa na wenzake waliiba simu 6 ambazo zilikuwa zikichajiwa katika nyumba ya Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Chikomo aliyefahamika kwa jina moja la Mwl. Komba iliyopo kijijini humo.

Thursday, December 6, 2012

TUACHENI TUPATE MVINYO, TUKIFURAHIA NDOA YETU





Pascal Mwabesa na mkewe wakinyweshana kinywaji, wakati wakiwa ukumbini (UVIKAMBI) kusherehekea ndoa yao.(Picha na Muhidin Amri)

TUPO KATIKA POZI TUKIFURAHIA NDOA YETU


 
 
 
 
 
Pascal Mwabesa akiwa na mkewe katika pozi mara baada ya kufunga pingu zao za maisha. (Picha na Muhidin Amri)

TUPO NA WAPAMBE WETU


 
 
 
Pascal Mwabesa na mkewe wakiwa katika viwanja vya kanisa la mtakatifu Alois Gonzaga, mara baada ya kufunga ndoa yao huku wakisindikizwa na wapambe wao.(Picha na Muhidin Amri)

TUNAONESHA PETE ZETU, HII NI ISHARA YA UPENDO




Maharusi Pascal Mwabesa na mkewe Gonzalva Lupogo wakionesha pete zao za ndoa kwa ndugu na jamaa waliofika kushuhudia ndoa yao katika kanisa la Mtakatifu Alois Gonzaga mjini Mbinga.(Picha na Muhidin Amri)

WAKIVISHANA PETE KATIKA TUKIO LA KUFUNGA NDOA





Pascal Mwabesa akimvalisha pete ya ndoa mkewe Gonzolva Lupogo wakati wa ndoa yao katika kanisa la Mtakatifu Alois Gonzaga mjini Mbinga juzi.(Picha na Muhidin Amri)

ZIARA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA


Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Shamshi Vuai Nahodha akiangalia vyakula vinavyopikwa na askari wakiwa vitani, wakati alipotembelea kambi ya mazoezi ya vikosi vya jeshi kutoka brigedi ya 401 kv Songea juzi wilayani Namtumbo. Kulia ni mkuu wa kikosi cha 411 Meja Yahaya Chausi.(Picha na Muhidin Amri)

Wednesday, December 5, 2012

MBINGA: SHULE YAFUNDISHA WANAFUNZI BILA KUSAJILIWA

Wanafunzi wa shule ya msingi Twiga Mbinga, wakipata kifungua kinywa.


















Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

WATOTO hawa(Pichani) ni wanafunzi wa shule ya msingi Twiga iliyopo mtaa wa Mapera, kata ya Mbinga mjini mkoani Ruvuma, kama walivyokutwa na kamera yetu. 

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini kuwa shule hiyo inafundisha watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu. Lakini shule haijasajiliwa rasmi na kupewa kibali na serikali kuendesha masomo ya shule ya msingi.

Pamoja na serikali kupitia wizara yake husika kukemea shule kama hizi ziache kutoa huduma mpaka zipewe usajili, hali hiyo imekuwa kinyume katika shule hiyo na hii inaonesha ni ukiukwaji wa taratibu na sheria zilizowekwa. 

Hivyo tunashauri viongozi husika wa wilaya ya Mbinga, kuchukua hatua za haraka kunusuru hali hiyo kabla viongozi wengine kutoka ngazi ya taifa wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi, kuchukua hatua juu ya tatizo hili. 

Ofisi ya Mkurugenzi mtendaji na Mkuu wa wilaya ya Mbinga tunahitaji suala hili lifanyiwe kazi ili kusaidia watoto hawa waweze kupata elimu bora na sio kama ilivyo sasa, ukizingatia kwamba shule hiyo hata haina vifaa vya kutosha katika kukidhi mahitaji muhimu ya mwanafunzi anapokuwa darasani.

Cha kushangaza shule hii ina miaka mitano sasa, ikiendelea kutoa huduma hiyo bila kusajiliwa, Je viongozi tupo makini hapo katika kutekeleza majukumu yetu?


WANAOWAPA MIMBA WANAFUNZI KUKIONA CHA MOTO

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu.
















Na Steven Augustino,
Songea.

SERIKALI mkoani Ruvuma imeamua kuanzisha kampeni maalumu ya kukabiliana na wahusika wa vitendo vya kuwapa mamba wanafunzi kwa kutoa agizo kwa viongozi wa wilaya na halmashauri zote zilizopo mkoani humo.

Hizo ni juhudi zake kuhakikisha kuwa inakomesha wimbi kubwa la upataji wa mimba kwa watoto wakike wanaosoma katika shule za msingi na sekondari.

Kampeni hiyo inawahamasisha wananchi kuwabaini wanaume ambao wamekuwa wakiwashawishi watoto wa kike  na kuwaharibia mfumo wa masomo na maisha   yao.

Hayo yalisemwa na mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu alipokuwa akizungumza katika kikao cha kamati ya ushauri cha mkoa wa Ruvuma, kilichoketi hivi karibuni katika ukumbi wa Songea Club mjini hapa, ambapo pamoja na mambo mengine aliwaagiza wakuu wa wilaya na wakurugenzi watendaji wa halmashauri pamoja na viongozi wengine kuhakikisha wanaweka mikakati ya kukabiliana na tatizo hilo ambalo linazidi kuongezeka siku hadi siku mkoani humo.

ATEKETEZWA KWA MOTO AKITUHUMIWA KUIBA SIMU


Na Steven Augustino,
Tunduru.

MKAZI mmoja wa kijiji cha Mbesa wilayani Tunduru, mkoani Ruvuma ameuwawa kikatili, na wananchi wenye hasira kali na mwili wake kuuteketeza kwa kuchomwa moto.

Aliyefanyiwa kitendo hicho cha kinyama ni Seif Jafari(18) baada ya kumtuhumu ameiba simu.
Kabla ya mauaji hayo wananchi hao walimuangushia kipigo kikali  na kwamba
akiwa na wenzake wanadaiwa kuiba simu 6 ambazo zilikuwa zikichajiwa katika nyumba ya mwalimu mkuu wa shule ya msingi Chikomo aliyefahamika kwa jina moja la Mwl. Komba.

AFARIKI DUNIA BAADA YA KUNYWA GONGO


Na Mwandishi maalum,
Tunduru.

MTU mmoja mkazi wa Tunduru mjini mkoani Ruvuma, amefariki dunia wakati akiendesha mkokoteni ambao huutumia kubebea mizigo ya aina mbalimbali ya wateja wake, baada ya kunywa pombe haramu aina ya gongo.

Aliyefariki hufahamika kwa jina la Rashid Mpembu kwa jina maarufu “Wamunyama”(43) ambapo kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na mashuhuda wa tukio hilo, walisema kuwa Mpembu alianguka ghafla na kupoteza maisha wakati akisukuma mkokoteni huo.

Walisema tukio hilo lilitokea wakati akiwa amebeba viroba viwili vya mahindi ambayo inadaiwa kuwa alikuwa akiwapelekea wateja wake, kukoboa na kusaga katika mashine mojawapo mjini Tunduru.

ASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA MAUAJI


Na Mwandishi wetu,
Tunduru.
JESHI la Polisi mkoani Ruvuma limechukua hatua ya kumshikilia dereva wa kampuni “Progressive Higleig Jv Contractors”, inayojenga mradi wa barabara ambao kwa sasa unaosuasua wa kwa kiwango cha lami Kutoka wilaya ya Namtumbo hadi Tunduru, anayefahamika kwa jina la Philip Chigana kwa tuhuma za kusababisha mauaji.
Kamanda wa polisi wa mkoa huo Deusdedith Nsemeki alisema hayo kwa waandishi wa habari na kuongeza kuwa katika tukio hilo pia dereva huyo alimgonga mtoto wa miaka 12 na kumjeruhi vibaya.
Akifafanua taarifa hiyo alisema kuwa ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Mletele Manispaa ya Songea na kuongeza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi.

Monday, December 3, 2012

POLISI RUVUMA KUFUKUA KABURI ALILOZIKWA KICHANGA


Na Steven Augustino,
Songea.

JESHI la Polisi mkoani Ruvuma limeahidi kuomba Kibali cha Mahakama ili waweze kufukua kaburi linalodaiwa kuzikwa kitoto kichanga kwa kile kinachoelezwa, kunyimwa na kuzikwa na mama yake Jenister Mapunda (24).

Kuwepo kwa mkanganyiko wa hapa na pale unaoendelea kuzua maneno na taarifa tofauti na kuwachanganya wananchi, ndiko kunakolifanya jeshi hilo kufikia hatua hiyo.

Kamanda wa Polisi wa mkoa huo Deusdedith Nsemeki alisema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika mahojiano maalumu, na kuongeza kuwa uchunguzi huo pekee ndio utakao ondoa utata na maneno yalityopo sasa.

KAHINDI: JENGENI MIUNDO MBINU RAFIKI YA WALEMAVU

 Mkuu wa wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma Ernest Kahindi, akihutubia wananchi(Hawapo pichani) waliohudhuria siku ya maadhimisho ya walemavu duniani yaliyoadhimishwa kiwilaya, wilayani Mbinga, Mbinga mjini. Katikati ni Mwenyekiti wa walemavu wa wilaya hiyo Martin Mbawala na kulia kwake ni Diwani wa kata ya Mbinga mjini Kelvin Mapunda. Katika hotuba yake Kahindi aliwataka wataalamu wa serikali na jamii kwa ujumla kujenga(majengo) miundo mbinu rafiki na mazingira ya walemavu ili waweze kuitumia kwa urahisi kulingana na maumbile yao. (Picha na Kassian Nyandindi)

NAKABIDHI SHAIRI LANGU KWA KIONGOZI

Mlemavu wa ngozi(Albino) Dada Shukrani Ndunguru (kulia) akikabidhi shairi lake alilomaliza kuimba siku ya walemavu iliyoadhimishwa kiwilaya Mbinga mjini, kwa mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya ya Nyasa Ernest Kahindi. Anayeshuhudia kulia kwa mgeni rasmi ni mkuu wa wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga. Shairi hilo lilisheheni ujumbe ambao ukiitaka jamii na serikali kwa ujumla kuwajali watu wenye ulemavu na sio kuwabagua katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.(Picha na Kassian Nyandindi)

VIONGOZI WAKIBADILISHANA MAWAZO




 Mkuu wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Senyi Ngaga(aliyenyosha mkono) na wa Nyasa Ernest Kahindi (Katikati) wakibadilishana mawazo katika sherehe za maadhimisho siku ya walemavu duniani, zilizofanyika kiwilaya Mbinga mjini. (Picha na Kassian Nyandindi)

AKINA MAMA NA SIKU YA WALEMAVU MBINGA



 Akina mama wa mtaa wa Matarawe Mbinga mjini mkoani Ruvuma, wakicheza kwa pamoja na kufurahia sherehe za maadhimisho ya walemavu zilizofanyika kiwilaya wilayani Mbinga, mjini hapa mbele ya mgeni rasmi Ernest Kahindi (Hayupo pichani, Picha na Kassian Nyandindi)

WAKUBWA WAKITAFAKARI



Mkuu wa wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga na wa Nyasa Ernest Kahindi, wakifuatilia kwa pamoja matukio ya michezo mbalimbali(Haipo pichani) iliyokuwa ikichezwa katika siku ya maadhimisho ya walemavu yaliyofanyika Kiwilaya Mbinga mjini. (Picha Kassian Nyandindi)

WATOTO NA SIKU YA WALEMAVU



Watoto walemavu(Albino) na wasiokuwa walemavu, wakicheza kwa pamoja kusherehekea sherehe za maadhimisho ya siku ya walemavu zilizofanyika Mbinga mjini, mkoani Ruvuma mbele ya mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Nyasa Ernest Kahindi. (Hayupo pichani). (Picha na Kassian Nyandindi)

DIWANI AKIFURAHIA SIKU YA WALEMAVU




Diwani wa Kata ya Mbinga mjini mkoani Ruvuma, Kelvin Mapunda (kulia) akisakata dansi wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya walemavu duniani yaliyoadhimishwa kiwilaya mjini hapa. (Picha na Kassian Nyandindi)

SHEREHE YA WALEMAVU MBINGA

 Mkuu wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma Senyi Ngaga, (kushoto) akimkaribisha Mkuu wa wilaya ya Nyasa Ernest Kahindi aliyekaa ambaye amevaa taji, katika sherehe za kilele cha maadhimisho siku ya walemavu duniani kwa wilaya ya Mbinga yalifanyika mjini hapa na mgeni rasmi alikuwa mkuu wa wilaya hiyo ya Nyasa. Kulia ni Mwenyekiti wa Walemavu wa wilaya ya Mbinga Martin Mbawala. (Picha na Kassian Nyandindi)

UCHAFU: TASWIRA KATIKA JAMII


 Watoto hawa huku hawajui wakihatarisha afya zao, walikutwa na kamera yetukatika mtaa wa KKKT Mbinga mjini mkoani Ruvuma, wakiwa wanacheza na kuzunguka katika ghuba ambalo taka na uchafu wa aina mbalimbali humwagwa hapo. Ni vyema wazazi tuwaelimishe watoto wetu waache kucheza katika maeneo machafu kama haya.

Thursday, November 29, 2012

GAUDENCE KAYOMBO AWATAKA WANANCHI WAKE KUJITUMA KATIKA SHUGHULI ZA KIMAENDELEO


Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

WANANCHI wa jimbo la Mbinga Mashariki mkoani Ruvuma, wametakiwa kuendelea kujituma katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo ili waweze kuondokana na umaskini, ambao umekuwa ukiitesa jamii miongoni mwao.

Mbunge wa jimbo hilo Bw. Gaudence Kayombo(Pichani) alisema hayo wakati alipokuwa akizungumza na Mwandishi wa habari hizi, juu ya mikakati mbalimbali ya kusukuma maendeleo katika jimbo lake.

Bw. Kayombo alisema kuwa anafurahishwa na wananchi wa jimbo la Mbinga Mashariki, kwamba wengi wao wamekuwa wakijituma katika shughuli za maendeleo hasa katika nyanja ya kilimo cha mazao mbalimbali.

Wednesday, November 28, 2012

BALOZI ALITOA TAARIFA ZA KUPOTOSHA

BALOZI wa Marekani katika umoja wa mataifa Susan Rice amekiri kwamba alitoa habari zisizokuwa sahihi, kufuatia shambulio lililotekelezwa dhidi ya ubalozi mdogo wa Marekani nchini Libya mwezi Septemba.

Shambulio hilo lilisababisha kifo cha balozi wa marekani nchini Libya Christopher Stevens.

WAPINGA JESHI KUWAZUIA WANAWAKE MAREKANI

CHAMA cha kupigania haki za kiraia nchini Marekani kimewasilisha kesi mahakamani kupinga uamuzi wa jeshi la taifa hilo, kuwapiga marufuku wanajeshi wa kike kufanya kazi katika maeneo ya vita.

Chama hicho ambacho kiliwasilisha kesi hiyo kwa niaba ya wanajeshi wanne wa kike kinasema sera hiyo inakiuka katiba.

Kundi hilo linasema licha ya hatua ya kulegeza sera hiyo katika miaka ya hivi karibuni, wanawake bado wananyimwa fursa ya kuhudumu katika nyadhfa zaidi ya mia mbili vitani katika jeshi la Marekani.

WAKAMATWA KWA PESA HARAMU

WAZIRI wa mambo ya ndani wa Bolivia, Carlos Romero amesema, kuwa maafisa kadhaa wa serikali wametiwa mbaroni kwa kujaribu kupokea pesa kutoka kwa mfanyibiashara mmoja kutoka Marekani ambaye anahudumia kifungo cha jela nchini humo.

Wale waliokamatwa ni pamoja na Mkurugenzi wa maswala ya kisheria katika wizara ya mambo ya ndani Fernando Rivera.

WAANDAMANAJI WAKESHA KUMPINGA RAIS

Rais Mursi wa Misri anapingwa kwa kujilimbikizia madaraka












WAANDAMANAJI wamekesha usiku kucha katika medani ya Tahrir mjini Cairo kuelezea hasira zao dhidi ya tangazo la rais wao anayezingatia itikadi za kiislamu Mohammed Morsi kujipatia madaraka makubwa.

Walikesha wakiimba nyimbo za kumlaani rais pamoja na vuguvugu lake la kiislamu la Muslim Brotherhood.
Jana Jumanne, maelfu ya waandamanaji walifurika katika medani hiyo wakiandaa mandamano kadhaa huku wakisema watamkiuka rais Mursi huku wakipinga mamlaka aliyojilimbikizia.

TUNDURU WAITAKA SERIKALI KUWABANA VIONGOZI WASIOWAJIBIKA IPASAVYO


Na Steven Augustino,
Tunduru.

BAADHI ya wakulima wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, wameitaka serikali kuwabana viongozi wenye tabia ya kujinufaisha matumbo yao kupitia pembejeo za ruzuku ili wananchi waweze kuboresha mashamba yao katika msimu huu wa kilimo.

Hayo yalisemwa na wadau mbalimbali waliohudhuria katika mdahalo wa kukusanya maoni kupitia mdahalo wa kuwajengea uwezo juu ya utekelezaji wa shughuli za sekta ya kilimo uliowahusisha wadau wa kilimo kutoka jimbo la Tunduru Kaskazini uliofanyika ukumbi wa Skyway mjini hapa.

Kadhalika wakulima hao   walishauri kwamba serikali iangalie uwezekano wa kuondoa utaratibu wa kupeleka pembejeo hizo kwa wakulima wake na badala yake  ihamasishe wawekezaji kujenga viwanda vingi ili kuongeza uzalishaji na fedha hizo kuingizwa kama hisa katika viwanda hivyo ili mbolea au mbegu ziuzwe kwa bei nafuu.

Wakifafanua wakati wa kuchangia maoni yao kwa nyakati tofauti Bw. Sekula Matumla, Bw. Addo Makanya, Rashid Issaya, Halifa Chitemwe na Bi. Sarra Mwingira walisema kuwa hali hiyo inatokana na viongozi wa halmashauri ya wilaya hiyo wakiwemo wawakilishi wao madiwani na wabunge, kutokuwa na mwamko wa kusimamia kikamilifu ugawaji wa pembejeo za ruzuku zinazotolewa na serikali.

Tuesday, November 27, 2012

TAARIFA YA KIFO CHA SHARO MILIONEA HII HAPA

Sharo Milionea afariki dunia mkoani Tanga.

















Msanii na mwigizaji maarufu nchini Tanzania Sharo Milionea amefariki dunia leo saa 2:00 usiku mkoani Tanga kwa ajali ya gari.

Kamanda wa polisi mkoani Tanga, amesema kwamba msanii hiyo amepata ajali saa 2:00 usiku tarehe 26, Novemba, 2012.

“Leo majira ya saa 2:00 usiku kwenye Barabara ya Segera Muheza mtu mmoja alietambulika kwa jina la Hussein Ramadhani au Sharo Milionea akiwa anaendesha gari namba T478 BVR Toyota Harrier akitokea Dar es salaam kwenda Muheza,


"alipofika eneo la Maguzonizonga wilayani Muheza, gari lake liliacha njia na kupinduka mara kadhaa na kusababisha kifo chake, mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza”, amesema Kamanda huyo.

Monday, November 26, 2012

HALMASHAURI YATENGA BAJETI YA SHILINGI MILIONI 40 KWA MIRADI YA KILIMO

Na Dustan Ndunguru,
Songea.
HALMASHAURI ya wilaya ya Songea mkoani Ruvuma, imetenga kiasi cha shilingi milioni 40 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kilimo katika kipindi cha mwaka 2012 hadi 2013.

Mwenyekiti wa kamati ya uchumi ujenzi na mazingira Bw. Teofanes Mlelwa, alisema hayo alipokuwa akizungumza na mwandishi wetu, juu ya utekelezaji wa miradi ya DADPS katika kipindi hicho.

Bw. Mlelwa ambaye pia ni diwani wa kata ya Wino Songea vijijini,  alivitaja vijiji vitakavyonufaika na fedha za mradi huo wa maendeleo ni Mpandangindo, Matimira ambavyo vitalima zao la alizeti, Wino na Lilondo na Liganga vitajikita katika kilimo cha zao la kahawa, ambapo vijiji vya Muhukuru Nakawale na Ngadinda vyenyewe vitashughulika na kilimo cha zao la korosho na kwamba kijiji cha Magingo kitajihusisha na kilimo cha zao la Tangawizi ifikapo June 2013.

SERIKALI MKOANI RUVUMA KUMUONDOLEA UVIVU MKANDARASI WA BARABARA YA NAMTUMBO TUNDURU



Na Steven Augustino,

Songea.


SERIKALI mkoani Ruvuma imesema, imefikia mwisho wa kuendelea kumvumilia mkandarasi anayejenga barabara kwa kiwango cha lami, kutoka wilaya ya Namtumbo kwenda Tunduru mkoani humo, yenye urefu wa kilometa 192 kwa madai kuwa ameshindwa kazi na ujenzi wake haukidhi viwango vinavyotakiwa.



Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bw. Said Mwambungu amesema hayo na kuitaja kampuni hiyo kuwa ni ya Progressive Higleig Jv Contractors.

WAFANYABIASHARA WAJERUHIWA NA MAJAMBAZI TUNDURU



Na Steven Augustino,
Tunduru.

WATU wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wamemvamia mfanyabiashara mmoja anayenunua mpunga na kujeruhiwa kwa silaha za jadi huku akikatwakatwa mapanga na kufanikiwa kuporwa fedha tasilimu.
Taarifa za tukio hilo zinadai kuwa maharamia hao walifanikiwa kupora shilingi milioni 4,500,000.

Licha ya kujeruhiwa mfanyabiashara huyo kadhalika wenzake aliokuwa nao ambao ni Nurudin Mshamu, maarufu kwa jina Chinga(30) aliyekuwa naye akipelekwa kununua mpunga katika kijiji cha Mpanji wilayani Tunduru mkoani Ruvuma.

Saturday, November 24, 2012

VIONGOZI WA MAZIWA MAKUU WAJADILI DRC

 
Mkimbizi wa Goma akiingia kambi ya Umoja wa Mataifa nje ya Goma

Ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyochapishwa awali juma hili iliishutumu Rwanda kuwa inawasaidia wapiganaji hao, shutuma ambazo zinakanushwa na serikali ya Rwanda.

Kiongozi wa kiraia wa kundi la wapiganaji wa M23 piya yuko kwenye mkutano wa Kampala.

Haijulikani mchango wake ni wa kiasi gani kwenye mkutano huo wa dharura wa viongozi wa kanda ya Maziwa Makuu.

Wapiganaji wanataka kuzungumza ana kwa ana na serikali ya Congo.

Lakini Rais Joseph Kabila anasema atazungumza tu na Rwanda.
Huku nyuma wapiganaji wanaendelea kusonga mbele wakielekea kusini na kaskazini kutoka shina lao mjini Goma.

Umoja wa Mataifa unasema kikosi chake kilioko huko kitajaribu kuwazuwia wapiganaji wasisonge mbele, lakini umesema askari wake wa kuweka amani hawawezi kubeba jukumu la jeshi la serikali ya Congo.(BBC News)

SERIKALI YAOMBWA KUJENGA SOKO LA MAZAO TUNDURU


Na Steven Augustino,
Tunduru.

WAKULIMA  wa zao la korosho wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma wameiomba serikali  kuchukua hatua za haraka, kutatua kero ya kukosekana kwa soko la mazao wanayozalisha hali inayowafanya, kuuza mazao hayo kwa walanguzi wanaotumia kipimo
maarufu kwa jina la Kangomba, ili waweze kusukuma maisha yao ya kila siku.

Pamoja na malalamiko hayo wakulima hao walitumia nafasi hiyo kuishauri halmashauri ya Tunduru kupunguza ushuru wa mazao ambao umekuwa ukitozwa sasa kwa wakulima wake shilingi 200 kwa debe.

Kilio hicho kilipazwa na wakulima hao kupitia mdahalo wa mchakato wakukusanya maoni ya wananchi katika utekelezaji wa shughuli za sekta ya kilimo uliowahusisha wadau wa kilimo kutoka katika  Jimbo la Tunduru Kusini na kufanyika katika  ukumbi wa Skyway mjini hapa.

Friday, November 23, 2012

RAIS ATAKA JINA LA NCHI LIBADILISHWE

Rais wa Mexico amewasilisha mswada kwa bunge la Congress kutaka jina rasmi la nchi hiyo kubadilishwa.

Jina la sasa la jimbo la Mexico lilianza kutumiwa mwaka 1924 baada ya kupata uhuru kutoka Uhispania .

Hata hivyo halijakuwa likitumiwa na rais Felipe Calderon anataka libadilishwe na kuwa Mexico tu.

MZOZO KUHUSU BAJETI YA EU

Viongozi wa Ufaransa na Ujerumani wamesema kuwa wana shaka ikiwa makubaliano yaliyofikiwa kuhusu bajeti ijayo ya muungano wa ulaya katika mkutano wa EU unaoendelea.

Rais wa ufaransa Francois Holland na Chancella wa Ujeruamani, Angela Merkel walisema hayo baada ya kuhudhuria ufunguzi wa mkutano huo ambao ulifanyika saa tatu baada ya muda uliotarajiwa kutokana na tofauti zilizokuwepo kuhusu mipango ya bajeti.

MKUU WA MAJESHI DRC AFUTWA KAZI

Generali Amisi.
Mkuu wa majeshi  Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, amesimamishwa kazi huku uchunguzi ukiendelea kufuatia madai kuwa aliwauzia silaha makundi ya waasi yanaopambana na serikali ya nchi hiyo.

Ripoti moja ya Umoja wa Mataifa, imemtuhumu, Generali Gabriel Amisi kwa kuendesha mtandao wa kusambaza silaha kwa wawindaji haramu na makundi ya waasi, likiwemo kundi la Mai Mai Raia Mutomboki.

RAIA KUANDAMANA LEO MISRI

Wafuasi wa Rais wa Misri, Mohamed Morsi, wamesisitiza kuwa madaraka makubwa ambayo amejipatia ni ya muda.

Msemaji wa chama chake cha Freedom and Justice ameiambia BBC, kuwa Bwana Morsi amejipatia mamlaka hayo kwa minajili ya kulinda malengo ya mapinduzi yaliyomuondoa madarakani mtangulizi wake Hosni Mubarak.

Makundi ya upinzani nchini Misri, yameitisha maandamanao ya umma hii leo kupinga uamuzi wa rais wa nchi hiyo wa kujiongezea mamlaka kupindukia.

Kadhalika mmoja wa viongozi wa upinzani, Mohamed El Baradei, amemlaumu Moursi kwa kujiteua mwenyewe kuwa Pharao mpya.

Mamlaka hayo yanampa uwezo rais ambapo maamuzi yake hayawezi kubatilishwa na mamlaka yoyote na hata Mahakama kuu zaidi nchini humo.(BBC News)

CWT YALALAMIKIA UCHELEWESHAJI WA MALIPO YA WANACHAMA WAKE






 Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Bw. Gratian Mukoba.(Picha IPP MEDIA)






Na Steven Augustino,
Tunduru.

CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT) Wilayani Tunduru mkoani Ruvuma, kimelalamikia ucheleweshaji wa malipo ya wanachama wake na kudai kuwa hali hiyo inawafanya wanachama hao kuishi katika maisha ya kuwa omba omba.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo jumla ya shilingi 120,423,080 zinazo daiwa na walimu 111  wa wilaya hiyo, yakiwa ni mapunjo yao ya mishahara yaliyolimbikizwa kuanzia mwaka 2009.

Katibu wa chama hicho Bw. Lazaro Saulo alisema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea katika ofisini za CWT wilayani humo, na kuongeza kuwa kutokana na hali hiyo pia walimu wengi katika maeneo mbalimbali hivi sasa wanakabiliwa na madeni makubwa ambayo wamekuwa wakikopa kutoka katika asasi za fedha ili kujikimu kimaisha.

MADEREVA PIKIPIKI TUNDURU WALISHUTUMU JESHI LA POLISI


















Kamanda wa polisi mkoa wa Ruvuma, Bw. Deusdedith Nsemeki.


Na Steven Augustino,
Tunduru.

Madereva wa pikipiki maarufu kwa jina la Boda boda wameaswa kuunganisha nguvu zao na kuisaidia serikali kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kudumisha amani na utulivu.

Pamoja na utekelezaji wa maadhimio hayo pia madereva hao wamehimizwa kuwa na leseni za udereva pamoja na kutumia fursa na asilimali zilizopo katika maeneo yao, ili kujiletea maendeleo.

Mwito huo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya Tunduru Bw. Chande Nalicho alipokuwa akizungumza na Madereva hao katika kikao kilichofanyika ukumbi wa Klasta mjini hapa, na kuongeza kuwa endapo wataendelea kujitenga hawatapata mafanikio huku wakihatarisha hali ya amani ya taifa lao, kwani taarifa zao pia zitasaidia kulinda maisha yao na jamii nyingine kwa ujumla.

Akifafanua taarifa hiyo Bw. Nalicho alisema kuwa ili wapate mafanikio kupitia kazi wanazozifanya wanapaswa kutoa ushirikiano kwa kuwataja wahalifu, ambao ni kati ya wateja ambao kwa namna moja au nyingine huwasafirisha na kuwapeleka katika maeneo ya uhalifu huku wakiwa
wanafahamu au la.

WAKAZI TUNDURU MJINI AFYA ZAO ZIPO HATARINI, WANANCHI WAULALAMIKIA UONGOZI WA WILAYA

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Bw. Said Mwambungu.
















Na Steven Augustino, 
Tunduru.

ABIRIA na Wananchi wanaotumia Kituo kikuu cha mabasi  mjini Tunduru mkoani Ruvuma, wamelalamikia kuendelea kukithiri kwa uchafu katika kituo hicho na kuhofia usalama wa afya zao.

Waandishi wa habari ambao wamezungumza na abiria na baadhi ya wananchi kwa nyakati tofauti, kwa masharti ya kutotajwa majina yao, walisema mbali na kuwepo kwa utaratibu wa halmashauri ya wilaya hiyo, kutoza ushuru wa aina mbalimbali ikiwemo magari yanayoegeshwa katika kituo hicho hali bado ni tete na hakuna juhudi zozote
zinazoonyesha kuzaa matunda katika kukabiliana na suala hilo.

Walisema ushuru ambao hutozwa ni shilingi 1000 kwa kila gari linaloingia na kutoka katika kituo hicho, na magari  yanayoegeshwa ndani ya kituo hicho hutozwa shilingi 1000 kwa kila gari linalo egeshwa hadi asubuhi.

WATENDAJI WA VITONGOJI KATA YA MBINGA MJINI LAWAMANI

















Aliyesimama katika picha ni Mtendaji wa kata ya Mbinga mjini Bw. George Maliyatabu, kulia kwake ni Diwani wa kata hiyo Bw. Kelvin Mapunda na wajumbe wengine. Bw. Maliyatabu alikuwa akiwashutumu na kuwalalamikia watendaji wa vitongoji vilivyopo katika kata hiyo, kwamba wamekuwa ni tatizo katika kuibua miradi mipya ya maendeleo ya wananchi katika maeneo yao ya kazi. Shutuma hizo alizitoa leo mbele ya kikao cha Baraza la maendeleo la kata(WDC) kilichoketi kwenye ukumbi wa Maktaba mjini hapa, na kuwaamuru watendaji hao ifikapo Novemba 24 mwaka huu majira ya asubuhi, wakutane tena katika ukumbi huo na kuanza kupanga upya taratibu za uibuaji wa miradi ya wananchi wa kata hiyo, ili aweze kuwasilisha katika ngazi husika. Miradi hiyo  itakayoibuliwa ni kwa ajili ya mwaka 2013 / 2014.(Picha na Kassian Nyandindi)

Thursday, November 22, 2012

MAPIGANO YAENDELEA GAZA

Mapigano yameendelea usiku kucha katika eneo la Gaza licha ya fununu kuwa kumewekwa mkataba wa kusitisha mashambulio.


Israel inadaiwa kuendeleza mashambulio hayo katika maeneo kadhaa ya Gaza yaliyosababisha kupoteza kwa nguvu za umeme.

Takriban wapalestina ishirini wameripotiwa kuuawa .

AJALI YA GARI

Wakazi wa jiji wakipita kando ya gari Toyota Canter namba T 612 BHY, lililopinduka baada ya kugongana na gari jingine Toyota Canter namba T 529 AAY (halipo pichani). Ajali hiyo ilitokea eneo la Buguruni Barabara ya Mandela, Dar es Salaam jana. (Source Majira newspaper)

Tuesday, November 20, 2012

CHANZO CHA MTO LUHIRA SONGEA CHAPOTEZA MAJI YAKE

















Mshauri wa mtandao wa maji safi katika mamlaka ya maji safi na taka(SOUWASA) manispaa ya Songea mkoani Ruvuma Bw. Waiton Nyadzi, akionyesha chanzo cha mto Luhira jinsi gani kinavyozidi kupoteza maji yake kutokana na kile alichosema ni sababu ya mabadiliko ya tabia nchi shughuli za binadamu zisizo rasmi.(Picha na Kassian Nyandindi)

MITAMBO YA KUSUKUMIA MAJI SONGEA

















Hii ni mitambo ambayo imejengwa karibu na chanzo cha maji cha mto Luhira, mitambo hii hutumika katika shughuli ya kusukuma maji pale linapotokea tatizo la upungufu wa maji katika manispaa hiyo kama ilivyo sasa.(Picha na Kassian Nyandindi)

MAABARA YA KUTIBU MAJI SONGEA

















Mshauri wa mtandao wa maji safi kutoka mamlaka ya maji safi na taka manispaa ya Songea(SOUWASA) Bw. Waiton Nyadzi, akionyesha waandishi wa habari mitambo inayotumika kuchanganyia dawa ambazo hutumika kuyatibu maji ambayo husambazwa kwa watumiaji katika manispaa hiyo. Maabara ya mitambo hiyo imejengwa katika eneo la Matogoro.(Picha na Kassian Nyandindi)

KUCHUJWA MAJI NA KUYATIBU

















Bw. Waiton Nyadzi ambaye ni mshauri wa maji safi manispaa ya songea katika mamlaka ya maji safi na taka(SOUWASA) aliyenyosha mkono pichani, akiwa katika eneo la mtambo wa kuchuja na kutibu maji akiwapa maelezo waandishi wa habari juu ya maji hayo yanavyochujwa na kuyatibu. katikati ni mwandishi wa habari gazeti la Majira Cresencia Kapinga na kushoto ni Bw. Jaffary Yahaya ambaye ni Mhandisi wa mipango na ujenzi katika mamlaka ya maji safi na taka(SOUWASA) manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.(Picha na Kassian Nyandindi)