Sunday, December 9, 2012

NYAMSIKA: ENEO LILE NDILO LITAKALOCHIMBWA URANI

Waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma, wakioneshwa eneo la mto Mkuju ambalo hapo baadaye mara baada ya serikali kutoa kibali cha kuruhusu kuchimba madini hayo, yataanza kuchimbwa. Anayeonesha kwa mkono ni Mjiolojia mkuu wa kampuni ya Mantra Tanzania, Emmanuel Nyamsika. Waandishi hao walifanya ziara hiyo leo ili kujiridhisha juu ya uvumi uliojitokeza kuwa madini hayo yameanza kuchimbwa lakini imebainika kwamba kazi ya uchimbaji bado haijaanza kutokana na serikali bado haijatoa kibali cha kuruhusu kazi hiyo kuanza kufanyika.

No comments: