Thursday, December 20, 2012

KELVIN MAPUNDA: ZINGATIENI ELIMU MNAYOPEWA NA WALIMU WENU

Diwani wa Kata ya Mbinga mjini Kelvin Mapunda(Aliyevaa koti jeusi) akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Mbambi, Mbinga na Nyerere zilizopo katika kata hiyo wakati akiwa katika ziara yake ya kutembelea vituo vya masomo wakati wa likizo vilivyopo katika kata hiyo. Lengo la wanafunzi hao kuwa pamoja katika kituo hicho ni kuwaongezea ujuzi na maarifa katika masomo yao, na huu ni mpango ambao umwekwa na uongozi wa wilaya ya Mbinga, ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi kwa mitihani ya darasa la nne na la saba. Hata hivyo Diwani huyo aliwataka wanafunzi hao kuzingatia masomo yao. Vilevile katika ziara hiyo alitembelea vituo vinne vinavyotumika kufundishia watoto hao katika kata hiyo, ambavyo vipo shule ya msingi Mbinga, Makita sekondari, Lupilisi english medium school na shule ya msingi Mahela.(Picha na Kassian Nyandindi)

No comments: