Friday, November 23, 2012

WATENDAJI WA VITONGOJI KATA YA MBINGA MJINI LAWAMANI

















Aliyesimama katika picha ni Mtendaji wa kata ya Mbinga mjini Bw. George Maliyatabu, kulia kwake ni Diwani wa kata hiyo Bw. Kelvin Mapunda na wajumbe wengine. Bw. Maliyatabu alikuwa akiwashutumu na kuwalalamikia watendaji wa vitongoji vilivyopo katika kata hiyo, kwamba wamekuwa ni tatizo katika kuibua miradi mipya ya maendeleo ya wananchi katika maeneo yao ya kazi. Shutuma hizo alizitoa leo mbele ya kikao cha Baraza la maendeleo la kata(WDC) kilichoketi kwenye ukumbi wa Maktaba mjini hapa, na kuwaamuru watendaji hao ifikapo Novemba 24 mwaka huu majira ya asubuhi, wakutane tena katika ukumbi huo na kuanza kupanga upya taratibu za uibuaji wa miradi ya wananchi wa kata hiyo, ili aweze kuwasilisha katika ngazi husika. Miradi hiyo  itakayoibuliwa ni kwa ajili ya mwaka 2013 / 2014.(Picha na Kassian Nyandindi)

No comments: