Tuesday, November 13, 2012

TUNDURU WATAKIWA KUJIENDELEZA KIELIMU

MKuu wa mkoa wa Ruvuma, Bw. Said Mwambungu.

    






 







Na Dustan Ndunguru,
Tunduru.

VIJANA wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma wametakiwa kutokata tamaa ya maisha badala yake watumie muda wao kujiendeleza kielimu  ikiwemo kujiunga na vyuo vya ufundi ili waweze kupata mafanikio wanayohitaji.

Hayo yalisemwa na mkuu wa wilaya hiyo Bw. Chande Nalicho, wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Chiwana huku akisema, kama kijana atakuwa hajapata nafasi ya kujiendeleza kielimu ajikite katika shughuli za kimaendeleo.

Bw. Nalicho alisema kuwa vijana wengi wamekuwa na tabia ya kukata tama, jambo ambalo sio zuri na kwamba badala yake wanapaswa kubuni njia mbalimbali za kujiletea maendeleo, ikiwa ni pamoja na uanzishwaji wa vikundi vya uzalishaji mali.

“Kutokana na tatizo la ajira lililopo sasa ni muhimu kwa vijana kutumia akili zao wenyewe kutafuta na kubuni njia bora za kufanya, zitakazowasaidia kujipatia mahitaji yao ya kila siku kuliko kusubiri ajira ambazo hawana uhakika nazo, serikali imeweka mazingira mazuri ambayo yatamwezesha kila anayewajibika kwa lolote kufanikisha”, alisema.

Alisema ujinga na maradhi ni  kichocheo kikubwa cha umasikini na kwamba hali hiyo huchangiwa kwa kiasi kikubwa ukosefu wa elimu hivyo wakati umefika kwa wazazi na vijana wenyewe kuanza kubadilika na kutambua umuhimu wa elimu.

Mkuu huyo wa wilaya aliwakumbusha wananchi wa wilaya hiyo kuanza maandalizi ya msimu mpya wa kilimo, kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa, mwaka huu mvua zimewahi kunyesha mapema ikilinganishwa na miaka ya nyuma.

No comments: