Thursday, November 1, 2012

RC MWAMBUNGU MALIZA KERO HII, ITAENDELEA KUDUMU MPAKA LINI ?

  
Pikipiki na magari yakiwa katika foleni ya kwenda kununua mafuta katika sheli za mafuta zilizopo mjini Songea Ruvuma. Foleni hiyo inatokana na wamiliki wa vituo vya kuuzia mafuta mjini humo kutia mgomo wa kukataa kuuza mafuta kutokana na serikali kuwataka wapunguze shilingi 300. Hata hivyo pamoja na mkuu wa mkoa huo Bw. Said Mwambungu kuingilia kati na kutoa amri wamiliki wa vituo vya mafuta mjini Songea kuuza mafuta haraka iwezekanavyo, bado hali ni tete na mgomo umeendelea kuwepo, wananchi wamekuwa wakitaabika na adha hiyo wanayoipata sasa kutokana na kukosa nishati hiyo muhimu.(Na Kassian Nyandindi).

No comments: