Wednesday, November 14, 2012

UZOAJI WA TAKA KATIKA MAGHUBA MBINGA UWE ENDELEVU


Katapila la halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, likifanya kazi ya kuchimbua taka katika moja kati ya ghuba la kuhifadhia taka lililopo Mbinga mjini. Uzoaji huo wa taka umeanza kutekelezwa kwa kasi tofauti na hapo awali na hili limetokana na wakazi wa mji huo kulalamika kwa kipindi kirefu kwamba maghuba mengi ya kuhifadhia taka yaliyopo mjini humo, kufurika taka na kukaa muda mrefu bila kuzolewa. (Picha na Kassian Nyandindi).



CHANGAMOTO:

ZOEZI la uzoaji wa taka Mbinga mjini ni jambo la busara ambalo tungependa kuliona linakuwa endelevu.

Jicho letu limeshuhudia changamoto iliyopo sasa ni kwamba wazoaji wanaofanya kazi hiyo wamekuwa wakizoa taka, bila kupewa vifaa kama vile "Gloves" utakuta wanazoa taka bila vifaa hivyo muhimu.

Ni vyema sasa uongozi husika ukachukua jukumu la kuwapa vifaa muhimu ambavyo vitakinga afya zao, zisiweze kushambuliwa na wadudu watokanao na uchafu.


Tunatambua kwamba mji wa Mbinga una mamlaka ya mji mdogo ambayo ina viongozi wa sekta mbalimbali, ikiwemo hii ya afya. 

Tunachohitaji hapa ni kuona Bwana afya wa mamlaka hiyo anatekeleza majukumu yake ya kazi alizopewa, ikiwemo hili la kusimamia kazi ya kugawa vifaa vya kufanyia kazi ya uzoaji taka kwa wafanyakazi waliopewa jukumu la kufanya kazi hiyo.


No comments: