Friday, November 9, 2012

WAASI WADUNGUA NDEGE YA KHARTOUM







Mapigano Kordofan Kusini.






Mapigano Kordofan Kusini:

Waasi katika jimbo la Kordofan Kusini, nchini Sudan wanasema kuwa wamedungua ndege ya kijeshi karibu na mpaka wake na Sudan Kusini.

Msemaji wa kundi la SPLM-North amesema kuwa ndege hiyo ilidunguliwa kufuatia ufyatuaji mkubwa wa risasi, katika eneo la milima ya Nuba siku ya Jumatano.

Hakuna tamko lolote kutoka kwa serikali ya Khartoum kuhusu shambulizi hilo.

Waasi wamekuwa wakipigana dhidi ya serikali ya Sudan katika eneo hilo tangu Juni mwaka jana.

Mzozo huu wa Kordofan Kusini pamoja na Ule wa jimbo la Blue Nile umewafanya maelfu ya watu kutoroka makwao. (BBC News)

No comments: