Monday, February 19, 2018

VIONGOZI WAANDAMIZI CHADEMA WATAKIWA POLISI



Na Mwandishi wetu,

VIONGOZI Waandamizi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wameitwa na Jeshi la Polisi wakitakiwa kwenda kuripoti leo jioni Februari 19 mwaka huu.

John Mrema ambaye ni kiongozi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje kwa chama hicho alithibitisha hilo kwamba wameitwa kwa barua hiyo ambayo wameipokea makao makuu ya chama majira ya saa kumi jioni.

Ambapo barua hiyo inawataka kwenda kuripoti kwa Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum Dar es Salaam katika Ofisi yake.


Mrema alifafanua kuwa viongozi hao waliotakiwa kwenda kuripoti huko wameshindwa kufika kituo cha Polisi, kwa kile alichodai kucheleweshwa kwa barua hiyo kwani imewafikia saa kumi na dakika 51 na ikisema viongozi hao wafike saa kumi na moja jambo ambalo limeshindikana kutokana na ukweli kwamba viongozi hao wanaishi katika maeneo mbalimbali hivyo isingewezekana kuwapata wote ndani ya dakika tisa.

“Cha ajabu walikuwa wanawataka viongozi hawa saa kumi na moja kamili jioni hivyo kulikuwa na dakika tisa tu wakati viongozi wanaowataka ni wengi na wamesambaa maeneo mbalimbali, 

“Hivyo wanasheria wetu wanashughulika kuwajulisha Jeshi la Polisi juu ya hilo kwa sababu kama Mbunge John Heche ni Mbunge wa Tarime, Esther Matiko na Mbunge wa Tarime hawa watu wamesambaa sasa huwezi kuleta barua Makao makuu halafu utegemee kuwapata saa kumi na moja jioni,

“Yaani dakika tisa wawe wamewasili Polisi, hivyo Mawakili wetu watawajulisha Polisi, na wale watakaopatikana na kuwajuza wataripoti saa ngapi”, alisema Mrema.

No comments: