Thursday, April 9, 2015

BENKI YA NMB YATOA MAFUNZO KWA WADAU WA KAHAWA MBINGA

Upande wa kushoto, Mkuu wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Senyi Ngaga akikaribishwa leo katika ukumbi wa Jimbo Katoliki uliopo mjini hapa na Meneja wa benki ya NMB tawi la Mbinga Lugano Mwampeta, kwa ajili ya kufanya ufunguzi wa semina ya siku moja kwa wadau wa kahawa wa wilaya hiyo. Anayeshuhudia tukio hilo ni Meneja wa benki hiyo tawi la Litembo wilayani Mbinga, Victor Msoffe.

Meneja wa NMB Kanda ya kusini Lillian Mwinula, akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Mbinga Mashariki mkoani Ruvuma, Gaudence Kayombo ambaye alikuja kushiriki katika semina ya Wadau wa kahawa inayofanyika leo kwenye ukumbi wa Jimbo Katoliki mjini hapa. Kwa ujumla semina hiyo inaendeshwa na benki hiyo kwa manufaa ya kumuinua mkulima kiuchumi ili aweze kuondokana na umasikini. 

No comments: