Monday, November 18, 2013

WAANDISHI WA HABARI WANOLEWA MJINI DODOMA, WASISITIZWA KUZINGATIA MAADILI YA KAZI ZAO

Mratibu wa mafunzo ya kuandika habari na kuziweka kwenye mtandao Japhet Sanga (kushoto) kutoka TMF, akisisitiza jambo wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari ambao wanashiriki mafunzo hayo ya siku tano mjini Dodoma.

Mwandishi wa habari Franci's Godwin (aliyesimama) kutoka mkoani Iringa, akichangia hoja katika mafunzo ya siku tano ya uandishi bora wa habari na kuziweka kwenye mitandao, yanayoendelea kufanyika mjini Dodoma. (Picha zote na Kassian Nyandindi)

Na Kassian Nyandindi,
Aliyekuwa Dodoma.

WAANDISHI wa habari nchini wamesisitizwa kuendelea kuzingatia misingi ya taaluma yao, ili kuweza kulinda heshima katika tasnia ya habari na taifa kwa ujumla.


Wito huo ulitolewa leo na Mratibu wa mafunzo ya habari za mitandao(Online Journalism) Japhet Sanga, kutoka shirika la Tanzania Media Fund (TMF) Jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na baadhi ya Waandishi wa habari mjini Dodoma.


Sanga alikuwa akizungumza na Waandishi hao, ambao wanashiriki mafunzo ya siku tano ya uandishi bora wa habari za uchunguzi na kuziweka mitandaoni, yanayofanyika kwenye ukumbi wa New Dodoma hotel uliopo mjini hapa.


Waandishi hao ni wale ambao wanashughulika katika majukumu ya kazi zao za kila siku, katika kuandika habari na kuziweka kwenye mitandao yao.


“We want to have Quality blogger's…………… tunahitaji mtu ambaye anazingatia maadili ya vyombo vya habari, hatuhitaji mtu anayeandika vitu vyenye kulenga uchochezi”, alisema.



Naye Mkufunzi mkuu wa mafunzo hayo Beda Msimbe alisema, katika zama hizi Waandishi wengi wamekuwa wakizembea kuzingatia maadili ya kazi zao, na hivyo kujikuta jamii kukosa imani nao.  

No comments: