![]() |
| Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. |
Na Mwandishi wetu,
Tarime.
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira kusitisha uuzwaji wa mali za Chama
cha Ushirika cha Kilimanjaro (KNCU).
Majaliwa alitoa agizo hilo jana wakati
alipokuwa akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara, uliofanyika kwenye
uwanja wa Serengeti Wilayani Tarime Mkoani hapa.
Hatua hiyo imekuja baada ya KNCU
kutangaza kuuza shamba lake kwa ajili ya kuiwezesha benki yake ya KCBL kutimiza
sharti la mtaji la Benki Kuu ya Tanzania (BOT).























