Monday, January 6, 2014

WAKAZI WA MBINGA MJINI WASHAURIWA KUTOA MSAADA KWA WAGONJWA

Mganga wa zamu wodi ya watoto (kulia) katika hospitali ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma,  Revina Kayombo akipokea msaada wa sabuni za kufulia wagonjwa, kutoka kwa Philiberth Hyera (aliyevaa suti nyeusi ambaye amekaa) mkazi wa Mbinga mjini. Hyera alitoa wito kwa wakazi wengine waliopo mjini hapa kupenda kuwasaidia wagonjwa.

Aliyevaa suti nyeusi ni Philiberth Hyera mkazi wa Mbinga mjini akitoa msaada wa sabuni za kufulia, kwa wagonjwa ambao wamelazwa katika wodi ya akina mama hospitali ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, hivi karibuni. (Picha zote na Kassian Nyandindi)

No comments: