Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.
MENEJA Mahusiano wa benki ya CRDB Kanda ya Nyanda za juu
kusini, Hassanaly Japhary amesema kuwa ameshangazwa na kauli ya Wajumbe wa bodi
ya Chama cha ushirika Mbinga Kurugenzi SACCOS, kwamba hawazitambui baadhi ya
nyaraka za benki hiyo ambazo zilitumika kuwapatia mkopo wa shilingi milioni 500
kwa ajili ya kuwakopesha wanachama wa ushirika
Alifafanua kuwa kauli hiyo ya kushangaza ilitolewa na Wajumbe hao katika mkutano wao maalumu uliofanyika mjini hapa na kwamba benki hiyo, haipo tayari kuchafuka kwa mambo hayo badala yake itafungua mashtaka dhidi ya matumizi mabaya ya fedha za mkopo huo, yaliyofanywa na Wajumbe hao kwa kujinufaisha wao binafsi badala ya kuwakopesha wanachama wa SACCOS hiyo.
Alifafanua kuwa kauli hiyo ya kushangaza ilitolewa na Wajumbe hao katika mkutano wao maalumu uliofanyika mjini hapa na kwamba benki hiyo, haipo tayari kuchafuka kwa mambo hayo badala yake itafungua mashtaka dhidi ya matumizi mabaya ya fedha za mkopo huo, yaliyofanywa na Wajumbe hao kwa kujinufaisha wao binafsi badala ya kuwakopesha wanachama wa SACCOS hiyo.
Hassanaly alisema hayo juzi alipokuwa akihojiwa na waandishi
wa habari mara baada ya kusomwa taarifa ya ukaguzi juu ya mwenendo wa Chama
hicho cha ushirika ambayo ilibainisha wizi wa fedha zilizotokana na mkopo huo shilingi milioni 405,204,514 katika
mkutano mkuu maalumu wa wanachama, uliofanyika kwenye ukumbi wa Jumba la
maendeleo mjini hapa.
“Benki hatupo tayari kuchafuka kwa mambo haya, sisi kama
benki nasi tutahakikisha tunafungua mashtaka mahakamani dhidi ya wizi huu
uliofanyika hapa Mbinga katika SACCOS hii ili tuweze kurejesha fedha zetu”,
alisisitiza Hassanaly.








