Na Mwandishi wetu,
Namtumbo.
MWITO umetolewa kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari
wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma, kuongeza juhudi katika masomo yao na
kujiepusha kushiriki vitendo viovu vinavyoweza kukatisha ndoto yao ya kujiendeleza
kimasomo kama vile kwa wanafunzi wa kike kupata mimba wakati wakiwa na umri
mdogo, au virusi vya Ukimwi.
Aidha wametakiwa kuwa na dhamira ya kweli juu ya kusukuma
maendeleo ndani ya wilaya yao, ili watakapohitimu masomo yao na kupata ajira
warudi kwenye maeneo yao kuwatumikia wananchi na sio kwenda kufanya kazi katika
mikoa au wilaya zingine ambako tayari wamepiga hatua kimaendeleo.
Imeelezwa kuwa kufanya hivyo kutasaidia kupunguza tatizo la
watumishi, hasa kwa idara ya afya, elimu na kilimo ambako mahitaji ya watumishi
wake ni makubwa.
















