Na Mwandishi wetu,
NIMECHUKUA jukumu la kuvishauri vyama vya wafanyakazi pamoja
na shirikisho la wafanyakazi hapa nchini, kutokana na hali halisi ya utatanishi
kati ya waajiri na wafanyakazi katika mahusiano yao. Mahusiano hasi kati ya
mwajiri na mwajiriwa yamekuwa nikawaida katika mazingira ya kazi hapa nchini.
Binafsi naamini vyama vya wafanyakazi ni kiungo kati ya
waajiri na wafanyakazi hivyo kuwa daraja katika kushughulikia kero, changamoto
au matatizo mbalimbali kati ya mwajiri na mfanyakazi, pia hushughulikia kutoa
msaada wa kisheria kwa inapobidi.
Licha ya hapa kwetu Tanzania, kuwa na vyama vya wafanyakazi
pamoja na juhudi mbalimbali za vyama hivyo bado kumekuwa na changamoto nyingi
zinazowakabili wafanyakazi.
Hivyo upo umuhimu wa vyama hivyo kushirikiana na taasisi
binafsi kutoa msaada wa kisheria pamoja na elimu kwa wafanyakazi, ili kuondoa
hali ya manyanyaso, ukiritimba na urasimu unaofanywa na waajiri kazini.