Sunday, February 1, 2015

PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI KATIKA MAADHIMISHO YA SHEREHE ZA CCM SONGEA MKOANI RUVUMA

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Jakaya Kikwete, akilakiwa na maelfu ya wananchi wakati akiingia katika uwanja wa Majimaji mjini Songea mkoani Ruvuma, leo kuongoza kilele cha sherehe za kuadhimisha miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akilakiwa na Katibu mkuu wa umoja wa vijana Taifa (UVCCM) Sixtus Mapunda, na viongozi mbalimbali wa chama hicho wakati akiingia katika uwanja wa Majimaji mjini Songea, leo kuongoza kilele cha sherehe za kuadhimisha miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM.

  Rais Jakaya Kikwete, akikagua gwaride la heshima lililoandaliwa na UVCCM katika uwanja wa Majimaji mjini Songea leo, katika kilele cha sherehe za kuadhimisha miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM.

  Rais, Jakaya Kikwete akiwa pamoja na viongozi wengine wa CCM wakipokea gwaride la heshima lililoandaliwa na UVCCM, katika uwanja wa Majimaji mjini Songea leo katika kilele cha sherehe za kuadhimisha miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM.
Gwaride la lililoandaliwa na UVCCM likitoa heshima kwa viongozi katika uwanja wa Majimaji mjini Songea leo, wakati wa kilele cha sherehe za kuadhimisha miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM.
Mwenyekiti wa Chama tawala CCM, Rais Jakaya Kikwete akihutubia maelfu ya wananchi kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea, leo katika kilele cha sherehe za kuadhimisha miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM.
Msanii Diamond Platinum, akipongezwa na chipukizi wa UVCCM baada ya kutumbuiza katika uwanja wa Majimaji mjini Songea, leo katika kilele cha sherehe za kuadhimisha miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM.
  Rais Jakaya Kikwete, akipokea wanachama wapya akiwa na Mbunge wa Songea mjini Dokta Emmanuel Nchimbi na Katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, katika uwanja wa Majimaji mjini Songea leo, kwenye kilele cha sherehe za maadhimisho miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM. (Picha na Ikulu)

No comments: