Monday, February 9, 2015

WAFANYABIASHARA RUVUMA KUKAA NA WABUNGE WAO



Na Mwandishi wetu,
Songea.

WAFANYABIASHARA waliopo katika Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma  wamewataka wabunge wa mkoa huo, warudi kwenye majimbo yao ili waweze kujadili changamoto inayowakabili wafanyabiashara hao, juu ya ongezeko la kodi mara mbili na kiwango kilichokuwa kikitozwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania. (TRA)

Akizungumza katika mkutano  uliyofanyika kwenye ukumbi wa Songea Club uliopo mjini hapa, Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao, Isaya Mbilinyi alisema kuwa  ongezeko hilo limefikia asilimia 100 jambo ambalo, linalowafanya wafanyabishara wengi kushindwa kumudu gharama ya ulipaji wa kodi.

Mbilinyi alisema kuwa kutokana na Bunge kupitisha kiwango hicho cha ulipaji kodi, ni vyema wabunge wa majimbo ya mkoa wa Ruvuma warudi  na kukaa pamoja na wafanyabiashara  hao ili waweze kujadili na kutambua changamoto hiyo ambayo inawakabili.


 “Tuanawaomba wabunge wetu tukae pamoja kujadili suala hili, kabla bunge halijapitisha kuwa sheria ambalo kwa sasa bado limekuwa kwenye mswada kwa kuwa wafanyabiashara  tulio wengi, vipato vyetu ni vya chini ambavyo haviwezi kumudu ongezeko hilo la kodi hiyo,

“Wafanyabiashara wenzangu suala hili lisiwe la ugomvi, kinachotakiwa tuendelee kupaza sauti kwa kufuata taratibu zinazotakiwa ili mwisho wa siku serikali iweze kutusikiliza, ndio maana tunaanza na wabunge wetu ambao ni wawakilishi wetu,” alisema Mbilinyi.

Kwa upande wake Meneja wa TRA mkoa wa Ruvuma, Apili Mbaruku alisema ofisi yake haina uwezo wa kutengua mambo yaliyoopitishwa na bunge, bali bunge hilo ndilo lenye nafasi ya kuweza kujadili na kuamua maamuzi mengine.

No comments: