Tuesday, August 13, 2013

ANYOFOLEWA SEHEMU ZA SIRI NA MKEWE KUTOKANA NA KUTOHUDUMIA FAMILIA YAKE



Na Steven Augustino,
Tunduru.

MKAZI mmoja wa kijiji cha Mchuluka wilayani Tunduru mkoa wa Ruvma, Abdalah Njuga (23) amelazimika kutoa talaka kwa mkewe baada ya kumtuhumu kumjeruhi kwa kumvuta sehemu zake za siri, na kumsababishia maumivu makali.

Kufuatia hali hiyo Njuga alichukua hatua hiyo ya kuachana nae kwa madai kwamba, maamuzi hayo yametokana na hofu ya kuendelea kupata madhara zaidi.  

Akizungumza kwa taabu, Njuga ambaye amelazwa katika hospitali ya wilaya yaTunduru, alisema chanzo cha tukio hilo, kimetokana na mkewe kumtuhumu kushindwa kumhudumia yeye pamoja na watoto wake, kwa kuwapatia mahitaji muhimu ya maisha yao ya kila siku.
  
Akifafanua taarifa hiyo Njuga alisema kuwa katika tukio hilo mkewe huyo ambaye alimtaja kwa jina la Sauda Njuga, alisema kuwa pamoja na kumvuta nyeti hizo, pia alimpiga kwa kutumia mti na kumuuma meno sehemu mbalimbali za mwili wake.

Alisema ugomvi huo ulianza usiku wa manane wakati mkewe ghafla alipoanza kucharuka na kuanza kumshambulia mwilini, na baadaye kumvuta sehemu zake za siri ambapo baada ya tukio hilo ndipo alikimbizwa katika zahanati ya kijiji cha Mchuluka, kwa ajili ya kupatiwa matibabu ya huduma ya kwanza.

Mganga mfawidhi wa hospitali hiyo Dokta Joseph Ng’ombo alisema kuwa hali ya majeruhi huyo inaendelea vizuri, baada ya kupatiwa matibabu.

Alisema katika tukio hilo majeruhi huyo aliumizwa vibaya sehemu zake
za siri, pamoja na kupata majeraha makubwa mwilini mwake.

No comments: