Tuesday, August 20, 2013

BREAKING NEWS: WATU WAWILI WAFARIKI DUNIA NA WENGINE 40 WAJERUHIWA VIBAYA KUTOKANA NA AJALI YA GARI


Baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo Rahabu Nziku kushoto, na mwenzake Joseph Kapinga wakiwa wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Mbinga wakiendelea kupatiwa matibabu. (Picha na Kassian Nyandindi)

Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.


WATU wawili wamefariki dunia na wengine 40 wamejeruhiwa vibaya, kufuatia ajali iliyotokea usiku wa kuamikia leo katika milima ya Burma wilayani Nyasa mkoa wa Ruvuma.

Tukio hilo limetokea Agosti 19 mwaka huu majira ya saa 3 usiku na kwamba, baadhi ya majeruhi wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Mbinga.

Aidha majeruhi wengine ambao hali zao ni mbaya, taratibu za kuwasafirisha kuwapeleka hospitali ya Peramiho iliyopo Songea mkoani humo zinafanywa.

Pamoja na mambo mengine taratibu za kutambua miili ya marehemu hao zinafanywa, hivyo ndugu wasomaji wa mtandao huu tutaendelea kuwajuza hapo baadaye.

Gari lililopata ajali ni aina ya fuso lenye namba za usajili T. 807 AVH ambalo lilikuwa likiendeshwa na Lehani Mohamed Makunganya.

Kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika vya habari, vimedai kuwa ajali hiyo ilitokana na gari hilo, kuwa katika mwendo kasi na kupakia mizigo mingi ya nguo ambazo zilikuwa zikipelekwa Mbamba bay wilayani Nyasa, kwa ajili ya kwenda kufanya biashara ya kupiga mnada.


No comments: