Saturday, August 3, 2013

MKWANDA SUDI AENDELEA KUPETA TUNDURU, ASHINDA KWA KISHINDO

Mbunge wa Tunduru Kaskazini Mhandisi Ramo Makani, akizungumza baada ya katibu wa uchaguzi huo Roberth Nehatta kumaliza kutangaza matokeo ya uchaguzi wa Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru, ambapo alisisitiza madiwani wajenge ushirikiano katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Baadhi ya madiwani wa Tunduru wakifuatilia kwa makini taratibu za uchaguzi huo, ambao ulifanyika kwenye ukumbi wa Klasta ya walimu Tunduru mjini. (Picha zote na Steven Augustino)



Na Steven Augustino,
Tunduru.

MADIWANI wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma wamemchagua kwa mara ya pili, Diwani wa Kata ya Mchoteka wilayani humo, Mkwanda Sudi kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) kuwa makamu wa Mwenyekiti wa halmashauri hiyo.

Diwani huyo aliweza kupata kura za ushindi 42 ambazo ni za ndiyo baada ya diwani mwenzake Rashid Omary, kujitoa katika kinyang’anyiro hicho.

Matokeo hayo yalitokana na  mgombea wa nafasi hiyo, ambaye ni wa kutoka chama cha upinzani, kupitia tiketi ya Chama cha Wananchi CUF alijiondoa kwa hiari yake.

Akitangaza matokeo hayo Katibu wa uchaguzi huo, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya Tunduru, Albart Nehatta alisema kuwa idadi ya wapiga kura ilikuwa 48, ambapo kura zilizoharibika zilikuwa 2, kura za hapana 4 na kura za ndiyo zilikuwa 42 ambazo zilimfanya mgombe huyo wa CCM apate ushindi.


Akitangaza matokeo ya kamati ya elimu ambayo wapiga kura walikuwa 16, kamati hiyo ilimchagua Diwani wa Kata ya Mbati Burhan Nakanje aliyepata kura 9 na kumshinda Diwani wa Kata ya Nandembo Bi. Idaya Lweso aliyepata kura 7 .
Nehatta alieleza kuwa upande wa kamati ya uchumi, ujenzi na mazingira wao walimchagua Diwani wa Kata ya Majengo Athuman Nkinde kwa kura 6 baada Diwani Fadhili Mshamu aliyepata kura 3, Anita Komba kura  5 na kura 2 ziliharibika.
Upande wa kamati ya maadili katika halmashauri ya Wilaya hiyo wajumbe hao walimchagua Diwani wa Kata ya Kidodoma Seifu Yusuph  ambaye alipita bila kupingwa.

No comments: