Wednesday, August 14, 2013

WAANDISHI WA HABARI MKOANI RUVUMA WAPATIWA MAFUNZO JUU YA MATUMIZI BORA YA INTANETI


Mwezeshaji wa mafunzo ya Intaneti Simon Berege kutoka mkoani Iringa (aliyesimama) akitoa maelezo kwa waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma juu ya matumizi ya kisasa ya tekinolojia ya habari kwa kutumia Intaneti. Waandishi wa habari wapo katika mafunzo ya siku tatu wakishiriki mafunzo hayo ambayo yanafanyika kwenye ukumbi wa VETA mjini Songea.

Waandishi wa habari mkoani Ruvuma wakiendelea na mfunzo hayo katika ukumbi wa VETA mjini Songea.

Mwezeshaji Simon Berege akisisitiza jambo juu ya matumizi ya Intaneti kwa Waandishi wa habari(hawapo pichani) wa mkoa wa Ruvuma.


Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari mkoani Ruvuma, Juma Nyumayo naye akishiriki katika kazi ya kutoa maelekezo juu ya matumizi ya Intaneti.

Mwandishi wa habari Kassian Nyandindi anayeandikia magazeti ya Businesstimes LTD na Joyce Joliga wa gazeti la Mwananchi, nao wakiwa makini katika kushiriki mafunzo hayo.

Mwezeshaji Simon Berege upande wa kulia, akizungumza na Juma Nyumayo aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari mkoani Ruvuma.

Waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma, wakiendelea na mafunzo ya Intaneti mjini Songea, lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo waandishi wa mikoani katika utendaji wa kazi zao kwa kutumia Intaneti.(Picha zote na Kassian Nyandindi)

No comments: