Wednesday, August 14, 2013

TUJIKUMBUSHE YALIYOJIRI SIKU YA KILELE CHA SHEREHE ZA NANENANE WILAYANI MBINGA

Vallence Ndendya, mkazi wa Mbinga mjini akiangalia mbogamboga na matunda siku ya maadhimisho ya kilele cha sherehe za Nanenane wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma. Anayeshuhudia upande wa kulia ni mkulima Kandidus Komba mkazi wa kitongoji cha Masasi.

Kandida Lyambila, mtaalamu wa kutengeneza vyungu vya udongo kutoka kikundi cha Mbalawala Women Organisation kilichopo kata ya Ruanda wilayani Mbinga, akionyesha utalaamu wake siku ya maadhimisho ya sherehe hizo Mbinga mjini.

Meneja mkuu wa kikundi cha Mbalawala Women Organisation, Leah Kayombo akitoa maelezo mafupi kwa mgeni rasmi Katibu tawala wa wilaya ya Mbinga, Idd Mponda aliyevaa suti nyeusi juu ya utengenezaji wa vitu mbalimbali vya asili siku ya kilele cha sherehe za nane nane zilizoazimishwa wilayani Mbinga, mtaa wa Lusaka Mbinga mjini.

Mama Kayombo akiendelea kutoa maelezo ya utengenezaji wa vyungu, kwa wageni waliotembelea banda la kikundi cha Mbalawala Women Organisation.

Meneja mkuu wa Mbalawa Women Organisation, Leah Kayombo akitoa maelezo juu ya utengenezaji wa mkaa wa mawe kwa mgeni rasmi Katibu tawala wa wilaya ya Mbinga Idd Mponda aliyevaa suti nyeusi. Mkaa huo ukisha tengenezwa hutumika pia katika shughuli za kupikia nyumbani.

Katibu tawala wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Idd Mponda aliyeinama amevaa suti nyeusi, akiangalia majiko yaliyotengenezwa na kikundi cha Mbalawala Women Organisation.

Pia maua ya asili nayo hutengenezwa na Mbalawala Women Organisation, kushoto Mama Kayombo akitoa maelezo namna yanavyotengenezwa.

Banda la Maliasili na Mazingira nalo halikuwa mbali katika maonesho hayo.


Katibu tawala wa wilaya ya Mbinga Idd Mponda, akitia sahihi katika kitabu cha wageni, kwenye banda la maonyesho la kikundi cha Mbalawala Women Organisation, kilichopo katika kata ya Ruanda wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma.


Banda la maliasili na mazingira Mbinga, nalo likiendelea na maonyesho.

Katibu tawala wilayani Mbinga Idd Mponda (aliyevaa suti nyeusi) akipewa maelezo juu ya uzalishaji wa miche ya miti unavyofanywa. (Picha zote na Kassian Nyandindi)

No comments: