Wednesday, July 24, 2013

RODNEY NDUNGURU, SHUJAA ALIYEFIA DARFUR AZIKWA KWAO SONGEA MKOANI RUVUMA


 Asikari wa JWTZ, wakiwa wamebeba mwili wa Rodney Ndunguru.
 
Aliyekaa katikati ni mama wa marehemu Rodney Ndunguru.
 
 Askari wakiwa wamebeba mwili wa marehemu Rodney Ndunguru, wakati wakielekea  katika makaburi ya Mjimwema mjini Songea.
 
 Umati wa watu uliojitokeza katika mazishi ya Rodney Ndunguru katika makaburi ya  mjimwema jana.
 
 
 Mwili wa Rodney Ndunguru ukiingizwa katika kaburi.
 
 Mama wa marehemu Rodney Ndunguru akiweka taji katika kaburi la mwanaye.
 
 
Na Mwandishi wetu,
Songea.


SIMANZI, vilio na majonzi  vimetawala wakati wa mazishi ya askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Rodney Ndunguru wa kikosi cha makomando cha 92 KJ Ngerengere mkoani Morogoro, ambapo mamia ya wakazi wa mkoa wa Ruvuma, wakiwemo askari wa Jeshi la wananchi ambao walihudhuria mazishi hayo yaliyofanyika jana kwenye makaburi ya Mjimwema Manispaa ya Songea.

Katika mazishi hayo ambayo yaliongozwa na Paroko wa kanisa katoliki jimbo kuu la Songea parokia ya Mjimwema padre Noel Duwe, ambaye wakati  akiendesha ibada ya mazishi aliwaonya Watanzania kutochezea amani  na kwamba utulivu walionao watanzania unahitajika kulindwa kwa namna ya aina yeyote na sio vinginevyo.

Padre Due alisema kuwa kwa wale wote wanaotaka kuchezea amani na utulivu tulionao sasa, wanapaswa kukemewa kwa nguvu zote kwa kuwa watanzania hatujazoea vurugu wala umwagaji wa damu jambo ambalo lilionekana kuvuta hisia kwa watu waliofika kuomboleza msiba huo.

Aidha Padri Due alimfagilia Waziri mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda kwa kauli yake aliyoitoa Bungeni kuwa jeshi la Polisi lihakikishe linawadhibiti watu wanaoleta fujo kwa kupiga na kwamba kauli yenye agizo hilo inapaswa kuungwa mkono kwa nguvu zote, badala ya kuibeza kwa kuwa hivi sasa watu wengi wamekuwa wakidharau vyombo vya Dola  wakidhani kwamba serikali haipo.
 
Kwa upande wake  Kaimu wa Brigedi ya kanda ya Kusini Kanarli George Msongole alieleza kuwa taarifa ya kifo cha Rodney, ilipokelewa muda mfupi baada ya kifo chake na kuwa Jeshi la wananachi linaungana  na familia ya marehemu katika majonzi na msiba huo mzito.

Kwa upande wake msemaji wa familia ya Marehemu Rodney Ndunguru alisema kuwa  familia imepata pengo kubwa kwa kuondokewa na kijana wao ,na ameiomba serikali kuangalia uwezekano wa kuisaidia  ili waweze kujengewa nyumba ambayo itwasaidia kwa kuishi mama yake mzazi na mjane.
 
Alisema kuwa Rodney Ndunguru amefariki akiwa na miaka takribani miaka saba kazini na akiwa na umri wa miaka 28 ambapo kimsingi kifo chake kimeacha pengo kubwa katika famila kwani katika uhai wake ilikuwa farja kwa ndugu na jamaa.
 
Rodney Ndungu amezikwa saa 10:45 jioni kwenye makaburi ya Mjimwema ambako mamia ya wakazi ya mkoa wa Ruvuma, walihudhulia akiwemo mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu ambaye ni Katibu tawala wilaya ya songea Joseph Kapinga na kwamba mazishi yaliendeshwa kijeshi ambapo askari wote walikuwa wamevaa sare huku wakifunga vitambaa vyeusi kwenye mikono yao. 
(habari kwa hisani ya demashonews.blogspot.com)
 

No comments: