Hii ndio adha iliyopo katika barabara ya kwenda Tunduru mkoani Ruvuma, serikali mmeliona hili, kama tumeliona sasa kilio cha wananchi hawa kifanyiwe kazi haraka ni miaka mingi sasa imepita hali bado ni tete hasa katika kipindi cha masika.(Picha na Steven Augustino)
Na Steven Augustino,
Tunduru.
VYOMBO vya habari nchini vimehimizwa kufuatilia na kuandika habari za maendeleo, changamoto na matatizo yote yanayowasumbua wananchi waishio vijijini hususani pembezoni mwa wilaya husika.
VYOMBO vya habari nchini vimehimizwa kufuatilia na kuandika habari za maendeleo, changamoto na matatizo yote yanayowasumbua wananchi waishio vijijini hususani pembezoni mwa wilaya husika.
Hayo yalisemwa na mkuu wa Wilaya ya Tunduru Bw. Chande Nalicho wakati akitoa taarifa ya utekeelezaji wa Serikali ya awamu ya nne kupitia
Ilani ya uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) ya mwaka 2005 na 2012.
Ilani ya uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) ya mwaka 2005 na 2012.
Aidha katika taarifa hiyo Nalicho alidai kuwa endapo daraja hili la vyombo vya habari na wanahabari nkwa ujumla, endapo hawatatembelea huko na kuandika taarifa hizo watakuwa hawawatendei haki wananchi wa maeneo hayo hali ambayo itawafanya waendelee kulishwa taarifa za kupendelea wakati wote na kuwatetea viongozi ambao wapo maofisini.