Monday, January 14, 2013

WILAYA YA TUNDURU YATOA TAARIFA YA UTEKELEZAJI SERIKALI YA CHAMA CHA MAPINDUZI

  
Hii ndio adha iliyopo katika barabara ya kwenda Tunduru mkoani Ruvuma, serikali mmeliona hili, kama tumeliona sasa kilio cha wananchi hawa kifanyiwe kazi haraka ni miaka mingi sasa imepita hali bado ni tete hasa katika kipindi cha masika.(Picha na Steven Augustino)





Na Steven Augustino, 
Tunduru.
 
VYOMBO vya habari nchini vimehimizwa kufuatilia na kuandika habari za maendeleo, changamoto na matatizo yote yanayowasumbua wananchi waishio vijijini hususani pembezoni mwa wilaya husika. 

Hayo yalisemwa na mkuu wa Wilaya ya Tunduru Bw. Chande Nalicho wakati akitoa taarifa ya utekeelezaji wa Serikali ya awamu ya nne kupitia
Ilani ya uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) ya mwaka 2005 na 2012.

Aidha katika taarifa hiyo Nalicho alidai kuwa endapo daraja hili la vyombo vya habari na wanahabari nkwa ujumla, endapo hawatatembelea huko na kuandika taarifa hizo watakuwa hawawatendei haki wananchi wa maeneo hayo hali ambayo itawafanya waendelee kulishwa taarifa za kupendelea wakati wote na kuwatetea viongozi ambao wapo maofisini.

TUNDURU NA UTEKELEZAJI WA CHANJO YA KUZUIA MAGONJWA VICHOMI NA KUHARA


Na Steven Augustino, 
Tunduru.

WILAYA ya Tunduru mkoani Ruvuma imeanza kutekeleza mpango wa kuwapatia chanjo mpya ya kuzuia ugonjwa vichomi na kuharisha kwa kuwapatia chanjo hiyo jumla ya watoto 12,372 walio chini ya umri wa mwaka mmoja ikiwa ni juhudi ya serikali kupambana na vifo vitokanavyo na magonjwa hayo.

Mkuu wa wilaya ya Tunduru Chande Nalicho alisema hayo alipokuwa akizundua chanjo hizo katika ukumbi wa kutolea huduma ya mama na mtoto   hospitali ya serikali ya wilaya hiyo iliyopo mjini hapa.
 
Katika hilo Nalicho aliwahimiza wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao bila kukosa, ili wapatiwe chanjo hizo zikiwa ni juhudi za mapambano dhidi ya magonjwa hayo.

Alisema endapo kutatokea wazazi na walezi kuzembea katika kuzingatia kupeleka watoto wao kupatiwa chanjo ya magonjwa hayo kunaweza kusababisha vifo vingi visivyo vya lazima.


Sunday, January 13, 2013

NAIBU WAZIRI WA MAJI AKIBADILISHANA MAWAZO NA MKUU WA MKOA WA RUVUMA MARA BAADA YA KUMALIZA ZIARA YAKE YA SIKU TANO MKOANI HUMO

Naibu waziri wa maji mhandisi Dkt. Bilinith Mahenge upande wa kulia, akimsikiliza mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu alipokwenda kumtembelea ofisini kwake mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku tano mkoani humo.(Picha na Muhidin Amri)


NAIBU WAZIRI WA MAJI AKIKAGUA MASHINE ZA KUSUKUMIA MAJI KATIKA KIJIJI CHA PERAMIHO

Naibu waziri wa maji mhandisi Dkt. Bilinith Mahenge akiangalia mashine za kusukumia maji katika kijiji cha Peramiho.(Picha na Muhidin Amri)

KIONGOZI AKITOA NENO MARA BAADA YA KUKAGUA MRADI WA MAJI

Naibu waziri wa maji mhandisi Dkt. Bilinith Mahenge akizungumza mara baada ya kuona mradi wa maji katika kijiji cha Peramiho A  wilayani Songea mkoani Ruvuma.(Picha na Muhidin Amri)

MKIRIKITI AKITOA TAARIFA YA MAENDELEO KATIKA KIKAO CHA MAJUMUISHO YA ZIARA YA NAIBU WAZIRI WA MAJI



Mkuu wa wilaya ya Songea Josepph Mkirikiti kushoto akitoa taarifa ya maendeleo ya wilaya yake kwa Naibu waziri wa maji mhandisi Dkt. Billinith Mahenge aliyekaa katikati wakati wa majumuisho ya ziara ya waziri huyo mkoani Ruvuma.(Picha na Muhidin Amri)

KIONGOZI AKIELEKEZA JAMBO



Naibu waziri wa maji mhandisi Dkt.  Bilinith Mahenge akielekeza jambo kwa viongozi wa wilaya ya Namtumbo mara baada ya kutembelea chanzo kimojawapo cha maji mjini Namtumbo hivi karibuni.(Picha na Muhidin Amri)

NAMTUMBO WATAKIWA KUWA WABUNIFU KATIKA UJENZI WA MIRADI YA MAJI

Naibu waziri wa maji mhandisi Dkt. Bilinith Mahenge akizungumza na viongozi wa wilaya ya Namtumbo, ambapo aliwataka kuwa wabunifu wa miradi ya maendeleo ikiwemo ya maji badala ya kusubiri misaada kutoka serikalini hali inayozidisha kuongezeka kwa umasikini wa wilaya hiyo. Kushoto ni mkuu wa wilaya hiyo Abdul Lutavi na kulia mkurugenzi wa wilaya  Mohamed Maje.(Picha na Muhidin Amri)

KARIBU NAIBU WAZIRI UZUNGUMZE NA VIONGOZI WA WILAYA YA NAMTUMBO



Mkuu wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Abdul Lutavi akimkaribisha Naibu waziri wa maji mhandisi Bilinith Mahenge aliyekaa katikati, kwa lengo la kuzungumza na viongozi wa wilaya hiyo. Kulia ni mkurugenzi wa wilaya hiyo Mohamed Maje.(Picha na Muhidin Amri)

NAIBU WAZIRI AKIZUNGUMZA NA WATAALAMU WA MAJI

Naibu waziri wa maji mhandisi Bilinith Mahenge wa kwanza kushoto, akizungumza na watumishi wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira mji wa mbinga(MBIUWASA) hivi karibuni alipokuwa katika ziara yake wilayani humo.(Picha na Muhidin Amri)

VIONGOZI WA WILAYA YA MBINGA WATAKIWA KUFUATILIA KWA KARIBU UJENZI WA MIRADI YA MAJI AMBAYO INAENDELEA KUJENGWA WILAYANI HUMO



Mkuu wa wilaya Mbinga Senyi Ngaga aliyekaa upande wa kulia, akimsikiliza Naibu waziri wa maji mhandisi Bilinith Mahenge wakati akitoa maagizo kwake juu ya ufuatiliaji wa miradi ya maji inayoendelea kutekelezwa katika wilaya hiyo.(Picha na Muhidin Amri)

MAHENGE: JENGENI MIRADI YA MAJI KWA VIWANGO VINAVYOKUBALIKA


Naibu waziri wa maji mhandisi Bilinith Mahenge kulia, akisisitiza juu ya wataalamu wa maji kuhakikisha wanajenga miradi hiyo ya maji kwa kiwango bora. Anayeshuhudia upande wa kushoto ni Mbunge wa viti maalum mkoani Ruvuma, Injinia Stella Manyanya.(Picha na Muhidin Amri)

STELLA MANYANYA AKISISITIZA JAMBO KWA NAIBU WAZIRI



Mbunge wa viti maalum mkoani Ruvuma mhandisi Stella Manyanya kushoto akisisitiza jambo kwa Naibu waziri wa maji mhandisi Bilinith Mahenge, wakati waziri huyo alipokuwa katika ziara yake wilayani Nyasa.(Picha na Muhidin Amri)

KIONGOZI AKIPOKEA MAELEZO

Mhandisi wa maji wilaya ya Mbinga Evaristo Ngole kushoto akimfafanulia jambo Naibu waziri wa maji Mhandisi Dkt. Bilinith Mahenge juu ya kukamilika kwa   ujenzi wa tangi la maji na huduma ya   maji katika kijiji cha Ng'ombo wilayani Nyasa, Ruvuma ulivyokamilika ambapo utasaidia kupunguza tatizo kubwa la upatikanaji wa maji katika kijiji hicho.(Picha na Muhidin Amri)

NAIBU WAZIRI WA MAJI AKIKAGUA TANKI LA MAJI AMBALO LIMEJENGWA NA UNDP

Naibu waziri wa maji mhandisi Dkt. Bilinith Mahenge akipanda kukagua tanki la maji safi na salama katika kijiji cha Ng'ombo wilayani Nyasa Ruvuma hivi karibuni akiwa katika ziara yake wilayani humo ya kukagua miradi ya maji ambayo imejengwa kwa msaada wa fedha kutoka shirika la maendeleo la kimataifa UNDP. Tanki hilo limejengwa kwa thamani ya shilingi milioni 298. (Picha na Muhidin Amri)




Saturday, January 12, 2013

AFARIKI DUNIA KUTOKANA NA KUGONGANA NA GARI USO KWA USO

Na Steven Augustino, 
Songea.
 
Mwendesha Pikipiki mkazi wa kijiji cha Lipokela Songea vijijini Issack Gillas(31) amefariki dunia katika ajali mbaya ya kugongana  Pikipiki aliyokuwa akiiendesha na gari lililokuwa likipita barabarani.
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Ruvuma Deusdedith Nsemeki alisema, tukio hilo lilitokea Januari 8 mwaka huu katika Barabara ya Songea kwenda Mbinga mkoani humo.
Nsemeki alisema kuwa katika tukio hilo pikipiki hiyo yenye namba za usajiri T. 937 CCA  iligongana uso kwa uso na gari aina ya Toyota Hilux lenye namba za usajili T. 730 AXZ.

Tuesday, January 8, 2013

AUAWA NA MWILI WAKE KUTUPWA MASHAMBANI KUTOKANA NA UGOMVI WA KIMAPENZI


Na Steven Augustino,
Tunduru.

MKAZI mmoja wa kijiji cha Tinginya tarafa ya Nakapanya wilayani Tunduru, Ruvuma amekutwa mwili wake ukiwa umetupwa katika mashamba ya kijiji hicho, baada ya kuuawa kikatili na kujeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili wake.

Marehemu ametambuliwa kwa jina la Abdallah Kingunge(35) ambapo kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo walisema, tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Januari 4 mwaka huu.

Walifafanua  kuwa mkasa huo umewasikitisha wengi na kuleta gumzo katika kijiji hicho na kutajwa kuwa huu ni mwanzo mbaya kwao kwa mwaka huu ni sawa na kutia nuksi kwa wanakijiji wa Tinginya ambao daima huishi kwa amani na upendo.

WATOTO MKOANI RUVUMA KUPATIWA CHANJO YA VICHOMI NA KUHARISHA

Na Steven Augustino,
Songea.

ZAIDI ya watoto 53,000 wenye umri chini ya miaka mitano mkoani Ruvuma, wanatarajiwa kupata chanjo mpya ya ugonjwa wa kichomi na kuharisha mkoani humo.

Wakati taarifa za takwimu za magonjwa hayo zikitolewa, zinaonesha  kusababisha watoto takribani 6000 kupoteza maisha kila mwaka na kushika nafasi ya pili na ya tatu kwa kusababisha vifo vingi vya watoto yakitanguliwa na ugonjwa wa Malaria.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu alisema hayo wakati wa uzinduzi wa chanjo hizo za kuzuia ugonjwa wa kichomi na kuharisha, kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano ambao umekuwa ukisababisha vifo vingi kwa watoto hao.

Friday, January 4, 2013

TANESCO MBINGA MASWALI MENGI KULIKO MAJIBU

Kassian Nyandindi



















Na Kassian Nyandindi,                                         Uchambuzi.

TATIZO la upatikanaji wa umeme wa uhakika katika mji wa Mbinga, hivi sasa imekuwa ni kero kiasi ambacho wakazi wa mji huo wameanza kulalamikia hali hiyo.

Binafsi nimelichunguza tatizo hili na kubaini  TANESCO kuanzia ngazi ya wilaya hadi huko juu, ni muhimu kuchukua hatua za haraka kunusuru hali hiyo ili isiweze kuendelea na kuleta malalamiko yasiyo ya lazima miongoni mwa jamii.

Ukosefu wa umeme wa uhakika katika mji huu wa Mbinga unatokana na Transfoma yenye ukubwa wa KVA 100 – 11KV kushindwa kufanya kazi yake ipasavyo kwa sababu ya kubebeshwa mzigo mkubwa nje ya uwezo wake.

Transfoma hiyo ndio kiini kikuu ambacho hutegemewa kusambaza nishati hiyo muhimu katika maeneo ya viwanda, mashine za kukobolea nafaka na maeneo mengine ya nyumba za kuishi watu.

WAJUMBE WA ALAT RUVUMA WAKIANGALIA MTARO WA KUPELEKA MAJI SHAMBANI KWA AJILI YA KILIMO CHA MPUNGA



Baadhi ya wajumbe wa ALAT mkoa wa Ruvuma, wakiangalia mtaro mmojawapo katika mradi wa shamba la mpunga Mbamba bay wilayani Nyasa hivi karibuni walipokuwa katika kikao chao kilichofanyika katika mji wa Mbamba bay.(Picha na Muhidin Amri)