Saturday, February 23, 2013

WADAU WA ELIMU MBINGA WASHAURIWA KUJENGA MSHIKAMANO




Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Agustivo iliyopo wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, wakitumbuiza katika mahafali ya kidato cha sita yaliyofanyika shuleni hapo jana.(Picha na Kassian Nyandindi)





Na Julius Konala,
Mbinga.

WADAU wa elimu wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, wametakiwa kujenga mshikamano katika kuendeleza na kukuza kiwango cha elimu wilayani humo.

Sambamba na hilo wametakiwa kujenga mshikamano katika kuhakikisha kwamba watoto wao, wanafuatilia kwa umakini masomo yao darasani.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa shirika lisilo la kiserikali la Mission Africa, Emmilian Kapinga wakati akihutubia katika mahafali ya kidato cha sita shule ya sekondari Agustivo iliyopo mjini hapa.


Alisema kuwa wasipozingatia hilo, huenda Mbinga ikazalisha kundi kubwa la watu wasiojua kusoma na kuandika hivyo kuhatarisha maendeleo ya taifa hili kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Kapinga alisisitiza kuwa kinachotakiwa ni mzazi kuhakikisha kwamba mtoto  anampeleka shule na kumlea katika maadili mazuri.

Mwenyekiti huyo aliweza kuchangia shule vitabu 20 vya somo la hesabu na kompyuta nne vyote vikiwa na jumla ya thamani ya shilingi milioni 1.6.

Kufuatia taarifa ya maendeleo ya shule hiyo iliyotolewa na mkuu wa shule ya sekondari Agustivo, Moses Mapunda ilisema shule hiyo inakabiliwa na tatizo la ukosefu wa jengo la maabara na vifaa vyake, vitabu vya kiada na ziada na baadhi ya wanafunzi kukatisha masomo yao kutokana na hali duni za wazazi wao au mzazi husika kufariki dunia.








 

No comments: