Thursday, July 17, 2014

DOKTA KIKWETE LEO AANZA ZIARA MKOANI RUVUMA, AZINDUA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU SONGEA



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Kikwete akikata utepe kufungua rasmi nyumba zilizojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika eneo la Mkuzo, Songea mkoani Ruvuma. Kushoto ni mke wa Rais Mama Salma Kikwete, Waziri wa ardhi nyumba na makazi Prof. Anna Tibaijuka, Kaimu mkurugenzi mkuu wa shirika la nyumba la taifa David Misonge Shambwe na upande wa kulia ni Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu.

Ris Dokta Jakaya Kikwete akifunua jiwe la msingi wakati wa ufunguzi wa nyumba zilizojengwa kwa gharama nafuu na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) huko Mkuzo Songea mjini mkoani Ruvuma leo. Kushoto ni kaimu Mkurugenzi wa NHC David Misonge Shambwe na wa pili kutoka kushoto ni Waziri wa ardhi nyumba na makazi Prof. Anna Tibaijuka. (Picha zote na Freddy Maro.)

No comments: