Thursday, July 17, 2014

UZINDUZI WA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU SONGEA WAFANA, RAIS AIPONGEZA NHC


Rais Jakaya Kikwete akiwa na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu (upande wa kulia), Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) David Shambwe wakikata utepe kwa pamoja ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mradi wa nyumba za shirika hilo.
 Rais Kikwete akipata taarifa ya mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC mjini Songea, kutoka kwa kaimu mkurugenzi wa shirika hilo  David Shambwe.
 
  Rais Kikwete akizungumza leo wakati wa uzinduzi wa mradi huo wa nyumba mjini Songea, ambapo aliipongeza NHC kwa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu na kulitaka shirika hilo liendeleze jitihada hizo za ujenzi wa nyumba bora.
 
 Rais Kikwete akipata maelezo juu ya Mashine za kufyatulia matofali  ambazo zimegawiwa kwa kila wilaya za mkoa wa  Ruvuma.
 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Profesa Anna Tibaijuka akizungumza katika hafla hiyo mchana wa leo mjini Songea.
 
 Akiwasalimia wananchi waliofika kushuhudia tukio hilo la ufunguzi wa nyumba hizo.

Vikundi mbalimbali vya ngoma za asili mkoani Ruvuma, vikitoa burudani wakati Rais Kikwete akiwasili eneo la tukio la ufunguzi wa nyumba hizo. (Picha zote kwa hisani ya NHC)
 

No comments: