Na Steven Augustino,
Tunduru.
SERIKALI wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, imewahimiza wananchi wake kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, ili waweze kupata vitambulisho vya kitaifa.
SERIKALI wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, imewahimiza wananchi wake kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, ili waweze kupata vitambulisho vya kitaifa.
Wito huo umetolewa na Mkuu wa wilaya hiyo, Chande Nalicho
wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo ambalo lilifanyika kwenye ofisi za mkuu huyo
wa wilaya, zilizopo mjini hapa.
Nalicho alifafanua kuwa miongoni mwa faida za vitambulisho
hivyo, ni pamoja na kila Mtanzania kutambuliwa kadhalika kitakuwa na msaada
mkubwa kwa mtu binafsi hasa pale anaposafiri nje ya nchi.
Alisema kuwa wito huo ameutoa kwa wananchi wake wa wilaya
hiyo, kutokana na kuwa pembezoni mpakani mwa Tanzania na Msumbiji hivyo kuwepo
kwa vitambulisho hivyo kutasaidia hata mamlaka husika, kuwatofautisha wananchi
wake kutokana na muingiliano uliopo miongoni mwao.