Thursday, June 13, 2013

CCM IKIPINGA SERIKALI TATU, CHIKAWE AJIPANGA KWA KATIBA YA BARA

 


    Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akifafanua jambo.
     

























    Editruda Mashimi, 
    Dar es Salaam.

    RASIMU ya Katiba mpya inayoruhusu muundo wa serikali tatu imezidi kukichanganya Chama Cha Mapinduzi (CCM),  Chama hicho tawala kimepinga muundo huo kimesema bado kinaamini katika muundo wa Serikali mbili.

    Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dodoma jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye aliwaambia kwamba mapendekezo yaliyofikishwa mbele ya tume hiyo yatabaki kama yalivyo,Na hivyo msimamo wao ni kuwepo kwa muungano wenye Serikali mbili kama ilivyo sasa.


    “Mapendekezo ambayo ndiyo msimamo wa chama tulishayawasilisha kwenye Tume kuwa sisi tunapendekeza mfumo wa Serikali mbili na siyo tatu wala moja,” alisema Nape alipokuwa akitoa taarifa ya uamuzi wa Kamati Kuu (CC) ya CCM iliyokutana usiku wa kuamkia jana kujadili suala hilo.

    Wakati CCM ikipinga kuwepo kwa serikali tatu, Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chakawe amesema upo uwezekazo wa Katiba Mpya ya Tanzania Bara ikapatikana kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2015.

    Chikawe alisema kwamba ikiwa mchakato wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano utakamilika kama inavyokusudiwa na rasimu hiyo kupitishwa na wananchi katika ngazi zote bila mabadiliko, muda utakaobaki utatosha kuandaa Katiba ya Tanzania Bara.

    “Watu wasiwe na hofu. Sioni tatizo endapo rasimu itapita bila mabadiliko na kupata Katiba Mpya. April mwakani mpaka Desemba inatosha kabisa kuandaa Katiba ya Tanzania Bara na tukaenda katika Uchaguzi Mkuu tukiwa na Katiba Mpya,” alisema Chikawe.

    No comments: