Tuesday, June 11, 2013

KAMPUNI YA SUPERFEO EXPRESS, YAZINDUA MAGARI YAKE YA KUTOKA MBINGA HADI DAR ES SALAAM

Magari ya Kampuni ya Superfeo Express, yakiwa pamoja katika eneo la Stand kuu Mbinga mjini yakisubiri kuzinduliwa tayari kwa safari ya kutoka Mbinga hadi Dar es Salaam.

Katibu tawala wa wilaya ya Mbinga, Idd Mponda akizundua magari ya Kampuni ya Superfeo Express katika eneo la Stand kuu Mbinga mjini, tayari kwa kuanza safari ya kutoka Mbinga mjini kwenda Dar es Salaam, gari hizo zinatarajia kuanza safari yake mapema alfajiri kesho, Juni 12 mwaka huu.

Hapa Wadau wakifurahia mara baada ya uzinduzi huo kufanyika, ambapo kushoto ni Mwenuyekiti wa CCM mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho, wa pili kutoka kushoto ni Katibu tawala wa wilaya ya Mbinga Idd Mponda na watatu ni Mkurugenzi wa kampuni ya Superfeo Express Omary Msigwa.

Hizi ni moja kati ya gari mpya mbili, za kampuni ya Supperfeo Express ambazo zitaanza safari yake kuanzia kesho alfajiri Juni 12 mwaka huu, kutoka Mbinga kwenda Dar es Salaam. (Picha zote na Kassian Nyandindi)

No comments: