Saturday, December 27, 2014

UVCCM RUVUMA YAITAKA JAMII KUFARIJI WAGONJWA



Steven Augustino na Abbas Mlanya,
Tunduru.

UMOJA wa Vijana Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoani Ruvuma, umewataka wadau mbalimbali kujenga tabia ya kuwatembelea wagonjwa ambao wamelazwa hospitalini, kwa lengo la kuwafariji na kuwapatia zawadi hasa katika kipindi cha sikukuu za kitaifa.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa umoja huo mkoani hapa, Alex Nchimbi wakati alipowatembelea wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya wilaya ya Tunduru.

Aidha Nchimbi ambaye aliongozana na viongozi wenzake wa chama cha mapinduzi wilayani humo, wakiwemo wakiwemo katibu wa CCM wilaya Mohammed Lawa, Abdakah Zubery Mmala (Mwenyekiti wa UVCCM wilaya), Jumma Khatibu (Katibu UVCCM wilaya) wakiwemo pia makada na wakereketwa wa chama hicho.

Monday, December 22, 2014

SAKATA LA ESCROW: RAIS KIKWETE AZUNGUMZA NA WAZEE

Na Mwandishi wetu,
Dar.

RAIS Jakaya Kikwete hatimaye leo ametengua nafasi ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka kupitia hotuba aliyotoa kuzungumzia kashfa ya upotevu wa fedha kutoka akaunti ya Tegeta Escrow.

Hatua hiyo imechukuliwa na Rais Kikwete mbele ya wazee wa Dar es Salaam, aliokuwa akiongea nao na matangazo kurushwa moja kwa moja kupitia televisheni ya taifa na vyombo vingine.

Uchunguzi uliofanywa na kamati ya hesabu za umma ya Tanzania (PAC) ilidai kuwa Profesa Tibaijuka ni mmoja wa watu walionufaika kinyume cha sheria, kwa kujipatia fedha zilizotoka katika akauti hiyo iliyofunguliwa kutunza fedha kusubiri ufumbuzi wa mgogoro wa kibiashara kati ya kampuni ya kusambaza umeme TANESCO na kampuni binafsi ya kuzalisha umeme ya IPTL.

Siku chache zilizopita Profesa Tibaijuka aliitisha mkutano na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam, kubainisha kuwa hakuwa akikusudia kujiuzulu kutokana na tuhuma zilizokuwa zikimkabili.

Aidha Rais Kikwete hakutangaza kuwachukulia hatua watumishi wengine waliodaiwa kuhusika na tuhuma hiyo, kwa maelezo kuwa uchunguzi zaidi unatakiwa kwa kila mtuhumiwa.

Kumekuwa na ubishi mkubwa kujadili endapo fedha ambazo ni mabilioni zilizochukuliwa zilikuwa za umma au la. 

Hata hivyo Rais Kikwete alisema maelezo aliyopewa na wataalamu yanaonyesha hazikuwa mali ya TANESCO.

KAYOMBO ALALAMIKIWA NA WAPIGA KURA WAKE KWA KUMTETEA MKURUGENZI MTENDAJI NA MKUU WA WILAYA YA MBINGA, WASEMA MWAROBAINI WAKE UCHAGUZI MKUU MWAKANI

Gaudence Kayombo.
Na Kassian Nyandindi,

Mbinga.

BAADHI ya Wakazi wa mji wa Mbinga mkoani Ruvuma, wamemtaka Mbunge wa jimbo la Mbinga, Gaudence Kayombo kufuta kauli zake anapokuwa akihutubia wananchi katika majukwaa ya kisiasa na kujenga hoja za kuwatetea Mkurugenzi mtendaji Hussein Ngaga na Mkuu wa wilaya hiyo, Senyi Ngaga kwamba ni viongozi wazuri na wameleta maendeleo makubwa wilayani humo.

Sambamba na hilo wananchi hao ambao ni wapiga kura wake, wamesema kuwa kauli za Kayombo kuwatetea viongozi hao ni sawa na kujichimbia kaburi kwa kupoteza nafasi aliyonayo, katika uchaguzi mkuu ujao ambao unatarajiwa kufanyika mwakani kwa nafasi ya kumchagua Rais, Wabunge na Madiwani.

Walifafanua kuwa wanamshangaa Mbunge huyo amekuwa akiwasafisha viongozi hao wawili kwamba wanafanya vizuri, wakati maendeleo mengi yaliyofanywa wilayani humo yamefanywa na viongozi wenzao waliowatangulia na sio wao ambao wamefika hapa wilayani wanamuda mfupi na hakuna jambo jipya la maendeleo walilobuni na  kuweza kujivunia   kwa wananchi wakati mengi yaliyopo wanayoyaendeleza ni yale ambayo yalifanyiwa ubunifu na viongozi wenzao waliowatangulia.

Hayo yalisemwa jana na wakazi wa mji wa Mbinga kwa nyakati tofauti, mara baada ya Mbunge Kayombo kumaliza kuhutubia katika viwanja vya soko kuu mjini hapa, kwenye mkutano wa hadhara ambao uliandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo kwa ajili ya kushukuru wapiga kura wake kukipatia viti vingi vya nafasi ya Wenyeviti wa vitongoji, katika chaguzi za serikali za mitaa zilizofanyika hivi karibuni. 

Saturday, December 20, 2014

WAPOTEZA MAISHA KWA MAMBO YA KIMAPENZI NA USHIRIKINA



Steven Augustino na Abbas Mlanya,
Ruvuma.

WATU wawili wamefariki dunia mkoani Ruvuma, katika matukio mawili tofauti yaliyotokea wilayani Tunduru na Namtumbo mkoani humo, ambapo la kwanza linasababishwa na wivu wa kimapenzi na lingine linahusishwa na mambo ya ushirikina.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio lililotokea wilayani Tunduru, walisema kuwa marahemu aliyetambuliwa kwa jina la Yusuph Jafari ambaye amehamia wilayani humo, akitokea wilaya ya Masasi alikuwa kinara wa kutembea na wake za watu na baadaye kuuawa na watu wasiojulikana.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Ruvuma, ASP Mihayo Msikhela alisema kuwa tukio la kwanza lilitokea  Disemba 16 mwaka huu katika kitongoji cha Naunditi kijiji cha Majimaji, kilichopo kata ya Muhuwesi wilayani humo.

MKURUGENZI MTENDAJI MBINGA AMDANGANYA RAIS KIKWETE, ADAIWA KUCHOTA FEDHA ZA WAKULIMA WA KAHAWA NA KUZIPANGIA MATUMIZI KINYUME NA TARATIBU ZA USHIRIKA

Rais Jakaya Kikwete.

Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

SHILINGI bilioni 2 ambazo baadhi ya vyama vya ushirika wa kahawa wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, vilikopeshwa hivi karibuni na shirika la hifadhi ya jamii (NSSF) zimezua malalamiko kwamba, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo, Hussein Ngaga hakuzipeleka kwenye vyama hivyo badala yake anadaiwa kuziingiza kwenye akaunti ya halmashauri ya wilaya hiyo na kuanza kukopesha vikundi husika.

Imeelezwa kuwa kitendo kilichofanywa na mkurugenzi huyo, ni ukiukwaji wa sheria na taratibu za ushirika, hivyo alitakiwa fedha hizo azifikishe kwanza kwenye ushirika kwa kufuata mgawo husika na sio yeye kuzipangia matumizi na kwamba kwa kufanya hivyo, amemdanganya Rais Jakaya Kikwete kwa kauli yake aliyoitoa hivi karibuni mbele yake kwamba fedha hizo watakabidhiwa walengwa wa vyama vya ushirika.

Rais Kikwete mnamo Julai 19 mwaka huu, alikabidhi mfano wa hundi kwa viongozi wa vyama vya ushirika ambavyo vilikopeshwa fedha hizo alipokuwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo, kwa vyama vinne ambavyo vilipewa mkopo huo na shirika hilo.

Friday, December 19, 2014

WAANDIKISHAJI NA WASIMAMIZI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA WILAYANI MBINGA WALALAMIKIA POSHO ZAO

Waziri wa TAMISEMI Hawa Ghasia (kulia) pamoja na Katibu mkuu TAMISEMI Jumanne Sagini. (kushoto)
Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

KASORO za uchaguzi zilizojitokeza katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika hivi karibuni hapa nchini, pia hali ya hewa imechafuka wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma kufuatia baadhi ya Waandikishaji na Wasimamizi wa uchaguzi huo, kumlalamikia Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo Hussein Ngaga, kwamba malipo ya posho walizolipwa katika zoezi hilo amewalipa kidogo, tofauti na maeneo mengine nje ya wilaya hiyo.
Aidha kufuatia hali hiyo Waandikishaji na Wasimamizi hao wamemuomba Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Hawa Ghasia, kuingilia kati na kuweza kulifanyia kazi jambo hilo ili waweze kupata haki yao ya msingi kwa kazi waliyofanya.
Malalamiko hayo yalitolewa kwa nyakati tofauti walipokuwa wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, kwa kuomba majina yao yasitajwe gazetini ambapo walisema kuwa hata wakati wanafanyiwa semina na kupewa miongozo juu ya utekelezaji wa zoezi hilo, hawakulipwa posho badala yake waliambiwa kwamba watalipwa mara baada ya uchaguzi kufanyika.

Thursday, December 18, 2014

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA: WACHOMEWA NYUMBA MOTO KUTOKANA NA MALUMBANO YA KISIASA



Na Steven Augustino,
Tunduru.

UCHAGUZI wa Serikali za Mitaa ambao umefanyika hivi karibuni Disemba 14 mwaka huu, umeacha makovu wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma kwa baadhi ya viongozi na wakereketwa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kuchomewa moto nyumba zao na watu wasiojulikana, na kusababisha hasara kubwa ya kuunguliwa mali zilizomo ndani ya nyumba hizo pamoja na kukosa makazi. 

Taarifa za tukio hilo zinaeleza kuwa Diwani wa kata ya Ngapa Rashid Issaya na mwanachama wake Hassan Liugu nyumba zao zilichomwa moto, baada ya kuzuka malumbano ya kisiasa na kuwasababishia hasara kubwa ya kuungua nyumba zao pamoja na mali zilizokuwemo ndani yake.

Sambamba na tukio hilo, mfuasi mmoja wa Chama Cha Wananchi (CUF) Yashua Kawisa (21) ambaye ni mkazi wa kijiji cha Mbesa wilayani humo, naye amejeruhiwa vibaya kwa kukatwa mapanga, wakati akiwa katika kampeni za uchaguzi huo.

AFARIKI DUNIA BAADA YA KUKANYAGWA NA LORI



Na Steven Augustino,
Tunduru.

KIJANA mwenye umri wa miaka 15 aliyefahamika  kwa jina la Khasim Mohammed, mkazi wa kijiji cha Mtangashari wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma amefariki dunia baada ya kupata ajali katika gari, ambalo alikuwa ameomba msaada ili aweze kusafiri.

Mihayo Msikhela kamanda wa polisi wa mkoa huo, alisema kuwa marahemu huyo alifariki dunia papo hapo baada ya kuanguka katika gari hilo.

Alisema ajali hiyo ilitokana na gari lenye namba za usajiri T699 BCX mali ya kampuni ya China Civil Engineering Construction Co.Ltd (CCECC) inayojenga kipande cha barabara kilometa 58.7 kutoka Tunduru mjini hadi Matemanga. 

Tuesday, December 16, 2014

MADIWANI MBINGA KUMSHTAKI MKURUGENZI KWA WAZIRI MKUU

Waziri mkuu, Mizengo Pinda.

Na Kassian Nyandindi,

Mbinga.

BAADHI ya Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, wanampango wa kwenda kumuona Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Mizengo Pinda kwa lengo la kufikisha kilio chao juu ya mgogoro ambao unaendelea kati ya mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo na Afisa elimu wa msingi wa wilaya hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari hizi, Madiwani hao walisema kuwa wamechoshwa na mambo ambayo yanafanywa na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Mbinga, Hussein Ngaga kwa kuendekeza migogoro na mambo yasiyokuwa na tija katika jamii.

Aidha walifafanua kuwa Ngaga ameshindwa kuiongoza wilaya hiyo, kutokana na kuendekeza migogoro na afisa elimu msingi wa wilaya hiyo, Mathias Mkali na kuchukua hatua ya kumsimamisha kazi kinyume na taratibu za utumishi wa umma wakati hana makosa.

SAFARI YA MWISHO YA MARAHEMU MENAS ANDOYA MBUNDA, ASKOFU NDIMBO AWATAKA WAKRISTO KUTENDA MEMA KATIKA MAISHA YAO

Mzee Asteri Ndunguru, upande wa kulia akisoma taarifa fupi ya marahemu Menas Mbunda Andoya nyumbani kwa marahemu mjini hapa.

Mwili wa marahemu Menas Mbunda Andoya ukiombewa katika kanisa la Mtakatifu Killian lililopo mjini Mbinga.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma naye alishiriki katika ibada ya mazishi hayo, kwenye kanisa la Mtakatifu Killian Mbinga mjini.

Na Kassian Nyandindi,

Mbinga.

WAKRISTO wametakiwa kuacha matendo ya kumpuuza mwenyezi Mungu, badala yake wametakiwa kutenda mema katika maisha yao ya kikristo kwani hakuna binadamu aliyefunga mkataba na Mungu juu ya kuishi.

Hayo yalisemwa na Askofu mkuu wa jimbo la Mbinga mkoani Ruvuma, John Ndimbo alipokuwa akihutubia katika misa takatifu ya mazishi ya marahemu Menas Andoya kwenye kanisa la mtakatifu Kiliani lililopo mjini hapa.

“Miili yetu ni hekalu la bwana na maskani ya mpito hapa duniani, inatupasa kufanya kila jitihada kwa mambo ambayo yanampendeza Mungu, hakuna binadamu asiyekuwa na utashi juu ya kifo”, alisema Ndimbo.

Monday, December 15, 2014

KABROTHER KUINGIA SOKONI NA MKUKI KWA NGURUWE

Msanii Gidion Kabrother akisisitiza jambo, wakati alipokuwa akizungumza na Mkurugenzi wa mtandao huu, Kassian Nyandindi Mbinga mjini mkoa wa Ruvuma.

Hii ni moja kati ya Filamu yake ambayo aliitoa mara ya mwisho, ikitamba kwa jina la Ni Shida, ambayo ipo sokoni.
Na Kassian Nyandindi,
Ruvuma.

MUIGIZAJI wa filamu nchini, Gidion Simon maarufu kwa jina la Kabrother anatarajia kutoa filamu yake mpya yenye picha kali, ambayo itatamba hivi karibuni kwa jina la Mkuki kwa Nguruwe hivyo wadau mbalimbali amewataka kukaa mkao wa kula na kuipokea albamu hiyo, kwa kuendelea kumuunga mkono kwa kazi zake.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Kabrother anasema filamu hiyo inazalishwa na kusambazwa na kampuni ya Pamoja Film, iliyopo Jijini Dar es Salaam.

Anafafanua kuwa filamu hiyo imebeba maudhui mazuri yenye kulenga kuelimisha jamii, ikiwemo inakemea vitendo vinavyofanywa na baadhi ya wafanyakazi mahospitalini wenye tabia ya kutibu wagonjwa, kwa kutumia madawa ambayo yamepitwa muda wake wa matumizi na kusababisha madhara kwa mtumiaji.

“Ndugu mwandishi katika matumizi ya madawa haya feki ni hatari sana, hata mkurugenzi husika mwenye hospitali hujikuta siku ya mwisho hata ndugu yake akiathirika na madawa hayo kwa sababu tu ya uzembe huu na kusababisha nguvu kazi ya taifa hili kupotea”, anasema Kabrother.

Pia filamu hiyo inaiasa jamii hasa kwa wale wenye kipato, kuacha tabia au matendo ya kuumiza wenzao kwa namna moja au nyingine kutokana tu, na hali ya uchumi mzuri walionao.

DEREVA ALIYEFANYA MAUAJI TUNDURU ASAKWA



Na Steven Augustino,
Tunduru.

POLISI wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, wanamsaka dereva aliyekuwa akiendesha pikipiki aina ya SUNLG yenye namba za usajiri T 115 CZE ili aweze kujibu mashitaka ya mauaji aliyoyafanya baada ya kumgonga mwendesha baiskeli.

Dereva huyo ambaye jina lake halijafahamika anadaiwa kufanya mauaji hayo, Disemba 13 mwaka huu majira ya saa 5:00 asubuhi katika kijiji cha Tuleane kilichopo Tarafa ya Mlingoti – Namasakata mjini hapa.

Imeelezwa na Kamanda wa polisi wa mkoa huo, Mihayo Msikhela kuwa mauaji hayo aliyafanya kwa kumgonga na pikipiki Rashid Tawakali (50) wa kijiji cha Nakayaya wilayani humo na kumsababishia kifo papo hapo.

ILE NYOTA ILIYONG'ARA MBINGA KIMAENDELEO IMEZIMIKA, KATIBU MKUU UMOJA WA VIJANA TAIFA ATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI


Menas Mbunda Andoya wakati wa uhai wake akiwa na mkewe na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, hivi karibuni wakati wa uzinduzi wa mradi wake wa kuzalisha umeme, maporomoko ya maji katika kijiji cha Lifakara, kata ya Mbangamao wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma.



Na Kassian Nyandindi,
Ruvuma. 

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Vijana Taifa kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Sixtus Mapunda, ametoa salamu za pole kwa wananchi wa wilaya ya Mbinga na mkoa wa Ruvuma kwa ujumla, kwa kuondokewa na mwanaharakati ambaye ni mpiganaji katika mchango wa kukuza maendeleo wilayani humo, Marahemu Menas Mbunda Andoya.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Katibu huyo alisema kuwa amepokea taarifa ya kifo cha mwanaharakati huyo, kwa masikitiko makubwa na kuwataka wananchi wa wilaya hiyo, kuungana pamoja katika kipindi hiki cha majonzi.

Mapunda alifafanua kuwa katika kipindi hiki kigumu, wananchi hawana budi kumuombea kwa Mungu Marahemu huyo, kwani sote tupo safarini na hapa duniani tunapita.

Marahemu Andoya alikuwa mpiganaji hasa katika shughuli nyingi za kimaendeleo wilayani Mbinga, ambapo ameacha kazi muhimu ambayo alikuwa akiitekeleza na yenye kufikia hatua ya mwisho juu ya ujenzi wa mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa maporomoko ya maji ambao unafahamika kwa jina maarufu, Andoya Hydro Electric Power (AHEPO) uliopo katika kijiji cha Lifakara kata ya Mbangamao wilayani humo. 

Lengo la mradi huo ukishakamilika taratibu husika, utaunganishwa katika mfumo wa gridi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tawi la Mbinga. 

Sunday, December 14, 2014

WANANCHI WENYE HASIRA KALI WAFANYA MAUAJI NYASA



Na  Steven Augustino,
Nyasa.

WANANCHI wenye hasira kali ambao ni wakazi wa kitongoji cha Libonde kata ya Tingi wilaya ya Nyasa mkoa wa Ruvuma, wamefanya mauaji ya watu watatu katika tukio ambalo linadaiwa kuwa chanzo chake ni kulipiza kisasi.

ASP Mihayo Msikhela ambaye ni Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma, alisema kuwa tukio hilo lilitokea Disemba 4 mwaka huu, baada ya wananchi hao kuwatia katika mtego na kufanikiwa kuwanasa.

Katika tukio hilo Kamanda Msikhela aliwataja watu waliouawa kuwa ni Herman Ndunguru (25), Kwinibeti Komba (52) na Peter Kapinga (42).

Pamoja na mambo mengine alisema, kufuatia tukio hilo Jeshi la polisi limejipanga kuwasaka wahusika wote wa tukio hilo, na kuhakikisha wanatiwa mikononi mwa dola ili sheria iweze kufuata mkondo wake.

Amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa zitakazofanikisha kupatikana kwa watuhumiwa hao, ambapo inadaiwa kuwa chanzo cha tukio la mauaji hayo kilisababishwa na kifo cha binti mmoja muuza baa ambaye hakumtaja jina lake kilichotokea mwezi Novemba mwaka huu kijijini hapo.

Saturday, December 13, 2014

MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHAURI YA MBINGA, KWA HAYA UNAYOYAFANYA NINGEKUWA MIMI NIMEKUWEKA MADARAKANI NINGEKUFUKUZA KAZI MAPEMA ASUBUHI

Rais Jakaya Kikwete, wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

SIRI juu ya mipango ambayo inaendelea kusukwa chini kwa chini, katika kuhakikisha kwamba Afisa elimu msingi wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Mathias Mkali anachukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufikishwa Mahakamani, kufuatia mgogoro uliotengenezwa na Mkurugenzi wake wa Halmashauri ya wilaya hiyo Hussein Ngaga, zimeanza kuvuja ambapo mtandao huu umeelezwa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari vimeeleza na kudai kwamba licha ya kuwepo kwa mipango ya kufikishwa Mahakamani Afisa elimu huyo, huenda kama itashindikana katika hilo atachukuliwa hata hatua ya kuhamishwa, ilimradi adhma ya mkurugenzi huyo iweze kutimia kama alivyopanga.

Serikali licha ya kuunda tume na kuja kuchunguza tatizo hili linaloendelea sasa kukera wananchi wa Mbinga, imeonekana tume hiyo kumezwa na vigogo wa halmashauri hiyo wakitaka ilinde maslahi yao binafsi, ikiwemo hudaiwa kushiriki kwa namna moja au nyingine katika kupanga mipango hiyo.

Utafiti uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini kuwa, kumekuwa na vikao ambavyo vimekuwa vikifanyika mara kwa mara katika Ikulu ndogo ya Rais wilayani hapa, kati ya vigogo wa wilaya hiyo na wajumbe husika wa tume hiyo hasa nyakati za usiku na mapema alfajiri.

TUME YATILIWA MASHAKA, BAADHI YA VIGOGO MBINGA WADAIWA KUTENGENEZA MBINU CHAFU KUHARIBU UKWELI ULIOPO

Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Na Mwandishi wetu,
Mbinga.

TUME ya watu wawili ambayo imeundwa na serikali, kwa ajili ya kuja kuchunguza mgogoro uliopo kati ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Hussein Ngaga na Afisa elimu msingi wa wilaya hiyo, Mathias Mkali imetiliwa shaka huku ikinyoshewa kidole na kudaiwa kutotenda haki kutokana na tume hiyo kuonekana ikiegemea upande wa mkurugenzi huyo.

Baadhi ya wadau wa elimu wakiwemo na watendaji wa serikali, ambao wameteuliwa kwa ajili ya kuhojiwa walisema hayo mjini hapa, wakati walipokuwa wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wetu mara baada ya kufanyiwa mahojiano na tume hiyo.

“Mambo tunayoulizwa ndani ya tume mengi yanaonesha ni yale yale ambayo yametengenezwa na mkurugenzi, sisi tunapotaka kutoa hoja zetu za msingi tunabanwa sana na kunyimwa uhuru wa kujieleza kweli hapa kuna haki? au tume hii imekuja kwa ajili ya kumbeba mtu”, ? walihoji.

Walisema wanashangazwa kuona wakati mwingine tume imekuwa ikihoji kwa kutumia lugha za vitisho, zenye kuonyesha kubeba kundi la upande mmoja na kwamba chumba cha mahojiano kilichopo katika jengo la ukumbi mdogo wa halmashauri ya wilaya hiyo, wahojiwa wamekuwa hawapewi uhuru wa kutosha wakati wa kujieleza jambo ambalo linajenga kukosa imani nao.

Aidha walieleza kuwa wanashangazwa kumuona Afisa utumishi wa wilaya ya Mbinga, Emmanuel Kapinga, kuwepo ndani ya chumba cha mahojiano na tume hiyo ambapo wakati wa mahojiano muda mwingi amekuwa mtu wa kupinga na kuwa mkali pale mhojiwa anapokuwa akitoa maelezo yenye ukweli juu ya jambo husika linaloulizwa kutoka kwa mjumbe wa tume.

Friday, December 12, 2014

MKURUGENZI MBINGA AENDELEA KUKALIA KUTI KAVU, WADAU WASEMA UMEFIKA WAKATI KWA SERIKALI KUMCHUKULIA HATUA ZA KINIDHAMU


Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

BARUA iliyoandikwa na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Hussein Ngaga juu ya kuifutia usajili asasi ya Waratibu elimu kata wilayani humo (UWEKAMBI) kwa madai kwamba imeshindwa kutimiza masharti na taratibu husika, imezua gumzo huku wakisema kuwa mkurugenzi huyo, amekosa kazi ya kufanya badala yake ajikite katika kufikiria maendeleo ya wanambinga na sio kuendekeza migogoro ambayo haina tija katika jamii.

Barua hiyo yenye kumbukumbu namba MDCC/F.10/20/64 ya Novemba 30 mwaka huu ambayo imesainiwa na mkurugenzi huyo, ambapo waratibu hao walipozungumza kwa nyakati tofauti walisema kuwa kitendo hicho kilichofanywa na mkurugenzi huyo, si cha kiungwana bali ana mambo yake binafsi ambayo hawatakii mema wananchi wa wilaya hiyo.

Walisema UWEKAMBI ilianzishwa kwa nia njema na kwa kufuata taratibu husika za usajili kupitia ofisi yake ya idara ya maendeleo ya jamii, hivyo yeye anavyosema leo kwamba umoja huo unakiuka sheria, kanuni na taratibu zinazoongoza misingi ya utendaji kazi wa asasi za kiraia, sio kweli bali anachuki binafsi huku wakimtaka asitumie vibaya cheo chake alichonacho na kuingiza mambo binafsi katika utendaji kazi wa maendeleo ya wananchi.

Wednesday, December 10, 2014

ACHENI TUME IFANYE KAZI ZAKE KWA UHURU BILA KUINGILIWA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

HATIMAYE serikali, imechukua hatua ya kuunda tume na kuileta katika halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoa wa Ruvuma, kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu juu ya tuhuma anazotuhumiwa Afisa elimu msingi wa wilaya hiyo Mathias Mkali.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Hussein Ngaga ndiye aliyeibua hoja kadhaa za kumtuhumu afisa elimu wake, na kufikia hatua ya kumsimamisha kazi kwa muda, hadi tume hii leo inaripoti hapa Mbinga kwa ajili ya kuja kuchunguza tuhuma hizo kwa lengo la kupata ukweli na kutoa ushauri nini kifanyike.

Kwa ujumla tunapenda kuipongeza serikali kwa jitihada hizi ilizozifanya, na kwamba tunashauri tu kwa kuiomba tume hiyo isimame kidete katika kutenda haki kwa pande zote mbili yaani aliyetuhumu na mtuhumiwa, ili wananchi siku ya mwisho tuweze kutambua ukweli wa jambo hili upo wapi, ambapo kila kukicha limekuwa likikera na kuleta mgogoro ambao umedumu kwa muda mrefu sasa.

Tuesday, December 9, 2014

DED MBINGA ALALAMIKIWA WAMTAKA AZINGATIE MAKUBALIANO YALIYOFANYWA NA WAZAZI

Hussein Ngaga, Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma.










Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

AGIZO lililotolewa hivi karibuni na Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, Hussein Ngaga juu ya michango wanayochanga wazazi kwa ajili ya watoto wao kujisomea wakati wa likizo (Makambi) wilayani humo, na kuingizwa kwenye akaunti ya fedha za ruzuku kutoka serikalini kwa ajili ya kuendeshea mitihani mashuleni (Capitation) limezua mapya, kufuatia kamati husika zinazojishughulisha na uendeshaji wa makambi hayo kulalamika wakidai kwamba, kufanya hivyo ni ukiukaji wa taratibu na makubaliano yaliyofanywa na wazazi kupitia vikao husika.
 
Imeelezwa kuwa ni vyema mkurugenzi huyo, akazingatia mawazo na makubaliano yaliyofanywa na wazazi hao na sio vinginevyo, hivyo kutozingatia hilo ni kukosa utawala bora katika jamii na kuleta migogoro isiyokuwa ya lazima.

Kwa nyakati tofauti walipozungumza na mwandishi wa habari hizi wajumbe wa kamati hizo walieleza kuwa, michango inayokusanywa kutoka kwa kila mzazi ambaye ana mtoto anayesoma katika shule husika, hukabidhiwa mkuu wa kambi na kamati hufanya kazi ya kupanga mapato na matumizi na sio utaratibu huo ambao mkurugenzi huyo ameutoa.

Walidai kuwa michango hiyo kuingizwa kwenye akaunti ya Capitation hivi sasa kunaleta kikwazo kikubwa kwao, hasa pale wanapohitaji kufanya matumizi husika kwani wanapokwenda kwa mkurugenzi huyo ili waweze kupata fedha hizo kwa ajili ya kuendeshea shughuli za watoto hao katika kambi, hukumbana na vikwazo vingi.

Walifafanua kuwa uendeshaji wa makambi hayo ni mfumo ambao wazazi wa wilaya hiyo walijiwekea mikakati yao wenyewe na kujenga makubaliano juu ya namna ya kuinua kiwango cha taaluma, kupitia vikao vya Mabaraza ya kata (WDC) ambapo makubaliano yao yalikuwa kila mchango unapokusanywa akabidhiwe mkuu wa kambi husika, kwa ajili ya kupanga matumizi na baadaye mwisho wa kambi taarifa ya mapato na matumizi itolewe kwenye kikao hicho cha WDC kwa eneo husika.

Saturday, December 6, 2014

WAFANYABIASHARA TUNDURU WALIA NA SERIKALI


Na Steven Augustino,

Tunduru.

WAFANYABIASHARA na walipa kodi wanaotakiwa kutumia mashine za kielektroniki (EFD'S) wilayani Tunduru mkoani hapa, wameiomba serikali inunue mashine hizo na kuzigawa bure kwa wafayabiashara hao, ili ziweze kusaidia serikali kukusanya kodi husika.

Ombi hilo limetolewa na wafanyabiashara hao wakati walipokuwa wakizungumza na maafisa waandamizi wanaosimamia ukusanyaji wa kodi, katika mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa New generation uliopo mjini hapa.

Mfanyabiashara aliyejitambulisha kwa jina la Kazembe Said ndiye aliyeanza kufanya uchokonozi wa kupenyeza ombi hilo, na kuongeza kuwa pamoja na mambo mengine wao hawapingani na taratibu za ulipaji wa kodi, isipokuwa kinacho wakwaza ni kutokuwa na mitaji ya kutosheleza kununua mashine hizo.

Wakati wafanyabiashara hao wakionekana kuunga mkono ombi hilo naye Leonsi Kimario akaja na hoja ya kuisihi serikali, kuandaa utaratibu mzuri wa matumizi na mapato ambayo yamekuwa yakitokana na kodi za wananchi tofauti na sasa, ambapo kumekuwa kukitokea kashfa za matumizi mabaya ya fedha yakiwa yanazungumzwa mara kwa mara Bungeni.

AFARIKI DUNIA BAADA YA PIKIPIKI ALIYOKUWA AKIENDESHA KUGONGA POWER TILLER



Na Mwandishi wetu,

Tunduru.

STAMILI Mohamed (42) ambaye ni mkazi wa kijiji cha Namiungo wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, amekutwa na mauti baada ya pikipiki aliyokuwa akiiendesha kupata nayo ajali, akiwa katika mwendo kasi.

Taarifa zinaeleza kuwa pikipiki hiyo aliyopata nayo ajali, ni aina ya SUNLG yenye namba za usajili T 339 na kwamba ajali hiyo, ilitokana pia na kuligonga trekta dogo ambalo hutumika kufanyia shughuli za kilimo shambani (Power tiller) na kusababisha kifo chake papo hapo.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma  Mihayo Msikhela amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo, akieleza kwamba ajali hiyo ilitokea Disemba 4 mwaka huu majira ya usiku.

CUF YATAMBA, YASEMA CCM UMEFIKA WAKATI WA KUFUNGA VIRAGO


Na Steven Augustino,

Tunduru.

CHAMA Cha wananchi (CUF) Taifa kimetangaza sera ya kutoa gawiwo kwa wananchi wake, endapo kitapatiwa ridhaa ya kuongoza nchi katika uchaguzi mkuu ujao ikiwemo wananchi watanufaika na rasilimali za taifa, katika kipindi chake cha uongozi.

Aidha kitafungua akaunti maalumu tatu ambapo baadhi ya mapato yake  ndiyo yatakayokuwa yakigawiwa kwa wananchi hao.

Katibu Mkuu wa CUF makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim seif Sharifu alisema hayo alipokuwa akihutubia wananchi wa wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kuhamasisha wananchi kujiunga na chama hicho.

Friday, December 5, 2014

TAARIFA ILIYOSOMWA NA MKAGUZI WA NDANI NA MADIWANI KUNYANG'ANYWA HII HAPA

Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

NDUGU wasomaji wa mtandao huu, sasa tunawaletea taarifa ya Mkaguzi wa ndani juu ya hoja zilizojitokeza katika kikao cha fedha, mipango na uongozi kilichoketi Septemba 25 mwaka huu wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, na kuwasilishwa katika kikao cha baraza la madiwani la wilaya hiyo Oktoba 27 mwaka huu, kama tulivyosema kuwa katika toleo lililopita kwamba Madiwani walinyang'anywa mara baada ya kusomwa katika baraza hilo.

Taarifa hiyo ambayo imesainiwa na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo Hussein Ngaga ina hoja saba za kumtuhumu Afisa elimu wake wa idara ya elimu msingi wilayani humo, Mathias Mkali kwamba amefanya ukiukwaji mkubwa wa sheria, kanuni na taratibu za fedha za utumishi wa umma, jambo ambalo baadhi ya Madiwani wengi wao walipinga hoja hizo na kusema kuwa jambo hilo halina kweli badala yake ni mambo ambayo yalikwisha kubaliwa na kupitishwa kwenye vikao halali na baraza la madiwani kwa ujumla. (nakala tunazo) 

Katika hali ya kushangaza, taarifa hiyo iligawiwa kwa madiwani katika baraza hilo, ghafla wajumbe husika (Madiwani) baada ya taarifa hiyo kumaliza kuisoma mkaguzi wake wa  ndani, Laston Kilembe na madiwani hao kuipinga, ghafla madiwani walinyang’anywa huku mkurugenzi akisimama mbele ya kikao na kueleza kuwa haijakamilika watapatiwa tena katika kikao kijacho cha baraza hilo.

Sasa taarifa yenyewe ni hii hapa.............................



Wednesday, December 3, 2014

KILELE CHA MAADHIMISHO YA WALEMAVU IRINGA: SERIKALI YAPIGA MARUFUKU UJENZI WA MAJENGO YASIYO RAFIKI KWA WALEMAVU


Waziri  wa nchi  ofisi ya  waziri  mkuu (sera na uratibu wa bunge) William Lukuvi akihutubia katika kilele  cha siku ya  walemavu duniani, maadhimisho  yaliyofanyika katika viwanja vya kichangani mjini Iringa Kitaifa,  na Lukuvi kumwakilisha  Waziri mkuu Mizengo Pinda ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo.


Waziri  wa nchi  ofisi ya  waziri mkuu  sera  na uratibu wa bunge, William Lukuvi akimkabidhi cheti cha ushiriki mlemavu, Tumaini  Mdegella kwa  niaba ya ofisi za Neema Crafti mjini Iringa  wakati wa kilele  cha maadhimisho ya  siku ya  walemavu duniani, yaliyofanyika kitaifa  mjini humo.
Na Mwandishi wetu,
Iringa.

SERIKALI  imeziagiza  Mamlaka  za  usafiri  wa majini na nchi kavu (SUMATRA )  nchini,  kuanza mchakato  wa  kukaa na  wamiliki wa  vyombo  hivyo  ili kuanza  uagizaji  wa vyombo  vya usafiri yakiwemo mabasi ambayo ni  rafiki na walemavu nchini, huku ikipiga marufuku  majengo ya   serikali kujengwa bila kuwepo kwa  mchoro  unaoonyesha mazingira yanayozingatia makundi  yote ya jamii  likiwemo la walemavu wa viungo.

Agizo   hilo  limetolewa na  Waziri  mkuu Mizengo  Pinda, wakati  wa maadhimisho ya  siku ya  walemavu  duniani yaliyofanyika   kitaifa  katika  viwanja  vya kichangani mkoani  Iringa.

Akiwahutubia   walemavu hao na  wananchi  waliofika katika  viwanja   hivyo waziri  mkuu, aliyewakilishwa na Waziri  wa nchi  ofisi ya  waziri mkuu (sera na uratibu wa bunge) Wiliam Lukuvi ambaye ni mbunge wa  jimbo la Isimani mkoani Iringa, alisema kimekuwepo kilio  cha muda  mrefu kutoka kwa  walemavu  juu ya kusahulika katika ujenzi  wa  majengo mbalimbali, ambayo yamekuwa  yakijengwa  bila kuzingatia  kundi la  watu  wenye  ulemavu jambo ambalo ni sawa na  kuwabagua watu  hao.

Aidha alisema  katika  kuona kilio  hicho  cha  walemavu  kinafanyiwa  kazi  kuanzia  sasa, majengo  yote ya  serikali  zikiwemo  shule na taasisi nyingine  kabla ya  kuanza  ujenzi  wake lazima  wasimamizi wa  ujenzi  huo kujiridhisha kwa  mchoro ambao  utaonyesha  mazingira  yatakayomuwezesha  mlemavu,   kutumia jengo  husika bila usumbufu  wowote tofauti na  ilivyo sasa ambapo  idadi kubwa ya majengo mazingira  yake  si rafiki kwa  mlemavu.

"Ni  siku  nyingi  watu  wenye ulemavu  wamekuwa  wakilalamika juu ya mazingira  yasiyo rafiki    katika majengo  mbalimbali............ sasa  leo naomba  kuagiza  kuwa michoro yote inayochorwa katika majengo ya  huduma za  kijamii,  ni marufuku  kupitishwa ama  wasimamizi  wa  ujenzi  husika  kuruhusu ujenzi  iwapo mchoro hauonyeshi  kama utajali makundi  yote wakiwemo  walemavu,

“Wasimamizi  wote msikubali  kusimamia  wala  kutangaza  tenda  ya ujenzi kama ramani  yake  si rafiki kwa  mlemavu, lakini  pia  hata  kwenye mabasi hivi unamtegemea mtu mwenye ulemavu wa miguu ataingia vipi na baiskeli  yake  katika gari iwapo hakuna mazingira  yanayomwezesha  kuingia, hivi  sasa  teknlojia  imezidi kukua na baadhi ya nchi  wameanza muda mrefu kuwajali walemavu kwa kuwa na mabasi ambayo mlemavu anaingia na baiskeli  yake  na  kushuka nayo   bila usumbufu, ni vyema hata Sumatra mkaangalia uwezekano wa  kuwajali  walemavu hawa”, alisema  Lukuvi.

WAZIRI MKUU PINDA MBINGA KUNA HAJA YA SERIKALI KUINGILIA KATI KUMALIZA TATIZO HILI

Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Na Kassian Nyandindi,

Mbinga.

TAARIFA ya Mkaguzi wa ndani juu ya hoja zilizojitokeza katika kikao cha fedha, mipango na uongozi kilichoketi Septemba 25 mwaka huu wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, na kuwasilishwa katika kikao cha baraza la madiwani la wilaya hiyo Oktoba 27 mwaka huu, imeendelea kukosolewa na wadau mbalimbali wa elimu wilayani humo wakisema kwamba ni mpango mbovu ambao ulisukwa na watu wachache wenye ni mbaya ya kurudisha nyuma maendeleo katika sekta ya elimu, licha ya kila kilichoelezwa kwenye taarifa hiyo kilikwishapitishwa kwenye vikao halali vya halmashauri ya wilaya hiyo.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo Hussein Ngaga ndiye anayenyoshewa kidole akidaiwa kuwa na kundi la watu wachache, ambao wanaelezwa ndiyo vinara wa kusuka mpango huo ambao sasa umefikia katika hatua ambayo inaleta mgogoro ambao hauna tija kwa wanambinga.

Ngaga katika taarifa hiyo ametoa hoja saba za kumtuhumu Afisa elimu wake wa idara ya elimu msingi Mathias Mkali kwamba, amefanya ukiukwaji mkubwa wa sheria, kanuni na taratibu za fedha za utumishi wa umma, jambo ambalo tumelifanyia utafiti na kubaini sio kweli badala yake ni mambo ambayo yalikwisha kubaliwa na kupitishwa kwenye vikao halali. (nakala tunazo) 

Katika hali ya kushangaza, taarifa hiyo iligawiwa kwa madiwani katika baraza hilo ambayo imesainiwa na mkurugenzi huyo, ghafla Wajumbe husika (Madiwani) baada ya taarifa hiyo kumaliza kusoma mkaguzi wa ndani, Laston Kilembe walinyang’anywa huku mkurugenzi akisimama mbele ya kikao na kueleza kuwa haijakamilika watapatiwa tena katika kikao kijacho cha baraza hilo.

Hali hiyo iliyojitokeza wengi wao walikuwa wakihoji inakuwaje baraza linaletewa taarifa ambayo haijakamilika, huku wengine wakisema huenda ndio ulikuwa mpango wenye kubeba matakwa binafsi ambayo hayana tija kwa jamii.

Tuesday, December 2, 2014

SONGEA WALALAMIKIA UBOVU WA DALADALA WAZITAKA MAMLAKA HUSIKA KUCHUKUA HATUA



Na Gideon Mwakanosya,
Songea.

BAADHI ya wakazi wa halmashauri ya Manispaa ya songea mkoa wa Ruvuma, wamezilalamikia  mamlaka husika zikiwemo kikosi cha usalama barabarani mkoani humo na  Sumatra kwa kushindwa kudhibiti daladala mbovu, zinazofanya kazi ya kubeba abiria katika manispaa hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi hao wameeleza kuwa kwa muda mrefu sasa, daladala ambazo zinaonyesha kuwa ni mbovu lakini zimekuwa zikiendela kubeba abiria zimekuwa zikihatarisha maisha ya abiria wanaotumia daladala hizo.

Felix Komba mkazi wa Mahenge alisema kuwa daladala zinazotoka Songea mjini mtaa wa Delux, kwenda Matogoro na Songea Boys zinaonekana hata kwa macho kuwa ni mbovu.

Monday, December 1, 2014

MBINGA WANASHUGHULIKA KUKOMOA WANANCHI BADALA YA KUSIMAMIA MAENDELEO, AGIZO LA RAIS KIKWETE UJENZI WA MAABARA UTATA MTUPU

Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Na Kassian Nyandindi,


SIKU zote misingi ya taifa linalojali maisha ya wananchi wake ni ujenzi bora wa elimu, afya na miundombinu inayokuza uchumi huku viongozi wake katika eneo husika hutakiwa kuwa makini, kujenga mshikamano na kuacha migogoro ya hapa na pale.

Wahenga wetu husema, ukiona kiongozi muda mwingi amekuwa akiendekeza migogoro basi tambua kwamba, mahali pale ameshindwa kutawala na maendeleo hayawezi kupatikana badala yake serikali, inashauriwa kuchukua hatua za haraka katika kunusuru hali hiyo ili wananchi wake wasipate mateso.

Kinyume chake kukosekana kwa kiongozi wa kweli na asiyejali utawala bora au maslahi ya wananchi, kunanyima watu fursa ya kufanya maamuzi sahihi kuhusu rasilimali zao, ikiwemo hata kujiondoa katika lindi la umasikini unaonuka.

Popote pale kiongozi wa namna hii, ni sawa na kusema ni kiongozi muflisi ambaye hutambulika muda mwingi kupenda kuruhusu mianya ya rushwa kutawala kila kona, hasa wakati wa utoaji wa huduma muhimu kwa wananchi anaowaongoza.

Katika makala haya napenda kuelezea juu ya kilio cha baadhi ya wananchi wa wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma, dhidi ya Mkuu wao wa wilaya Senyi Ngaga na Mkurugenzi wake Hussein Ngaga, jinsi gani wanavyoiyumbisha wilaya hiyo na kufikia hatua wananchi kukosa imani nao.

Nimefikia hatua ya kuliweka jambo hili hadharani kutokana na mambo kadhaa yanayokera wananchi ambayo viongozi hawa, wamefikia sasa kuchukiwa na watu wanaowaongoza kutokana na kile kinachoelezwa kuwa kupenda kufanya mambo ambayo hayana msingi katika mustakabali mzima, wa maendeleo ya wananchi wa wilaya hiyo.

Jambo la kwanza, kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali ambavyo vimetoa ushirikiano wa karibu kwa mwandishi wa makala haya, vimeeleza kuwa mkuu wa wilaya hiyo ameshindwa kukemea mgogoro ambao unaendelea kufukuta kwa muda mrefu kati ya mkurugenzi huyo na afisa elimu msingi wa wilaya hiyo, Mathias Mkali.

Aidha wanaongeza kuwa licha ya afisa elimu huyo kuonekana kufanya kazi zake vizuri katika kuboresha kiwango cha taaluma wilayani humo, cha kushangaza viongozi hao wamekuwa wakimpiga vita pasipo sababu yoyote ya msingi na kusababisha kuwepo kwa tabaka kubwa, ambalo linaitafuna wilaya kwa kurudisha nyuma maendeleo katika sekta hiyo muhimu.

Wanasema mkuu wa wilaya Ngaga, kukaa kwake kimya pamoja na serikali kukemea migogoro kazini huenda akawa amejenga maslahi yake binafsi, na kusahau jukumu alilopewa na Rais Jakaya Kikwete, wakati anamteua kwenda kutumikia wananchi wa wilaya hiyo kwa kuzingatia kuepuka misingi ya itikadi, rangi au dini na mambo mengine ambayo hayana tija katika jamii.

Wengi kwa nyakati tofauti wanasema, vitendo vinavyofanywa na mkurugenzi huyu huku mkuu huyo wa wilaya kutoingilia kati na kukemea, ni sawa na kushughulika kukomoa wananchi badala ya kubuni na kusimamia maendeleo kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho.

Senyi Ngaga namfahamu vizuri, ni dada yetu ambaye wananchi wa Mbinga tulikuwa na imani naye katika kujenga mshikamano wa kuweza kusukuma mbele gurudumu la maendeleo, lakini kwa haya yanayoendelea sasa anakatisha tamaa wananchi anaowaongoza.