Friday, December 5, 2014

TAARIFA ILIYOSOMWA NA MKAGUZI WA NDANI NA MADIWANI KUNYANG'ANYWA HII HAPA

Na Kassian Nyandindi,
Mbinga.

NDUGU wasomaji wa mtandao huu, sasa tunawaletea taarifa ya Mkaguzi wa ndani juu ya hoja zilizojitokeza katika kikao cha fedha, mipango na uongozi kilichoketi Septemba 25 mwaka huu wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma, na kuwasilishwa katika kikao cha baraza la madiwani la wilaya hiyo Oktoba 27 mwaka huu, kama tulivyosema kuwa katika toleo lililopita kwamba Madiwani walinyang'anywa mara baada ya kusomwa katika baraza hilo.

Taarifa hiyo ambayo imesainiwa na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo Hussein Ngaga ina hoja saba za kumtuhumu Afisa elimu wake wa idara ya elimu msingi wilayani humo, Mathias Mkali kwamba amefanya ukiukwaji mkubwa wa sheria, kanuni na taratibu za fedha za utumishi wa umma, jambo ambalo baadhi ya Madiwani wengi wao walipinga hoja hizo na kusema kuwa jambo hilo halina kweli badala yake ni mambo ambayo yalikwisha kubaliwa na kupitishwa kwenye vikao halali na baraza la madiwani kwa ujumla. (nakala tunazo) 

Katika hali ya kushangaza, taarifa hiyo iligawiwa kwa madiwani katika baraza hilo, ghafla wajumbe husika (Madiwani) baada ya taarifa hiyo kumaliza kuisoma mkaguzi wake wa  ndani, Laston Kilembe na madiwani hao kuipinga, ghafla madiwani walinyang’anywa huku mkurugenzi akisimama mbele ya kikao na kueleza kuwa haijakamilika watapatiwa tena katika kikao kijacho cha baraza hilo.

Sasa taarifa yenyewe ni hii hapa.............................



No comments: