Saturday, December 27, 2014

AFARIKI DUNIA BAADA YA KUUMWA NA NYOKA MWENYE SUMU KALI



Na Steven Augustino,
Tunduru.

BINTI wa miaka mitano Mwanahamis Omary, mkazi wa kijiji cha Kalulu wilayani Tunduru mkoa wa Ruvuma, amekutwa akiwa amefariki dunia baada ya kuumwa na nyoka mwenye sumu kali.

Akizungumzia tukio hilo baba wa mtoto huyo Omary Bakari alisema mkasa huo ulimpata mtoto huyo, wakati akiwa anavuka mto Kalulu kuelekea shambani na kwamba wakati anakumbwa na tatizo hilo alikuwa amefuatana na mama yake mzazi Zainabu Ally.

Baada ya tukio hilo mama yake huyo alipiga kelele za kuomba msaada wa kumpeleka mtoto wao katika zahanati ya kijiji hicho  kwa matibabu zaidi, lakini ilishindikana kwani mtoto huyo alifariki dunia wakiwa njiani kuelekea katika zahanati hiyo.

Hata hivyo nyoka huyo hakuweza kutambuliwa ni wa aina gani, wakati anamuuma mtoto huyo.

No comments: