Sunday, April 1, 2018

DOKTA MAGUFULI AWATAKIA WATANZANIA HERI YA SIKUKUU YA PASAKA


Na Mwandishi wetu, 


RAIS wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dokta John Pombe Magufuli leo Aprili Mosi mwaka huu ameungana na Wakristo wote katika maadhimisho ya Misa Takatifu, ya sikukuu ya Pasaka iliyofanyika kwenye Kanisa la Mtakatifu Joseph, Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kukaribishwa na Padri Venance Tegete kutoa salamu, Dokta Magufuli amewatakia Watanzania wote heri ya sikukuu hiyo huku akitoa wito kwa Watanzania kuendelea kuishi kwa amani, upendo na kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa maendeleo ya Taifa hili.

“Kifo na ufufuko wa bwana wetu Yesu Kristo ukafufue matendo yetu, tuendelee kuijenga amani yetu, upendo wetu na tujenge maendeleo ya Watanzania wote, kwani Kristo alitufundisha upendo miongoni mwetu,


“Kwa hiyo Baba nakushukuru sana kwa kuongoza misa hii, naomba ufikishe shukrani zangu kwa Kardinali Pengo, Maaskofu wote na Watanzania wote tuendelee kusimama pamoja ili tulijenge Taifa letu”, alisema Dokta Magufuli.

Pamoja na mambo mengine, Dokta Magufuli alikuwa ameongozana na mkewe Mama Janeth Magufuli katika misa hiyo ambayo ilikuwa ikiongozwa na Paroko wa Kanisa hilo, Msaidizi wa Parokia ya Mtakatifu Joseph Padri Venance Tegete.

No comments: