Monday, November 21, 2016

NFRA SONGEA YAONGEZA BEI YA KUNUNUA MAHINDI YA MKULIMA

Na Kassian Nyandindi,          
Songea.

SERIKALI kupitia Wakala wa Taifa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Kanda ya Songea mkoani Ruvuma, imelazimika kuongeza bei ya kununua mahindi ya wakulima kufuatia kuwepo kwa ushindani mkubwa kutokana na wanunuzi binafsi wengi wao mkoani humo, kununua mahindi kwa bei kubwa kutoka kwa wakulima wanaozalisha zao hilo.

Aidha kufuatia kuwepo kwa ushindani huo, NFRA imeongeza bei ambapo awali walikuwa wakinunua kwa shilingi 350 kwa kilo na kwamba kuanzia Novemba 7 mwaka huu wananunua mahindi kwa shilingi 580 kwa kilo maeneo ya vijijini na shilingi 600 kwa wale wanaoleta katika kituo kikuu cha Ruhuwiko kilichopo mjini hapa.

Kaimu Meneja wa Wakala huyo Kanda ya Songea, Majuto Chabruma alisema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya maendeleo ya zoezi la ununuzi wa mahindi linavyoendelea katika vituo mbalimbali vilivyotengwa katika wilaya zote za mkoa wa Ruvuma.


Alisema kuwa katika msimu wa mwaka huu serikali ilitenga shilingi bilioni 6.4 kwa ajili ya kununua mahindi tani 12,000 za awali mkoani hapa, huku malengo yakiwa ni kununua tani 22,000 na kwamba bado wanaendelea na kazi hiyo a ununuaji wa mahindi japo hawajafikia lengo husika kutokana na kuwepo kwa ushindani mkubwa wa soko kutoka kwa watu na makampuni binafsi.

Vilevile alibainisha kuwa serikali imeona ni vyema iongeze bei ili kuweza kukabiliana na ushindani huo uliopo kwa lengo la kuweza kufikia malengo iliyojiwekea ya kununua tani 22,000.

Alifafanua kuwa bado Wakala anaendelea na kazi ya kununua mahindi ambayo bado yapo kwa wakulima na wauzaji wengine katika kituo cha Ruhuwiko Songea na amewashauri wakulima mkoani Ruvuma, ambao bado wanayo ziada ya mahindi majumbani kwao kwenda kuuza kwa Wakala huyo wa taifa wa hifadhi ya chakula.

Kadhalika aliongeza kuwa hatua hiyo  itaiwezesha serikali kufikia malengo yake na nchi kwa jumla, ili iweze kuwa na akiba ya chakula cha kutosha na kuwezesha kutoa nafaka hiyo pale patakapojitokeza uhaba wa chakula mahali popote hapa nchini.

Pia Chabruma amewataka wakulima kuwa na kumbukumbu ya kutunza akiba ya chakula na kuacha kuuza yote kwa wafanyabiashara kwani wasipozingatia hilo wataweza kukaribisha njaa majumbani kwao.

Hata hivyo amewakumbusha wakulima mkoani Ruvuma, kuanza maandalizi ya msimu mpya wa kilimo cha zao la mahindi kufuatia mvua tayari zimekwisha anza kunyesha katika baadhi ya maeneo mkoani humo, badala ya kusubiri katikati ya msimu jambo ambalo linaweza kusababisha wakulima kupata mavuno kidogo kutokana na kuchelewa kwa maandalizi ya uzalishaji.

“Sisi kama halmashauri tayari kuna maeneo tumeyatenga kwa ajili ya shughuli za kilimo, idara ya ardhi ipo tayari kutoa kila aina ya ushirikiano kulingana na mwekezaji husika atahitaji kuzalisha zao gani”, alisema.



Pia Hyera  alibainisha kuwa mbali na kutenga maeneo kwa ajili ya shughuli hizo vilevile wanaendelea kuuza maeneo mengine kwa ajili ya viwanja vya ujenzi wa nyumba za makazi na biashara, ambapo viwanja zaidi ya 742.

No comments: