Saturday, April 29, 2017

JENISTA MHAGAMA AKUTANA NA UONGOZI WA SHIVYAWATA DODOMA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama akizungumza jambo wakati wa mkutano wake juzi na viongozi wa SHIVYAWATA kujadili utekelezaji wa majukumu yao katika ukumbi wa ofisi yake Bungeni Dodoma.
Wajumbe wa mkutano wa uongozi wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu nchini wakifuatilia maelekezo kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama wakati wa kikao chao mjini Dodoma.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama akiendesha mkutano na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) walipokutana ofisini kwake Dodoma kujadili utekelezaji wa majukumu yanayowahusu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa SHIVYAWATA mara baada ya kumaliza mkutano wao, kushoto kwake ni Naibu wake Kazi, Ajira na Vijana, Antony Mavunde. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma)

No comments: