Sunday, April 23, 2017

MADIWANI NA WABUNGE WANGING'OMBE WADAIWA KUHAMASISHA WANANCHI KUHARIBU VYANZO VYA MAJI

Uharibifu namna unavyoendelea.
WANANCHI waishio katika tarafa ya Wanging'ombe mkoani Njombe wapo hatarini kukumbwa na baa la njaa, kufuatia eneo la tarafa hiyo kukosa mvua kwa muda mrefu na mazao yao kushindwa kuendelea kustawi kutokana na uharibifu wa mazingira ikiwemo vyanzo vya maji.

Hayo yamebainika kufuatia kikosi kazi kilichoundwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan kutembelea katika eneo hilo na kushuhudia uharibifu uliofanyika.


Ofisa kilimo wa wilaya hiyo Bernadeta Fivao alisema kuwa licha ya serikali kuzuia wananchi kulima kwenye vyanzo vya maji, kumekuwa na baadhi ya wakulima katika tarafa hiyo wakiendelea kulima kwenye vyanzo vya maji kutokana na kukosa chakula.

Baadhi ya watumishi wa halmashauri ya wilaya Wangingombe wameeleza wakidai kuwa Madiwani na Wabunge ndiyo wamekuwa wakihamasisha wananchi kuendelea kuharibu vyanzo hivyo vya maji. 


Hivi sasa eneo la tarafa ya Wangingombe limekuwa likikabiliwa na tatizo kubwa la uhaba wa maji kutokana pia na kuwepo wa vitendo vya ufugaji holela pamoja uharibifu wa vyanzo hivyo kwa kuendesha kilimo cha mazao kando kando ya mito.

No comments: