Friday, May 24, 2013

SAFARI YA MWISHO YA MTUNZI MAARUFU WA VITABU CHINUA ACHEBE



















Na Halima Kambi,

MAELFU ya waombolezaji wamehudhuria katika mazishi ya mtunzi mashuhuri wa vitabu barani Afrika, Chinua Achebe yaliyofanyika karibu na nyumbani kwa familia yake mjini Ogidi, mji mdogo kwenye vilima vya jimbo la Anambra.

Mwili wa marehemu Achebe uliwasili nchini Nigeria siku ya Jumatano, kutokea mjini Bostan, Marekani ambako alikuwa amefariki dunia.

Mazishi hayo yalifanyika  katika kanisa la mtakatifu Philip la Anglikana, na kuhudhuriwa na waombolezaji ambao wamepewa mualiko maalum  huku wengine wakiwa nje wakisikiliza ibada hiyo, baada ya kuwekewa spika.


Rais Goodluck Jonathan ni miongoni mwa waombolezaji waliohudhuria mazishi ya mtunzi huyo mashuhuri wa vitabu barani Afrika, ambapo katika mazishi hayo kulikuwa na ulinzi mkali katika mji mdogo wa Ogidi nchini humo.

Mwandishi huyo mashuhuri alifariki mjini Boston, Marekani akiwa na umri wa miaka 82 baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Hayati Achebe anasifika sana kwa kuwa mwanzilishi wa fasihi ya kiafrika kwa luga ya kiingereza.

Kitabu chake alichokiandaa cha kwanza mwaka 1958, Things Fall Apart, ambacho kilizungumzia sana athari za ukoloni barani Afrika, aliweza kuuza zaidi ya vitabu milioni kumi.

Mwandishi huyo na msomi aliendelea na uandishi wake wa kuandika vitabu vingine 20 baadhi vikikosoa wanasiasa, na kile alichokitaja kama ukosefu wa uongozi nchini Nigeria.

Alikuwa anaishi nchini Marekani tangu mwaka 1990, baada ya kupata ajali ya barabarani kumjeruhi kiasi cha kumpa ulemavu.






No comments: